by Devis | 15 July 2025 08:46 pm07
Kuseta kama ilivyotumika kwenye maandiko maana yake ni kukiharibu kitu, aidha kwa kukiponda, kukikanyaga, au Kukivunja vipande vipande.
Kwamfano kwenye maandiko kama haya tunaweza kuona neno hilo..
Warumi 16:19-20
[19]Maana utii wenu umewafikilia watu wote; basi nafurahi kwa ajili yenu, lakini nataka ninyi kuwa wenye hekima katika mambo mema, na wajinga katika mambo mabaya.
[20]Naye Mungu wa amani atamseta Shetani chini ya miguu yenu upesi.
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi. [Amina.]
Hapa Mungu anaonyesha kwamba pale tunapokuwa mbali na mambo mabaya ndivyo anavyomponda shetani chini ya miguu yetu..
Kuonyesha kuwa njia kuu ya kumshinda shetani sio kumkemea bali ni kujitenga na mambo maovu.
Vifungu vingine ni kama hivi..
Zaburi 110:5
[5]Bwana yu mkono wako wa kuume; Ataseta wafalme, Siku ya ghadhabu yake.
Hapa Mungu anaonyesha ukali wa ghadhabu yake juu ya watu waovu..hata wale wanaoonekana ni wakuu, hawataikwepa hasira yake atawaharibu kwa kuwaponda- ponda.
kwa hitimisho ni kuwa kuseta ni kuharibu kabisa Kabisa ..Na Mungu amekusudia kufanya hivyo sio kwetu bali kwa shetani… Ni sisi tu kuishi maisha yanayomlingana yeye ikiwa tayari tumeshaokoka…Lakini ikiwa ni kinyume na hapo tutaingia katika mkondo huo huo wa shetani, wa kuharibiwa endapo hatutamwamini Yesu Kristo leo.
Je upo tayari kumpokea Yesu leo? Kama ni ndio basi bofya hapa >> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Source URL: https://wingulamashahidi.org/2025/07/15/kuseta-ni-nini/
Copyright ©2025 Wingu la Mashahidi unless otherwise noted.