KUOTA UNATOKA DAMU YA HEDHI.

by Admin | 8 August 2020 08:46 am08

kuota unatoka damu ya hedhi inamaanisha nini kibiblia?


Yapo mambo mawili;

Jambo la kwanza unapaswa ujue asilimia kubwa ya ndoto tunazoziota kila siku, si zote zina tafsiri ya rohoni kukusaidia, naweza kusema asilimia hata 90 ya unavyoviota kila siku vinatokana na ubongo wako wenyewe.

Ubongo wako Mungu kauumba kwa namna ambayo unaweza kuhifadhi kumbukumbu ya mambo unayofanya karibu kila siku, au mambo ambayo ulishawahi kuyapitia au mazingira ambayo ulishawahi kuyoana au kuwepo..

Kwahiyo katikati ya hayo yote, Ubongo wako utajiundia matukio na kuyachezesha akilini mwako wakati ukiwa umelala.

Biblia inasema hivi..

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi;….”

Umeona? Kwamfano ikiwa wewe kazi yako ni uvuvi na mara nyingi huwa unakesha baharini kuvua, kuota ndoto unajiona unavua au unatengeneza nyavu, itakuwa ni kitu cha kawaida kwako kujirudia rudia mara kwa mara, halikadhalika kwa  mpishi, au mwalimu, au mjenzi, kuota anafanya mojawapo ya ujuzi wake, litakuwa ni jambo la kawaida sana.

Vilevile katika hizo zipo ndoto ambazo zinaotwa na jinsia husika tu, kwamfano kuota unajifungua, hizi ndoto huwezi sikia zikiotwa na mwanaume, vivyo hivyo na kuota unatoka damu ya hedhi ni ndoto zinazowahusu wanawake peke yao, mwanaume hawezi kuota hivyo kwasababu jambo kama hilo hajawahi kulipitia katika Maisha yake yote,

Kwahiyo ndoto kama hii ikikujia isikusumbue sana. Elewa ni ndoto itokanayo na mazingira unayopitia.

Lakini pia jambo la pili ni kuwa.. Mungu anaweza kuzungumza na sisi, pia kwa njia hizo hizo za ndoto za mazingira yetu ya kila siku.

Kwamfano katika biblia utaona kulikuwa na wafungwa wawili waliokuwa gerezani na Yusufu, mmoja alikuwa anafanya kazi ya kumnywesha mfalme, na wa pili alikuwa ni mpishi. Siku moja wote wawili wakaota ndoto, na ndoto walizoota zililandana na mazingira yao ya kazi.. Lakini zilikuwa zimebeba ujumbe mzito kutoka kwa Mungu.

Mwanzo 40:5 “Wakaota ndoto wote wawili, kila mtu ndoto yake usiku mmoja, kila mtu kwa tafsiri ya ndoto yake, mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri waliofungwa gerezani. 

6 Yusufu akawajia asubuhi, akawaona wamefadhaika. 

7 Akawauliza hao maakida wa Farao, waliokuwa pamoja naye katika kifungo, nyumbani mwa bwana wake, akisema, Mbona nyuso zenu zimekunjamana leo? 

8 Wakamwambia, Tumeota ndoto wala hapana awezaye kuifasiri. Yusufu akawaambia, Kufasiri si kazi ya Mungu? Tafadhalini mniambie. 

9 Mnyweshaji mkuu akamhadithia Yusufu ndoto yake; akamwambia, Katika ndoto yangu nimeota, uko mzabibu mbele yangu. 

10 Na katika mzabibu mlikuwa na matawi matatu, nao ulikuwa kana unamea, unachanua maua, vishada vyake vikatoa zabibu zilizoiva. 

11 Na kikombe cha Farao kilikuwa mkononi mwangu, nikazitwaa zabibu, nikazikamua katika kikombe cha Farao, nikampa Farao kikombe mkononi mwake. 

12 Yusufu akamwambia, Tafsiri yake ndiyo hii. Matawi matatu ni siku tatu. 

13 Baada ya siku tatu Farao atakiinua kichwa chako, atakurudisha katika kazi yako; nawe utampa Farao kikombe mkononi mwake, kama desturi ya kwanza, ulipokuwa mnyweshaji wake……..

16 Mkuu wa waokaji alipoona ya kwamba hiyo tafsiri ni ya mema, akamwambia Yusufu, Mimi kadhalika nilikuwa katika ndoto yangu, na tazama, ziko nyungo tatu za mikate myeupe juu ya kichwa changu. 

