Je! msalaba kaburini una umuhimu wowote?

by Admin | 31 August 2019 08:46 pm08

SWALI: Ule msalaba unaowekwa kwenye kaburi, na ile ibada inayofanywa vina umuhimu wowote kwa mkristo?

JIBU: Inategemea hiyo ibada inayofanywa ina maudhui gani, kama ibada imelenga kumwombea huyo mfu hayo ni makosa mbele za Mungu, lakini kama imelenga kushukuru au kuwafundisha na kuwaonya watu waliosalia ambao bado wanaishi, kuhusu mwanzo wa safari yetu hapa duniani hadi mwisho wake, na kwamba kila mtu aweke mambo yake sawa na Mungu wake, ibada hiyo ni njema na inakubalika mbele za Mungu, 

Mhubiri 7: 2 “Heri kuiendea nyumba ya matanga, Kuliko kuiendea nyumba ya karamu. Kwa maana huo ndio mwisho wa wanadamu wote, naye aliye hai atautia moyoni mwake”. 

Na pia sio vibaya kuweka msalaba juu ya kaburi la marehemu, kwasababu ile ni ishara ya mauti ya mkristo na tumaini la ufufuo wa wafu, lakini ni makosa kuweka msalaba na kuuangalia kama ndio utimilifu wote, ule uwe ishara tu, usihusishwe na masuala yoyote ya ibada, kuepuka ibada za sanamu. Na vivyo hivyo kanisani sio vibaya kuweka msalaba kama ishara ya imani ila usitumiwe tu kusujudiwa kama baadhi ya madhehebu yanavyofanya. Utakuta hata kukemea pepo kiongozi anatumia msalaba badala ya jina la Yesu, sasa hayo yote ni makosa mbele za Mungu. 

Ubarikiwe sana. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada zinazoendana:

JE! KIONGOZI WA DINI ANAOUWEZO WA KUSAMEHE DHAMBI ZA MTU, MFANO PADRE?

JE! NI SAHIHI MTU KUNING’INIZA PICHA NYUMBANI MWAKO KAMA YA YESU?

JE! WEWE NI MWANA WA IBRAHIMU?

NJIA YA MSALABA

MWENDO UNAOSHANGAZA SANA!


 

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2019/08/31/ule-msalaba-unaowekwa-kwenye-kaburi-na-ile-ibada-inayofanywa-vina-umuhimu-wowote-kwa-mkristo/