Haini ni mtu gani? Mithali 13:2

by Admin | 14 March 2023 08:46 pm03

Tusome,

Mithali 13:2 “Mtu atakula mema kwa matunda ya kinywa chake; Bali nafsi ya mtu haini itakula jeuri”

Haini ni jina lingine la mtu ambaye ni “Msaliti”, mtu anayefanya usaliti juu ya mwingine ni sawa na kafanya “Uhaini”. Mtu anayeisaliti nchi yake mtu huyo ni Mhaini, vile vile  mtu anayeisaliti Imani yake yenye kumfikisha mbinguni, kwa kurudia mambo machafu mtu huyo anafanya uhaini kwa Mungu wake.

Zaburi 78:57 “Bali walirudi nyuma, wakahaini kama baba zao; Wakaepea kama upinde usiofaa

 58 Wakamkasirisha kwa mahali pao pa juu, Wakamtia wivu kwa sanamu zao.

 59 Mungu akasikia, akaghadhibika, Akamkataa Israeli kabisa.”.

Na maandiko yanazidi kuonyesha kuwa Wahaini wote wa imani watapata adhabu..

Zaburi 119:158 “Nimewaona watendao uhaini nikachukizwa, Kwa sababu hawakulitii neno lako”.

Mithali 22:12 “Macho ya Bwana humhifadhi mwenye maarifa; Bali huyapindua maneno ya mtu haini.”

Soma pia Mithali 13:15 na Zaburi 25:3.

Kama tayari ulikuwa umeyakimbia machafu ya ulimwengu, na sasa umeyarudi nyuma fahamu kuwa huo unafanya uhaini mbele za Mungu, kimbia haraka sana msalabani ukatubu,  kama ulikuwa umeacha uzinzi na sasa umeurudia, tubu kwa machozi sana mbele za Bwana, leo hii ni nafasi yako ya kutubu na kumgeukia Mungu, usingoje kesho, na hakikisha unatubu kwa kumaanisha kabisa kutofanya hayo uliyoyafanya au unayoyafanya, na Bwana atakupokea lakini ukizidi kukawia upo hatarini sana…

 Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

Je ni kweli kila nafsi itaonja mauti kulingana na (Zaburi 89:48)?

Sifa ni nini?

USIMFANYIE JEURI ROHO WA NEEMA.

MAGONJWA YAKUPATAYO MARA KWA MARA.

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2023/03/14/haini-ni-mtu-gani-mithali-132/