Sakitu ni nini? (Ayubu 38: 29)

by Admin | 26 June 2024 08:46 pm06

Sakitu ni BARAFU INAYOANGUKA KUTOKA JUU, ambayo mara nyingi inafunika mimea, au barabara au nyumba katika nchi zenye baridi kali. (Tazama picha juu).

Ayubu 38: 29 “Barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na SAKITU YA MBINGUNI ni nani aliyeizaa?

30 Maji hugandamana kama jiwe, Na uso wa vilindi huganda kwa baridi”.

Neno hili limeonekana pia katika Kutoka 16:14, ambapo biblia inaonyesha ile MANA ilifanan na sakitu kimwonekano (ingawa haikuwa sakitu).

Kutoka 16:14 “Na ulipoinuka ule umande uliokuwa juu ya nchi, kumbe! Juu ya uso wa bara kitu kidogo kilichoviringana, kidogo kama SAKITU juu ya nchi.

15 Wana wa Israeli walipokiona, wakaambiana, Nini hiki? Maana hawakujua ni kitu gani. Musa akawaambia, Ndio mkate ambao Bwana amewapa ninyi, mle”

Ingawa Mana haikuwa sakitu (barafu) lakini ilibeba tabia za sakitu, kwani Sakitu (barafu) inapopigwa jua inayeyuka, na ile Mana ilikuwa ina tabia hiyo hiyo, jua lilipozuka ilikiyeyusha.

sakitu ni mana

Kutoka 16:21 “Basi wakaokota asubuhi baada ya asubuhi, kila mtu kama ulaji wake ulivyokuwa; na hapo jua lilipokuwa ni kali, kikayeyuka”.

Kujua ni ufunuo gani uliopo nyuma ya MANA, fungua hapa >>>MANA ILIYOSHUSHWA KUTOKA MBINGUNI.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

USIWE NA TAMAA YA CHAKULA KINGINE.

JE UMEUFIKIA ULE UTUKUFU HALISI WA MANA? 

NYOTA YA ASUBUHI.

NI NANI ATAKAYETUTENGA NA UPENDO WA KRISTO?

MWONGOZO WA MAOMBI YA ASUBUHI.

Rudi Nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2024/06/26/sakitu-ni-nini-ayubu-38-29/