YESU alimaanisha nini aliposema “mkono wako ukikukosesha ukate?

by Admin | 1 September 2019 08:46 pm09

Mathayo 5:29 Jicho lako la kuume likikukosesha, ling’oe ulitupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum.
30 Na mkono wako wa kuume ukikukosesha, ukate uutupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum.


JIBU: Hapo ni kama inavyojieleza, kiungo kinaweza kikawa kiungo kama kiungo cha mwilini, hususani viungo vya uzazi hivyo ndivyo vinavyowakosesha wengi,…lakini pia kinaweza kikawa kiungo cha nafsi yako, mfano ndugu, marafiki, jamii, kazi, fani, n.k….Yaani kwa ujumla chochote kile kinachoweza kukufanya usiwe na uhusiano mzuri na Mungu, unapaswa ukiweke kando, mana ni heri kufanya hivyo uokoke kuliko kuwa nacho kisha ukaishia kuzimu.

Kwasababu Bwana Yesu alishasema katika,

Mathayo 16: 25 Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona.
26 Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?.

Ubarikiwe!

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Mada zinazoendana:

DHAMBI ZINAZOTANGULIA NA ZINAZOFUATA.

‘’MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI’’..NA NDIVYO ILIVYO KWA UASHERATI

LULU YA THAMANI.

KWANINI USIICHAGUE TUZO ISIYOHARIBIKA?

ALIPO NA ATAKAPOKUWEPO BIBI-ARUSI WA YESU KRISTO.


Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2019/09/01/mkono-wako-wa-kuume-ukikukosesha-ukate-uutupe-mbali-nawe/