by Devis | 4 June 2025 08:46 am06
Maisha Mapya ya wokovu yanasukumwa na maombi. Kama Neno ni chakula, basi maombi ni maji. Vilevile huwezi tenganisha maisha ya wokovu na uombaji.
Ni tendo la kuongea na Mungu, lakini pia kumsikia. Maombi sio maneno matupu tu, au utaratibu wa kidini, bali ni mahusiano halisi kati ya sisi na Mungu.
Yeremia 33:3
[3]Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua.
Maandiko hayatoi ukomo wa maombi. Zaidi sana yanasisitiza tuombe kila wakati na bila kukoma.
1Wathesalonike 5:17 ombeni bila kukoma;
Waefeso 6:18 kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;
Hivyo Maombi ni tendo endelevu la wakati wote.
Mathayo 26:41 Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.
Luka 3:21 Ikawa, watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu naye amebatizwa, naye anaomba, mbingu
zilifunuka
Mathayo 17:20 Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.
21 [Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]
Wafilipi 4:6 Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.
Zipo aina mbalimbali za maombi, ili kufahamu kwa kina bofya hapa >> KUNA AINA NGAPI ZA MAOMBI?
Ramani kuu ya maombi tulishafundishwa na Bwana Yesu Kristo. Ambayo ndio ile Sala, ijulikanayo kama “Sala ya Bwana”. Hivyo kufahamu namna ya kuiomba fungua hapa >>>> Namna bora ya kuiomba sala ya Bwana
Miongozo mingine itakayokusaidia kutanua upeo wako wa uombaji kwa lengo la ukuaji wa kiroho Bofya hapa >>> MWONGOZO WA MAOMBI YA KUJIKUZA KIROHO.
Haya ni mafundisho, mengine yatakayokusaidia kujua kwa undani kuhusu maombi;
Kuomba katika roho ni kupi? na je nifanye nini ili niweze kuomba hivyo?
MWONGOZO WA MAOMBI YA ASUBUHI.
JINSI YA KUVURUGA MIPANGO YA MUNGU.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Source URL: https://wingulamashahidi.org/2025/06/04/maombi-kama-sehemu-ya-maisha-ya-mwamini-mpya/
Copyright ©2025 Wingu la Mashahidi unless otherwise noted.