Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana

by Nuru ya Upendo | 12 September 2025 08:46 pm09

Mariamu alipotokewa na Malaika na kuelezwa habari ya mambo ambayo hayawezekaniki kibinadamu, alionyesha tabia ya kitofauti sana…hakuanza kubisha, Hakuanza kukinzana na kusudi na mpango wa Mungu juu yake, ulio juu ya upeo wa ufahamu wake, kinyume chake aliukubali, tena si Kwa maneno ya juu juu tu, bali kwa ukiri wa utumwa…akasema

“Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema.”

Maana yake ni kuwa ikiwa jambo hilo linanilazimu kulitumikia mimi nitafanya hivyo kama Mtumwa..

Luka 1:34-35,38

[34]Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno hili, maana sijui mume?

[35]Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu…

[38]Mariamu akasema, Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema. Kisha malaika akaondoka akaenda zake.

Mariamu ni kielelezo kamili cha mwanamke thabiti wa kikristo, lakini sio tu mwanamke bali bali kwa kanisa la Kristo kwa ujumla.

Utii wa namna hii ndio Bwana anaoutaka kwa watu wote wamchao yeye..

Ijapokuwa kibinadamu haikuwezekana, akijua pia ikishatokea itamletea aibu katika jamii, atakaposadikika amepata ujauzito, kimiujiza hakuna atakaye mwelewa, watasema ni mzinzi, akijua pia kuna majukumu mengine mazito yatafuata..bado alilipokea kusudi la Mungu..lililo juu ya uwezo wake.

Hakukubali kuingia kwenye kosa kama la Musa, kusema mtume mwingine, hakulimbikia kusudi la Mungu kama Yona kukimbilia Tarshishi…bali alilipokea zaidi ya mtumwa.

Si ajabu kwanini Bwana alimpa neema kubwa namna ile…

Ndugu/kaka Bwana anatazama Utayari wako zaidi ya uwezo wako, anatazama utii wako zaidi ya umri wako.

Kila mmoja wetu leo, aliyeamini katika agano jipya ameitwa kufanya MAKUBWA mfano tu wa Mariamu…Hakuna hata mmoja ambaye hajaitwa kwa ajili ya mambo makubwa ya Mungu… kwasababu Mungu ni Mungu wa miujiza na yaliyoshindikana.

Isipokuwa Imani zetu ni haba Kwa Mungu ndio maana hatuoni matokeo makubwa. Kinachohitajika ni kujiachilia tu kwake..kisha kumwacha yeye atende kazi zake ndani yetu.

Haijalishi wewe ni mwanaume au mwanamke, mzee au kijana, una elimu au huna elimu, tajiri au maskini.. kubali kujiachia kama Mariamu katika kusudi lolote la Mungu.. unapoona una nafasi ya kuombea wagonjwa Fanya hivyo, una nafasi ya kuwashuhudia watu mitaani, masokoni, viwanjani fanya hivyo, huko huko Bwana atajifunua kwako kwa namna isiyo ya kawaida. Na Utukufu utamrudia yeye.

Kumbuka tu Mungu amechagua kutumia vyombo Dhaifu kukamilisha kusudi lake timilifu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je Mariamu alikuwa na umri gani alipochukua mimba ya Bwana YESU?

JE BIKIRA MARIAMU ALIKUFA?

USICHELEWE KUMPAKA BWANA MARHAMU!

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2025/09/12/tazama-mimi-ni-mjakazi-wa-bwana/