Ni uchafu gani unaozungumziwa katika Wagalatia 5:19?

by Admin | 30 April 2024 08:46 pm04

Jibu: Turejee,

Wagalatia 5:19  “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, UCHAFU, ufisadi,

20  ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,

21  husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu”.

Dhambi zote ni “uchafu” lakini zipo dhambi ambazo ni “chafu Zaidi”, hizo ndizo zinazoitwa “Uchafu” Mfano wa hizo ni zile zilizotajwa katika Mambo ya Walawi 18 na 20(Dhambi za kulala na mnyama na ndugu wa karibu).

Walawi 18:23 “Wala usilale na mnyama ye yote, ili kujitia unajisi kwake; wala mwanamke asisimame mbele ya mnyama ili kulala naye; NI UCHAFUKO”.

Walawi 20:12 “Na mtu mume akilala na mkwewe mwanamke wote wawili hakika watauawa; wamefanya yaliyo UCHAFUKO; damu yao itakuwa juu yao”.

Utaona dhambi nyingine zimetajwa tu kama ni “Machukizo” mfano lakini hizi zimetajwa kama “Uchafuko” maana yake zimezidi machukizo.. Ni uchafu mkuu mbele za Mungu.

Kulala na Mnyama, ni uchafu, vile vile kulala na mama mkwe au baba mkwe ni uchafu..na wachafu wote hawataurithi uzima wa milele sawasawa na maandiko hayo.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni  ipi?

Kwanini Mungu awachome watu kwenye ziwa la moto na hali yeye ndiye aliyewaumba?

Ninyi ni chumvi ya dunia, Andiko hilo lina maana gani?

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

Pesa za bindoni ni nini?(Marko 6:8)

Rudi Nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2024/04/30/ni-uchafu-gani-unaozungumziwa-katika-wagalatia-519/