Kupoza maana yake nini katika biblia? (Mathayo 10:8).

by Admin | 17 June 2022 08:46 pm06

 Kupoza ni nini?

Jibu: “Kupoza” ni Kiswahili kingine cha neno “kuponya”. Hivyo badala ya kutumia neno kuponya, linaweza kutumika neno “kupoza” likawa na maana ile ile. (kama vile neno mtu na mwanadamu inavyoweza kuwa na maana moja).

Bwana Yesu aliwapa Mitume wake uwezo wa kupoza wagonjwa kupitia jina lake.

Marko 6:12 “Wakatoka, wakahubiri kwamba watu watubu.

13 Wakatoa pepo wengi, wakapaka mafuta watu wengi waliokuwa wagonjwa, WAKAWAPOZA”.

Na uwezo huo haukuishia tu kwa wale mitume 12, bali aliendelea hata watumishi wengine wengi waliomwamini Bwana Yesu kama akina Stefano na akina Barnaba, na Paulo.

Matendo 28:8 “Ikawa babaake Publio alikuwa hawezi homa na kuhara damu. Paulo akaingia kwake, akaomba, akaweka mikono yake juu yake, na KUMPOZA.

9 Yalipokwisha kutendeka hayo wengine waliokuwa na magonjwa katika kisiwa wakaja WAKAPOZWA”.

Na uwezo huo haukuishia tu kwa wakristo wa kanisa la Kwanza, bali hata leo uwezo huo Bwana katupa, wote tumwaminio pale tunapokwenda kuhubiri injili..

Mathayo 10:7 “Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia.

8 POZENI WAGONJWA, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure”.

Na si katika kuhubiri tu!.. bali hata popote pale tutakapokuwepo, uwezo huo utakuwa nasi..

Marko 16:17 “Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;

18 watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya”.

Yesu, anafanya miujiza hata leo!.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

LIPO LA KUJIFUNZA KWA WALE MASHUJAA 37 WA DAUDI.

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

Nini tofauti ya Uwezo na Uweza kibiblia?

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2022/06/17/kupoza-maana-yake-nini-katika-biblia-mathayo-108/