Sifa na Lami ni nini? (Kutoka 2:3).

by Admin | 28 June 2024 08:46 am06

Swali: Sifa na Lami ni nini kama tunavyosoma katika Kutoka 2:3

Jibu: Turejee..

Kutoka 2:3 “Na alipokuwa hawezi kumficha tena, akampatia kisafina cha manyasi akakipaka SIFA NA LAMI, akamtia mtoto ndani yake, akakiweka katika majani kando ya mto”

“Sifa” inayozungumziwa hapo sio “Utukufu” bali ni aina ya “Nta” inayopatikana/kuzalishwa na aidha mimea au mafuta. Mfano wa Nta ya mimea ni ile inayotokea katika baadhi ya mashina na miti (Tazama picha chini).

nta  ya mimea biblia

Lakini Nta ya “Sifa” ni ile inayopatikana kutoka katika mabaki ya “Makaa ya mawe” ambayo ni nyepesi kuliko Lami. (Tazama picha chini)

sifa ni nini biblia

Na “Lami” ni Nta nzito Zaidi inayoganda ambayo kimwonekano ni nyeusi na inapatikana katika hali ya uasili au baada ya kuchujwa kwa mafuta ya petroli kiwandani.

Lami inapatikana katika uasili wake maeneo ya bahari ya chumvi (Sidimu)mpakani mwa nchi ya Israeli na Yordani..

Mwanzo 14:10 “Na bonde la Sidimu lilikuwa limejaa MASHIMO YA LAMI. Nao wafalme wa Sodoma na Gomora wakakimbia, wakaanguka huko, nao waliosalia wakakimbia milimani”

“Lami” kimwonekano ni nzito kuliko “Sifa” na rangi yake ni nyeusi kama tu “Sifa”. (Tazama picha chini).

lami ni nini

Biblia inatabiri siku ya mwisho (ya kisasi cha Mungu) juu ya wanadamu wote watendao maasi, dunia itapigwa (kwa kuunguzwa kwa moto) na vijito na ardhi yote itakuwa Lami.

Isaya 34:8 “Maana ni siku ya kisasi cha Bwana, mwaka wa malipo, ili kushindania Sayuni.

9 Na vijito vyake vitageuzwa kuwa lami, na mavumbi yake yatageuzwa kuwa kiberiti, NA ARDHI YAKE ITAKUWA LAMI IWAKAYO”.

Sasa kufahamu kwa mapana kwanini Safina ile iliyomficha Musa ilipakwa Sifa pamoja na Lami?.. na ni ufunuo gani uliopo nyuma yake?, fungua hapa >>>>SAFINA NI NINI?

sifa ni nyeusi

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Sifa ni nini?

Nini maana ya Mithali 27:21  inaposema “mtu hujaribiwa kwa sifa zake?”

NI NINI KINATOKA KINYWANI MWA MTOTO WAKO?

MALAIKA NI WALIMU WA SIFA KWETU, TUJIFUNZE KWAO!

TENDA JAMBO LA ZIADA.

Rudi Nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2024/06/28/sifa-na-lami-ni-nini-kutoka-23/