Maombi kama sehemu ya maisha ya mwamini mpya.

by Devis | 4 June 2025 08:46 am06

Maisha Mapya ya wokovu yanasukumwa na maombi. Kama Neno ni chakula, basi maombi ni maji. Vilevile huwezi tenganisha maisha ya wokovu na uombaji.

Maombi ni nini?

Ni tendo la kuongea na Mungu, lakini pia kumsikia. Maombi sio maneno matupu tu, au utaratibu wa kidini, bali ni mahusiano halisi kati ya sisi na Mungu.

Yeremia 33:3

[3]Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua.

Je! tunapaswa tuombe wakati gani?

Maandiko hayatoi ukomo wa maombi. Zaidi sana yanasisitiza tuombe kila wakati na bila kukoma.

1Wathesalonike 5:17 ombeni bila kukoma;

Waefeso 6:18 kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;

Hivyo Maombi ni tendo endelevu la wakati wote.

Faidi za kuomba kwa mwamini.

i) Tunashinda  majaribu:

Mathayo 26:41 Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.

ii) Tunajazwa Roho

Luka 3:21 Ikawa, watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu naye amebatizwa, naye anaomba, mbingu

zilifunuka

iii) Tunatatua Matatizo yote:

Mathayo 17:20 Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.

21 [Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]

iv) Tunapewa haja zetu:

Wafilipi 4:6 Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.

Aina za maombi.

Zipo aina mbalimbali za maombi, ili kufahamu kwa kina bofya hapa >>   KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

Je! tunapaswa tuombaje?

Ramani kuu ya maombi tulishafundishwa na Bwana Yesu Kristo. Ambayo ndio ile Sala, ijulikanayo kama “Sala ya Bwana”. Hivyo kufahamu namna ya kuiomba fungua hapa >>>>  Namna bora ya kuiomba sala ya Bwana

Miongozo mingine itakayokusaidia kutanua upeo wako wa uombaji kwa lengo la ukuaji wa kiroho  Bofya hapa >>> MWONGOZO WA MAOMBI YA KUJIKUZA KIROHO.

Haya ni mafundisho, mengine yatakayokusaidia kujua kwa undani kuhusu maombi;

IFAHAMU NGUVU YA MAOMBI.

Kuomba katika roho ni kupi? na je nifanye nini ili niweze kuomba hivyo?

MWONGOZO WA MAOMBI YA ASUBUHI.

KANUNI YA KUOMBA NA KUPOKEA.

JINSI YA KUVURUGA MIPANGO YA MUNGU.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2025/06/04/maombi-kama-sehemu-ya-maisha-ya-mwamini-mpya/