JE MUSA ALIFIA WAPI?

by Admin | 9 October 2019 08:46 pm10

Jibu la swali hili tunalipata katika kitabu cha Kumbukumbu la Torati 34, 

Kumbukumbu 34:1 “Musa akapanda kutoka uwanda wa Moabu mpaka mlima Nebo, hata kilele cha Pisga kukabili Yeriko. Bwana akamwonyesha nchi yote ya Gileadi hata Dani;

2 na Naftali yote, na nchi ya Efraimu na Manase, na nchi yote ya Yuda, mpaka bahari ya magharibi;

3 na Negebu, na uwanja wa bonde la Yeriko, mji wa mitende, hata mpaka Soari.

4 Bwana akamwambia, Hii ndiyo nchi niliyowaapia Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, nikisema, Nitawapa wazao wako. Basi nimekuonyesha kwa macho yako, lakini hutavuka huko.

5 Basi Musa, mtumishi wa Bwana, akafa huko, katika nchi ya Moabu, kwa neno la Bwana.

6 Akamzika bondeni, katika nchi ya Moabu, kukabili Beth-peori; lakini hapana mtu ajuaye kaburi lake hata leo”.

Moabu kwa sasa ni maeneo ya Magharibi mwa Nchi ya JORDANI, Na Mungu alificha kaburi la Musa, ili watu wasipagueze mahali pale mahali pa ibada,  na kufanya ibada za sanamu na kufanya machukizo mbele za Mungu.


Mada Nyinginezo:

FIMBO YA HARUNI NI NINI?

NABII MUSA NI NANI?.

JE! MWANADAMU WA KWANZA KUUMBWA NI YUPI MZUNGU MWAFRIKA AU MCHINA?

NI RAHISI KWA NGAMIA KUPENYA KATIKA TUNDU LA SINDANO, JE! NI SINDANO IPI HIYO INAYOZUNGUMZIWA?


Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2019/10/09/je-musa-alifia-wapi/