by Nuru ya Upendo | 20 December 2025 08:46 am12
Jibu: Turejee..
Wimbo 3:10 “Nguzo zake alizifanyiza za fedha, Na mgongo wake wa dhahabu, Kiti chake kimepambwa URUJUANI, Gari lake limenakishiwa njumu, Hiba ya binti za Yerusalemu”.
“Urujuani” ni neno lingine la rangi ya “Zambarau”..
Neno hilo pia tunalisoma katika kile kitabu cha 2Nyakati 2:7..
2Nyakati 2:7 “Unipelekee basi mtu mstadi wa kazi ya dhahabu, na ya fedha, na ya shaba, na ya chuma, NA YA URUJUANI, na nyekundu, na samawi, mwenye kujua kuchora machoro, pamoja na wastadi walioko Yuda na Yerusalemu pamoja nami, aliowaweka baba yangu Daudi”.
Rangi ya Urujuani/Zambarau kibiblia iliwakilisha Enzi/Ufalme… Hivyo mtu aliyevaa Mavazi yenye rangi hiyo ya Urujuani/zambarau alifahamika kama mtu mkuu, aidha mfalme, Malkia au jemedari.
Ufunuo 7:3 “Akanichukua katika Roho hata jangwani, nikaona mwanamke, ameketi juu ya mnyama mwekundu sana, mwenye kujaa majina ya makufuru, mwenye vichwa saba na pembe kumi.
4 Na mwanamke yule alikuwa AMEVIKWA NGUO YA RANGI YA ZAMBARAU, na nyekundu, amepambwa kwa dhahabu, na kito cha thamani, na lulu, naye alikuwa na kikombe cha dhahabu mkononi mwake, kilichojawa na machukizo, na machafu ya uasherati wake”.
Utasoma tena juu ya rangi hiyo katika.. Mithali 31:22, Yeremia 10:9, Ezekieli 27:7, na Ezekieli 27:16.
Bwana atubariki.
Mafundisho Mengine
Kimiami ni nini? (Wimbo ulio bora 2:9).
Machela ni nini (Wimbo ulio bora 3:7)
Pambaja ni nini katika Biblia kama tunavyosoma katika kitabu cha Wimbo ulio bora 1:2?
Namna sahihi ya kusoma Neno (biblia).
Source URL: https://wingulamashahidi.org/2025/12/20/njumu-ni-nini-wimbo-310/
Copyright ©2026 Wingu la Mashahidi unless otherwise noted.