Ipi tofuati ya Andiko na Neno.

by Devis | 9 June 2025 08:46 am06

Swali: Huwa tunasema.. “tusome maandiko” na wakati mwingine “tusome Neno”..ipi tofauti ya maneno haya mawili?.


Jibu: Tuanze na Neno au Neno la Mungu.

“Neno” ni sauti ya MUNGU yenye ujumbe inayokuja kwa mtu kwa  njia ya maono au ndoto au njozi..

Kwamfano katika biblia utaona lugha iliyotumika kwa manabii wote waliojiliwa na sauti ya Mungu iliyobeba ujumbe ni hiyo ya “Neno la Mungu”

Mwanzo 15:1 “Baada ya mambo hayo NENO LA BWANA likamjia Abramu katika njozi, likinena, Usiogope, Abramu, Mimi ni ngao yako, na thawabu yako kubwa sana.

Soma pia  1Wafalme 17:8, Isaya 38:4, Yeremia 1:11, Ezekieli 1:3, Ezekieli 12:21, Hosea 1:1, Yona 1:1, Mika 1:1, Sefania 1:1 n.k 

Hata sisi wakati mwingine tunapotaka kuzungumza na mtu, tunaweza kutumia lugha hiyo kwa kumwambia “nina neno nataka kusema nawe”… au kama kuna mtu amekuambia jambo unaweza kusema “mtu Fulani kaniambia neno”.. kwahiyo ni hivyo hivyo hata katika biblia, Neno la Mungu ni sauti ya MUNGU.

Sasa kama “Neno” tafsiri yake ndio hiyo, vipi kuhusu “Andiko”?

Andiko ni Neno la Mungu lililo katika maandishi… Kwamfano; hilo Neno lililomjia Abramu, kwake yeye ni Neno la Mungu lakini kwetu sisi ni andiko, ndio maana tunalisoma.. Na Nguvu ya andiko na Neno ni ile ile.

Hivyo maneno ya Mungu yote yaliyoandikwa katika Biblia ni “MAANDIKO”.. Hata wewe maneno yako unayoyasema unaweza kuyaandika katika kitabu, na yakawa ni maandiko kwasababu ni maneno yaliyoandikwa.. Hali kadhalika, kila Neno la Mungu kwenye Biblia ni andiko.

Hivyo mtu anayesema “tusome maandiko” na Yule anayesema “tusome Neno la Mungu” ni kitu kimoja.. na nguvu ni ile ile..

Na kila Andiko lenye pumzi ya Mungu linafaa kwa mafundisho, kuonya, kuongoza na kuadibisha..

2Timotheo 3:16 “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;

17 ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema”

Kwa urefu kuhusiana na kazi ya MAANDIKO inayofanya kwa mtu fungua hapa >>MAMBO MANNE(4) YAFANYAYO NENO LA MUNGU.

Je umempokea YESU?, Umebatizwa katika ubatizo sahihi?..una uhakika Bwana YESU akirudi unaenda naye?.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

EPUKA KUJIFANYA HUJUI.

MANENO YA MUNGU YANAPINDULIWAJE?

TUUTAZAME PIA MWISHO WA UJENZI WETU.

ZIFAHAMU KARAMA 9 ZA ROHO MTAKATIFU NA UTENDAJI KAZI WAKE.

NI NANI TUNAPASWA TUMWONE ZAIDI KILA TUSOMAPO BIBLIA?

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2025/06/09/ipi-tofuati-ya-andiko-na-neno/