17 Na katika ungo wa juu, mlikuwa na kila namna ya chakula kwa Farao, kazi za mwokaji; ndege wakavila katika ungo juu ya kichwa changu. 

18 Yusufu akajibu, akasema, Tafsiri yake ndiyo hii Nyungo tatu ni siku tatu..

Ukiendelea kusoma pale utaona ni kweli, mambo hayo yaliwakuta vilevile kama Yusufu alivyowatafsiria.

Unaona sasa “point” hapo ni kuwa walichoota kiliendana na kazi zao au mazingira yao ya kila siku, yule wa kwanza alikuwa ni mnyweshaji wa mfalme akajiona anaweka divai mezani pa mfalme, kutoka katika mzabibu, ..Yule mwingine ni mpishi, aliona mikate kichwani pake.

Vivyo hivyo na wewe kuota unatoka damu ya hedhi, mara mara,  na tena kama ndoto hiyo inakujia kwa uzito Fulani basi ujue upo ujumbe mzito Mungu wa Mungu nyuma yake.. Na ujumbe huo unatoka kwenye biblia.

Sasa ipo Habari moja ambayo pengine ulishawahi kuisikia, lakini leo hii nataka uifuatilie tena kwa ukaribu. Habari yenyewe ni kuhusu yule mwanamke aliyekuwa anatokwa na damu kwa muda mrefu wa miaka 12. Tusome;

Luka 8:43  “Na mwanamke mmoja, ambaye ametokwa na damu muda wa miaka kumi na miwili, [aliyekuwa amegharimiwa mali zake zote kwa kuwapa waganga] asipate kuponywa na mtu ye yote,

44  alikwenda nyuma yake, akaugusa upindo wa vazi lake; na mara hiyo kutoka damu kwake kulikoma.

45  Yesu akasema, Ni nani aliyenigusa? Basi, watu wote walipokana, Petro alimwambia, Bwana mkubwa, makutano haya wanakuzunguka na kukusonga.

46  Yesu akasema, Mtu alinigusa, maana naona ya kuwa nguvu zimenitoka.

47  Yule mwanamke, alipoona ya kwamba hawezi kusitirika akaja akitetemeka, akaanguka mbele yake, akamweleza mbele ya watu wote sababu yake ya kumgusa, na jinsi alivyoponywa mara.

48  Akamwambia Binti, imani yako imekuponya; enenda zako na amani”.

Umeona mwanamke huyu, tatizo lililomsumbua kwa muda mrefu, lilimgharimu pesa nyingi, kwa waganga, halikuweza kutatuliwa na mtu mwingine yeyote isipokuwa YESU TU PEKE YAKE.

Jiulize kwanini liwe ni kutokwa na damu, na si kingine?

Wewe unaota kutokwa na damu, jiweke katika nafasi ya huyo mwanamke, na ujue leo ni mahali gani sahihi pa kukimbilia.

Kama wewe hujaokoka, na unadhani dunia itakuwa ni jibu la Maisha yako, au utatuzi wa matatizo yako, leo hii ujue Mungu anasema na wewe kuwa  UMEMWACHA YESU APITE.

Mungu anakuonyesha YESU tu ndio jibu la Maisha yako, haijalishi wewe ni muislamu, au dini gani,..Ni Yesu tu pekee ndiyo kila kitu kwako. Na anachotaka tu ni ushike pindo la vazi lake, aiponye roho yako.

Maana ya Kushika pindo la vazi lake, ni kuonyesha kuwa unahitaji msaada, hivyo hapo ulipo kama Maisha yako yapo dhambini, basi tubu leo, mpe Bwana Yesu Maisha yako. Na atakupokea na ataiponya roho yako, na hata mwili wako ikiwa una matatizo.

Hivyo ikiwa upo tayari kutubu leo na kutaka akufanye kuwa kiumbe kipya, akuponye misiba yako, akupe tumaini jipya, hata kama wewe ni muislamu,  basi uamuzi huo ni wa busara sana. Hivyo fungua hapa  Kwa ajili ya kuongozwa sala ya toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Jiunge na kundi la whatsapp kwa kubofya chini;

Group la whatsapp  Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Tazama masomo mengine chini.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au kwa namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

JE! DAMU INA UMUHIMU WOWOTE KATIKA MAISHA?

DAMU YA YESU INANENAJE MEMA KULIKO YA HABILI?

MAANA YA MAJINA NA TAFSIRI ZAKE.

KUOTA NYOKA.

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/08/08/kuota-unatoka-damu-ya-hedhi/