Biblia inasema nini kuhusu mtu ‘Mwenye kujipendekeza (Mithali 29:5)

by Admin | 8 October 2024 08:46 am10

SWALI: Naomba kufahamu ujumbe ulio katika Mithali 29:5

‘Mwenye kujipendekeza kwa jirani yake, Hutandika wavu ili kuitega miguu yake’.

JIBU: Mithali hii inazungumzia madhara yanayoibuka katika tabia ya kujipendekeza.

Kujipendekeza ni kitendo cha mtu kumthaminisha mtu, hata kama alikuwa hastahili sifa hizo, ili tu upate kitu Fulani kutoka kwake. Kumthaminisha kunaweza kuwa kumsifia, au kumpongeza, au kumzungumzia mema yake kupita kiasi, au kueleza mabaya ya wengine kwa huyo mtu, n.k.

 Na yote hayo hayawi kwa lengo la kuuthamini kweli uzuri wa Yule mtu, hapana bali  ni aidha upate kupendwa wewe zaidi ya wengine, au usaidiwe, au upewe cheo,  au kipaumbele Fulani. Hata kama utaona mabaya yake huwezi kumwambia kwasababu, huna lengo la kusaidia bali upate matakwa yako tu.

Sasa  hilo ni kosa, matokeo ya hilo biblia inatuambia “unamtandikia wavu ili kuitega miguu yake”. Yaana unampeleka kwenye mtego au aungamivu wake kabisa.  Hii ni kweli, tunaona hata viongozi wengi wa nchi wameponzwa na wasaidizi wao wa karibu,na matokeo yake wakaiharibu  nchi, kwasababu tu ya kupokea sifa za uongo kutoka kwao, kwamba wanafanya vema, wanawajibiki vizuri n.k..  Kama ilivyokuwa kipindi kile cha Mfalme Sedekia na wale manabii wa uongo wajipendekezao, walimtabiria uongo, lakini Yeremia alimweleza mfalme ukweli  hawakutaka kumsikiliza. Matokeo yake Mfalme Sedekia akaingia katika matatizo makubwa ya kutobolewa macho na kupelekwa utumwani, hiyo yote ni kwasababu alikaa na manabii wajipendekezao (Yeremia 34-41), kama tu ilivyokuwa Kwa Mfalme Ahabu naye na manabii wake mia nne wa uongo.

Hii ni kutufundisha nini?

Hasaa biblia hailengi, tuwe makini na watu wajipendekezao. Hapana, kwasababu wakati mwingine si rahisi kuwatambua, inahitaji neema ya Mungu. Lakini inalenga hasaa katika upande wetu , kwamba sisi tujiepushe na ‘tabia ya kujipendekeza”. Kwasababu tunaweza kudhani tunatafuta faidi yetu tu wenyewe, lakini kumbe tunamsababishia madhara Yule mtu ambaye tunajipendekeza kwake. Tunategea wavu mbaya sana, aanguke na kupotea kabisa, na huo si upendo.

Itakusaidia nini akutendee mema, halafu yeye aangamie?

Hivyo, pastahilipo kweli kusifia tusifie, lakini si kwa lengo la kujipendekeza, kwasababu tukienda huko, tunatenda dhambi kubwa zaidi. Hiyo ndio maana ya hivyo vifungu, tufikiriapo kujipendekeza, tuone kwamba ni watu wasio na hatia tunawategea wavu waangamie.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TUZIJARIBU HIZI ROHO.

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

USIJISIFIE KARAMA KWA UONGO.

Rudi Nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2024/10/08/mwenye-kujipendekeza-mithali-295/