KUOTA UNAOLEWA/UNAOA.

by Admin | 12 August 2020 08:46 am08

Kuota unaolewa/ unaoa kunamaanisha nini?


Zipo ndoto zenye maana katika Maisha yetu, na pia zipo ndoto zisizo na maana yoyote katika Maisha yetu,.

Hizi zisizo na maana ni ndoto ambazo, ubongo wetu unajiundia wakati tunapokuwa tumelala kutoka katika mazingira yetu yanayotuzunguka, au mambo ambayo tulikuwa tunayawaza au tunayafanya mara kwa mara, Na ndio maana biblia inasema;

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi..”

Hivyo asilimia kubwa ya ndoto tunazoziota kila siku, zinaangukia katika hili kundi. Kama wewe ni  mshonaji, basi tarajia asilimia kubwa ya ndoto utakazokuwa unaota mara kwa mara zitakuwa ni za namna hiyo,..Vilevile ndoto kama Kuota unaolewa/unaoa, wazo hilo pengine si geni katika kichwa chako,kwamba siku moja umekuwa ukifikiria kuwa utakuja kuoa au utaolewa, Hususani pale unapokuwa umefikia umri huo, lakini bado haijawa hivyo kwako.

Au inakuja kutokana na kuwa umekuwa ukihudhuria mazingira ya harusi mara kwa mara, Hivyo ubongo wako ukayachukua hayo matukio na kuyarudia hivyo hivyo au kwa namna nyingine unapokuwa umelala.

Lakini pia ndoto za namna hii zinaweza kuwa ni za rohoni, hivyo kubeba maana Fulani,

Kwa mfano ikiwa ulikuwa katika kumwomba Mungu, akupe mume/mke, ukiota upo katika ndoa, basi ujue jambo hilo lipo mlangoni kwako.

Lakini unachopaswa kufanya ili Mungu akupe sawasawa na chaguo lake.

Lakini ukiwa ni mzinifu, unatanga tanga na kila mwanaume, au mwanamke,  au unaishi mtu ambaye  hamjaona, sahau Mungu kulitekeleza hilo, na kama likifanikiwa basi ujue huyo utakayempata hujachaguliwa na Mungu.

Ili kufahamu njia sahihi ya kumpa mweza wa Maisha fungua hapa;

>>> NJIA SAHIHI YA KUMPATA MWENZA WA MAISHA KIBIBLIA.

Lakini hayo yote ni lazima uwe katika wokovu, ukimpata Kristo, umepata vyote, Ukimkosa yeye, umepoteza vyote mpaka uzima wako. Hivyo kama leo hii unahitaji kumkaribisha Bwana Yesu maishani mwako, basi uamuzi huo ni mzuri kwako..Ikiwa upo tayari kufanya hivyo sasa, basi fungua link hii, kwa ajili ya kuongozwa sala ya toba. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Pia kama utahitaji kujiunga katika magroup yetu ya Whatsapp unaweza ukabofya hapa chini>>

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

Bahari mbalimbali zilizoorodheshwa kwenye biblia.

UNAMCHUKULIA YESU KWAKO KAMA NANI?

KUOTA UNA MIMBA.

KUOTA UPO UCHI.

KUOTA NYOKA.

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/08/12/kuota-unaolewa-unaoa/