Fahamu ni nani aliye mwandishi wa kitabu cha Mathayo.

by Admin | 20 June 2024 08:46 am06

SWALI: Mwandishi wa kitabu cha Mathayo ni nani?


Kama jina la kitabu linavyojieleza “INJILI KAMA ALIVYOIANDIKA MATHAYO MTAKATIFU”. Maana yake ni kuwa kitabu hiki kiliandikwa na Mathayo. Lakini utata unakuja ni Mathayo yupi?

Ijapokuwa biblia haielezi ni Mathayo yupi lakini wanazuoni wengi na watafiti wa historia kibiblia, wanahitimisha kusema ni Mathayo mtume wa Yesu Kristo Yule mtoza ushuru, ambaye alijulikana pia kwa jina la Lawi (Marko 2:14) ndiye aliyekiandika kitabu hicho.

Kitabu hiki kinaeleza Mwanzo wa kutokea mwokozi duniani, mpaka Kifo chake na kufufuka kwake. Ndani yake kuna historia ya mwokozi, mafundisho na matendo ya miujiza aliyoyafanya. Katika kitabu hiki zipo hotuba kuu tano ambazo Yesu alizisema;

  1. Hotuba ya mlimani (Mathayo 5-7)
  2. Hotuba ya utume (Mathayo 10)
  3. Hotuba ya ufalme wa mbinguni (Mathayo 13)
  4. Hotuba ya kanisa (Mathayo 18)
  5. Hotuba ya Siku za mwisho (Mathayo 24)

Kwa upana wa hotuba hizi na uchambuzi wa kitabu hiki, fungua hapa, >> MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA MATHAYO.

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mwandishi wa kitabu cha Mithali ni nani?

Fahamu Mwandishi wa kitabu cha Wafalme(Opens in a new browser tab)(Opens in a new browser tab)

Nini maana ya  “manabii wote na torati walitabiri mpaka wakati wa Yohana” (Mathayo 11:13)

Rudi Nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2024/06/20/fahamu-ni-nani-aliye-mwandishi-wa-kitabu-cha-mathayo/