Bwana atusaidie tusiwe WASHABIKI WAKE au WAFUASI WAKE, bali tuwe watu tunayoiendea njia yake, tukiwa ni walevi na bado tunajiita wakristo sisi bado ni washabiki, tukiwa tunaenda kanisani na bado tunasengenya sisi bado tu ni washabiki, gharama za mbio hatuzijui, ikiwa bado tunavaa nusu uchi na mavazi yasiyostahili mbele za Mungu, bado sisi ni washabiki hatutaweza kufika kwa Baba wanaofika kwa Baba ni wale wanaoiendea NJIA YA BWANA YESU KRISTO, yeye hakuwa mlevi, hakuwa mtukanaji, hakuwa mwizi, hakuwa mwabudu sanamu, hakuwa mwasherati, hakuwa mfuasi wa mambo ya ulimwengu huu. Hiyo ndiyo njia tunayowekewa tuifuate, kama Mwana wa Mungu kapitishwa kwa hiyo, unadhani sisi wengine tutatengenezewa njia nyingine mbadala ya mkato?? Hapana njia ni moja tu, na imeshawekwa na kuthibitishwa na Mungu nayo ni njia ya YESU KRISTO.