Mhunzi ni nani? (Isaya 54:16)

by Admin | 28 June 2024 08:46 pm06

Jibu: Turejee..

Isaya 54:16 “Tazama, nimemwumba MHUNZI avukutaye moto wa makaa, akatoa silaha kwa kazi yake; nami nimemwumba mharibu ili aharibu”

Mhunzi/ Wahunzi  wanaozungumziwa katika biblia ni watu “wanaofua Vyuma, shaba, fedha au dhahabu”. Maana yake wanaviyeyusha vyuma hivyo au madini hayo na kuyaumba kwa maumbile mbalimbali kama silaha na urembo.

Tofauti ya Mhunzi na mfinyanzi, ni kwamba Mfinyanzi yeye anashughulika na udongo, anafanya kazi ya kutengeneza vyombo au zana kupitia udongo, (Soma Isaya 41:25, Isaya 64:8 na Yeremia 18:6) lakini “Mhunzi” yeye anatumia vitu vya metali kama vyuma, fedha, shaba au dhahabu kutengeneza vito au zana za kazi au silaha.

Mistari mingine katika biblia inayotaja Wahunzi (wafua vyuma/dhahabu/shaba au fedha) ni pamoja na 1Samweli 13:19, 2Wafalme 24:16, Isaya 44:12, Isaya 46:6, Yeremia 24:1, Zekaria 1:20, Matendo 19:24, na 2Timotheo 4:14.

Je umempokea BWANA YESU?. Kama bado fahamu kuwa upo katika hatari kubwa yenye mwisho mbaya, ni vyema ukafanya maamuzi leo ya kumpokea YESU kama BWANA na MWOKOZI wa maisha yako, kabla ya kumaliza muda wako wa kuishi, kwani hakuna nafasi ya pili baada  ya kifo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Sala ya baraka (Hesabu 6:24-26).

NDUGU,TUOMBEENI.

KWANINI NABII ISAYA ALIAGIZWA KUHUBIRI UCHI?

Mchuuzi ni nani? (Hosea 12:7).

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 12 (Kitabu cha Isaya)

Rudi Nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2024/06/28/mhunzi-ni-nani-isaya-5416/