Masihi ni nani?

by Admin | 7 December 2022 08:46 am12

Je! neno Masihi linamaanisha nini?

“Masihi” ni Neno la Kiebrania, linalomaanisha “Mpakwa mafuta” (Yaani mtu aliyeteulewa na Mungu kwa kusudi Fulani). Katika biblia watu walioteuliwa na Mungu rasmi kuwa Wafalme, hao waliitwa masihi wa Bwana, vile vile waliochaguliwa na Mungu kuwa manabii, nao pia waliitwa masihi wa Bwana.

Tafsiri nyingine ya neno Masihi ni “Kristo”. Kwahiyo katika biblia mamasihi (yaani makristo au watiwa mafuta) walikuwa wengi lakini aliyekuwa MASIHI KIKWEKWELI alikuwa ni Mmoja tu! Ambaye ni YESU KRISTO.

Mamasihi wengine ni kweli walipakwa mafuta na Mungu lakini hawakuwa wakamilifu asilimia zote..Daudi alikuwa ni masihi wa Bwana (Soma 1Samweli 16:6-13) lakini hakuwa mkamilifu asilimia zote, kwani aliua na pia alimtwaa mke wa Uria na kumfanya wake.

Vile vile Mfalme Sauli maandiko yanasema alikuwa ni masihi wa Bwana lakini tunasoma alikuja kukengeuka na kumdharau Mungu na maagizo yake..

1Samweli 24:9 “Daudi akamwambia Sauli, Kwa nini unasikiliza maneno ya watu wasemao, Tazama, Daudi anataka kukudhuru?

10 Tazama, leo hivi macho yako yameona jinsi Bwana alivyokutia mikononi mwangu pangoni, na watu wengine wakaniambia nikuue; lakini nikakuacha; nikasema, Sitaki kuunyosha mkono wangu juu ya bwana wangu; kwa maana yeye ni masihi wa BWANA”.

Soma pia 1Nyakati 16:22

Hawa wote walikuwa ni watiwa mafuta lakni walikuwa na kasoro nyingi,  Lakini Yesu Kristo alikuwa ni mkamilifu kuliko hao wote..Kwahiyo yeye ndiye aliyetiwa Mafuta Makuu kuliko wote, ndio maana tunasema aliye Masihi peke yake ni YESU.

Waebrania 1:8 “Lakini kwa habari za Mwana asema, Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele; Na fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili.

9 Umependa haki, umechukia maasi; Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta, Mafuta ya shangwe kupita wenzio”.

Kwahiyo Wayahudi wote, na wasamaria wote, walikuwa wanautazamia ujio wa huyu Masihi mmoja ambaye atakuwa mkamilifu, asiyekuwa na dhambi hata moja, ambaye atawafundisha sheria za Mungu na kuwaokoa na dhambi zao.

Yohana 4:25 “Yule mwanamke akamwambia, Najua ya kuwa yuaja Masihi, (aitwaye Kristo); naye atakapokuja, yeye atatufunulia mambo yote.

26 Yesu akamwambia, Mimi ninayesema nawe, ndiye”

Yohana 1:40 “Andrea, nduguye Simoni Petro, alikuwa mmoja wa wale wawili waliomsikia Yohana na kumfuata Yesu.

41 Huyo akamwona kwanza Simoni, ndugu yake mwenyewe, akamwambia, Tumemwona Masihi (maana yake, Kristo). .

Huyu Masihi Yesu Kristo, alishakuja miaka zaidi ya elfu 2 iliyopita, akapaa mbinguni, na sasa yupo hai, na pia amekaribia sana kurudi. Atakapokuja hatakuja tena kwa kusudi la wokovu, bali kwa HUKUMU.

Yohana 5:22 “Tena Baba hamhukumu mtu ye yote, bali amempa Mwana hukumu yote”

Je umemwamini Masihi Yesu?.. Umetii agizo lake la ubatizo?, na je umempokea Roho wake Mtakatifu.. Fahamu kuwa kama umekosa vitu hivyo vitatu, bado hujaokolewa kulingana na Neno lake. Hivyo ni vyema ukafanya uamuzi wa kumwamini na kutubu leo na kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo, na mambo mengine yaliyosalia Roho Mtakatifu utakayempokea atakuongoza katika kweli yote.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

ISHARA ITAKAYONENEWA

JUMA LA SABINI (70) LA DANIELI

Je tunaruhusiwa kujipaka mafuta au kujipulizia marashi?

 Je! Ni sahihi kutumia maji ya upako,katika kufanya maombezi?

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2022/12/07/masihi-ni-nani/