Neno ‘Kima’ linamaanisha nini Katika biblia? (Mathayo 27:9 )

by Admin | 13 April 2022 08:46 am04

Tofauti na “Kima” mnyama ambaye anajulikana (jamii ya nyani), ukirudi katika biblia Neno hili lina maana nyingine pia.

Kima maana yake ni “thamani ya kitu katika pesa”.

Kwa mfano tukisema kima cha nazi ni Tsh. 1000. Maana yake ni kuwa thamani ya nazi ni sh. 1000.

Kwamfano Neno hilo utalipata katika vifungu hivi;

Mithali 31:10 “Mke mwema, ni nani awezaye kumwona? Maana kima chake chapita kima cha marijani”.

Yaani thamani mke mwema, inazidi thamani ya madini ghali ya Marijani (Ruby).

Mathayo 27:9 “Ndipo likatimia neno lililonenwa na nabii Yeremia, akisema, Wakavitwaa vipande thelathini vya fedha, kima chake aliyetiwa kima, ambaye baadhi ya Waisraeli walimtia kima;”

Walawi 27: 11 “Na kama ni mnyama ye yote asiye safi, wa namna ambayo hawamsongezi kwa Bwana, basi atamweka huyo mnyama mbele ya kuhani;

12 na kuhani atamtia kima, akiwa mwema akiwa mbaya; kama wewe kuhani utakavyomtia kima, ndivyo itakavyokuwa.

13 Lakini kwamba ataka kumkomboa kweli, ndipo atakapoongeza sehemu ya tano juu ya hesabu yako.

14 Na mtu atakapoiweka nyumba yake iwe wakfu kwa Bwana ndipo kuhani ataihesabu kima chake hiyo nyumba, ikiwa njema ikiwa mbaya; kama kuhani atakavyoihesabu kima chake ndivyo itakavyokuwa”.

Soma pia Walawi 27:23, Ayub 18:28, Matendo 7:16

Je, kipo kima kinachozidi thamani ya Bwana Yesu?

Yuda alijaribu, kumsaliti Bwana kwa kima cha fedha, lakini Pamoja na kupokea mapesa yote, bado mwisho wa siku aliona, thamani yake hailinganishwi na utajiri wowote wa ulimwengu, ijapokuwa alikuwa ni mwizi lakini utaona alirudisha fedha zao zote, na kwenda kujinyonga.

Sasa Ikiwa watu waovu wanauona uthamani wa Bwana, hadi kwenda kujiua, iweje wewe uone kazi ni bora kuliko Bwana Yesu, anasa ni bora kuliko ibada?.

Je! thamani ya Bwana wako inazidi thamani ya huu ulimwengu? Bwana Yesu alisema Itakufaidia nini uupate ulimwengu mzima halafu upate hasara ya nafsi yako? Itakufaidia nini?

Tubu mgeukie Bwana..

Ikiwa hujampa Bwana Yesu Maisha yako, na upo tayari kufanya hivyo leo, kwa kumaanisha kabisa, basi fungua hapa kwa ajili ya mwongozo wa Sala ya Toba. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Konde la Soani ni nini? (Zaburi 78:12,43)

Deraya ni nini? Kama tunavyosoma katika Isaya 59:17

Bushuti ni nini?

Nondo ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Tunguja ni nini katika biblia? (Mwanzo 30:14).

Hisopu/ Hisopo ni nini katika biblia?(Zaburi 51:7)

Kuhusuru ni nini kibiblia? (Luka 19:43)

Kujuzu ni nini kama tunavyosoma katika 2Wakorintho 12:4?

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2022/04/13/neno-kima-linamaanisha-nini-katika-biblia-mathayo-279/