“Nami nikiinuliwa juu ya nchi,NITAWAVUTA WOTE KWANGU”(Yohana12:32).

by Admin | 1 September 2019 08:46 pm09

SWALI: Nini maana ya haya maandiko “Nami nikiinuliwa juu ya nchi,NITAWAVUTA WOTE KWANGU”(Yohana12:32)?.

JIBU: Tunaona wana wa Israeli baada ya kumkosa Mungu kule jangwani, Bwana aliwapiga kwa pigo la nyoka wa moto, na ndipo Musa akaambiwa atengeneze nyoka wa shaba na kumwinua juu ya nchi, ili kila amtazamaye apate kupona. Sasa Bwana wetu Yesu Kristo alifananishwa na yule nyoka wa shaba juu ya ule mti, kwamba na yeye aliinuliwa juu (Pale Kalvari) ili kila amtazamaye (kwa macho ya rohoni na kumwamini) apate uzima wa milele, na ndio maana alisema katika…

Yohana 3:14 ” Na kama vile Musa alivyomwinua yule nyoka jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa;

15 ili kila mtu aaminiye awe na uzima wa milele katika yeye.”

Kwahiyo hapo Bwana aliposema “Nami nikiinuliwa juu ya nchi,NITAWAVUTA WOTE KWANGU” alimaanisha kuwa “baada ya kusulibiwa pale msalabani” kwa ajili ya dhambi ya ulimwengu, itaachiliwa nguvu kubwa ya watu wengi kuvutwa kwake, na ndio maana ukiendelea kusoma mstari unaofuata utaona ameweka wazi kuwa kuinuliwa kunahusu mauti ya mwili wake..

Yohana 12:32 “Nami nikiinuliwa juu ya nchi, nitawavuta wote kwangu.
33 Aliyanena hayo akionyesha ni mauti gani atakayokufa”.

Ubarikiwe.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Mada zinazoendana:

MUNGU NDIYE ANAYEISHAWISHI MIOYO.

MWINUE YESU KRISTO KATIKA MAISHA YAKO.

DAMU YA YESU INANENAJE MEMA KULIKO YA HABILI?

AYUBU 28 : HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?

MAJI YA UZIMA.

UWEZA WA MUNGU UNAONEKANA WAPI?


Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2019/09/01/nami-nikiinuliwa-juu-ya-nchinitawavuta-wote-kwangu/