Roho ya Umasikini ni nini na inatendaje kazi?

by Admin | 3 March 2024 08:46 pm03

Swali: Roho ya umasikini ipoje na inatenda kazi kwa namna gani, na inawezaje kumtoka mtu?


“Roho ya umasikini” ni roho inayomshusha mtu kiuchumi, hata kumfanya asifike kule anakotaka kufika kimaendeleo.

Roho hii inapomvaa mtu inamfanya wakati mwingine awe katika hali ya mahitaji kupindukia na hata kuwa katika hali ya madeni mazito.

Kibiblia watu wa Mungu umasikini si sehemu yao.. Ingawa kuna vipindi ambavyo Mungu anaweza kumpitisha mtoto wake kuonja umasikini kwa muda ili kumfundisha baadhi ya mambo, ambayo yatamfaa baadaye atakapobarikiwa.

Na urefu wa kipindi hicho cha madarasa ya Mungu kinategemea mtu na mtu. Wapo ambao watadumu katika hiko kipindi kwa muda mrefu kidogo lakini baadaye watatoka huko, na wapo ambao watadumu katika kipindi kifupi na baadaye watatoka huko na kupewa pumziko la faraja ya Bwana.

Lakini kwa ujumla Mkristo hajapewa umasikini wa kudumu kama sehemu maisha yake…au labda mtu huyo atake mwenyewe kujifanya maskini kwa nafsi yake au kwaajili ya Bwana.

Mtu anayejifanya maskini kwa ajili ya Bwana ni yule ambaye Mungu anamfungulia milango ya kupata vingi lakini kila anachokipata anakitoa na hivyo muda wote anakuwa katika hali ya kutokuwa na vingi…(Mtu wa namna hii ni maskini ingawa ni tajiri).

Mtu huyu anakuwa hawezi kuona furaha au Amani akiwa na viwili wakati mwingine hana hata kimoja. Mtu wa namna hii anakuwa anajifanya mwenyewe maskini kwaajili ya Bwana na kwa taji yake mbinguni, ikiwa anafanya hivyo kwa dhamiri njema na si kama sheria.

Mfano wa watu waliojifanya wenyewe kuwa maskini ingawa wangeweza kuwa matajiri ni Yohana Mbatizaji na BWANA WETU YESU KRISTO.

2Wakorintho 8:9 “Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.

Na pia wapo ambao walikuwa matajiri na wakadumu na utajiri wao, mfano wa hao ni Ibrahimu na Ayubu..

Sasa hakuna agizo lolote maalumu katika biblia kuwa ni sheria tujifanye kuwa maskini, kama alivyokuwa Bwana au Yohana Mbatizaji,  mtu akijifanya hivyo basi iwe kwa nafsi yake na Mungu wake, na si amri wala agizo.

Lakini pamoja na hayo, upo umaskini mwingine ambao hauletwi na Mungu bali unaletwa na adui shetani. Mara nyingi umasikini huu ni ule unaompata mtu anapokuwa nje ya KRISTO (Maana yake hajaokoka).. au aliyeokoka lakini amepungukiwa na baadhi ya Maarifa ambayo yangemsaidia kusogea kimaisha.

Sasa ni njia gani za kushughulika na roho ya umaskini unaoletwa na adui shetani?

     1. KUOKOKA

Unapookoka kikweli kweli kwa kumaanisha, basi roho zote za adui zinazochochoe na kutengeneza umaskini maishani mwako zinaondoka, na hivyo maisha yako kutengenezeka upya kama yalikuwa yameshaharibiwa na pepo la umasikini.

     2. KUOMBA

Maombi ni silaha tosha kwa kila mwamini, na maombi ni ULINZI, Kama umeshuhudiwa kuwa hali unayopitia sio ya kawaida na wala haitokani na MUNGU, basi ni wakati wa kuingia vitani katika maombi, kuvunja na kukemea kila roho yote inayotaka kujiinua kinyume na maendeleo yako.

    3. PATA MAARIFA.

Kama umeshaokoka na tena ni mwombaji sana lakini bado unaona hali hiyo ya umasikini inadumu muda mrefu, basi huenda Mungu kashakufungulia milango mbele yako ili upige hatua, lakini milango hiyo huioni aidha kutokana na kupungukiwa na MAARIFA, sawasawa na Hosea 4:6.

Hivyo tia bidii katika kutafuta maarifa ya jinsi ya kujiendeleza mbele kupitia kanuni za kibiblia. (Soma sana biblia, na pia sikiliza mafundisho mbalimbali kutoka kwa watumishi wa kweli wa Mungu yahusuyo namna ya kujiendeleza, vile vile ongeza ujuzi katika kile ukifanyacho).

Kupitia njia hizo tatu basi utaweza kujifungua kutoka katika kifungo cha umasikini.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

Mbona ni maskini tu huwa ndio wanaolipuka mapepo, na sio matajiri?

UKITAKA KUMFUATA YESU NI SHARTI UACHE VYOTE!

Elewa maana ya Mithali 18:23 Maskini hutumia maombi; Bali tajiri hujibu kwa ukali. 

 Je kualikwa kwenye sherehe za watu ambao si wakristo ni dhambi?

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2024/03/03/roho-ya-umasikini-ni-nini-na-inatendaje-kazi/