Majini wanaotajwa kwenye Walawi 17:7 ni viumbe gani?

by Devis | 12 June 2025 08:46 am06

Jibu: Turejee kuanzia mstari wa 6..

Walawi 17:6 “Naye kuhani atainyunyiza damu yake juu ya madhabahu ya Bwana, mlangoni pa hema ya kukutania, na kuyateketeza mafuta yake, yawe harufu njema mbele za Bwana.

7 WALA HAWATATOA TENA SADAKA ZAO KWA WALE MAJINI, ambao huwafuata ili wafanye uasherati nao. Sheria hii itakuwa sheria ya milele kwao, kizazi baada ya kizazi”.

“Majini” wanaotajwa hapo ni “mashetani”..

Katika agano la kale sadaka yoyote iliyotolewa nje ya hema  ya mungu (maana yake katika madhabahu nyingine), sadaka hiyo ilihesabika kuwa imetolewa kwa majini/mashetani, na yeyote aliyetoa sadaka yake huko, akabainika sheria ilikuwa ni kutengwa na watu wake.

Walawi 17:8 “Nawe utawaambia, Mtu awaye yote katika nyumba ya Israeli, au miongoni mwa wageni, wanaokaa nao, atoaye sadaka ya kuteketezwa au dhabihu,

9 wala haileti mlangoni pa hema ya kukutania, ili aisongeze kwa Bwana BASI MTU HUYO ATATENGWA NA WATU WAKE”.

Mahali pekee Bwana Mungu alipopachagua pa kutolea sadaka ni katika “HEMA YA MUNGU”, katika kipindi cha Waamuzi na katika “NYUMBA YA MUNGU” aliyoitengeneza Sulemani katika kipindi cha Wafalme na kuendelea.

Kwahiyo sadaka yoyote inayopelekwa mahali panapoabudiwa ibilisi, basi sadaka hiyo ni imetolewa kwa majini/mashetani..na sadaka inayotolewa kwa mashetani basi mtu huyo au watu hao wanakuwa na ushirika na mashetani, ndivyo Neno la Mungu linavyosema..

1Wakorintho 10:20 “Sivyo, LAKINI VITU VILE WAVITOAVYO SADAKA WAVITOA KWA MASHETANI, wala si kwa Mungu; nami sipendi ninyi KUSHIRIKIANA NA MASHETANI. Hamwezi kunywea kikombe cha Bwana na kikombe cha mashetani”.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba “majini” wanaotajwa katika Walawi 17:7 ni mashetani/mapepo ambao pia wanatajwa katika Isaya 13:21 na 2Nyakati 11:15 wakati wa mfalme Yeroboamu.

2Nyakati 11:15 “naye akajiwekea makuhani wa mahali pa juu, na wa WALE MAJINI, na wa zile ndama alizozifanya.”

Na pia zipo sadaka zitolewazo kwa Mungu na pia zitolewazo kwa mashetani, Mtu anayeenda kwa waganga wa kienyeji sadaka yake anaitoa kwa mashetani, na kafara yoyote iwe ya mnyama au kiumbe chochote inayofanyika katika agano jipya ni sadaka kwa mashetani na si kwa Mungu, kwani hatuna tena kafara za wanyama katika agano jipya, wala hakuna kafara za watu kwa Mungu na hazijawahi kuwepo huko kabla, kafara zote za namna hiyo ni za mashetani.

Zaburi 106:37 “Naam, walitoa wana wao na binti zao Kuwa dhabihu kwa mashetani.

38 Wakamwaga damu isiyo na hatia, Damu ya wana wao na binti zao, Waliowatoa dhabihu kwa sanamu”

Je umempokea YESU?.. fahamu kuwa hakuna wokovu kwa mwingine yoyote isipokuwa kwake!, na tunaishi majira ya kurudi kwa YESU, huu si wakati wa kucheza na dunia, bali kujitoa kwa MUNGU.

1Petro 4:2 “Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika MAPENZI YA MUNGU, WAKATI WENU ULIOBAKI WA KUKAA HAPA DUNIANI.

3 Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?

MAJINI WAZURI WAPO?

Tunathibitisha vipi kuwa Yule Malaika wa (Yohana 5:4) ni wa MUNGU?

AINA ZA MAJINI, MAJINA YAO, KAZI ZAO, NA TIBA ZAKE.

Ipi tofauti kati ya Uhai na Uzima kibiblia?

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2025/06/12/majini-wanaotajwa-kwenye-walawi-177-ni-wapi/