Je!, Inakubalika kumtolea mtu mwengine damu?(blood transfusion).

by Admin | 2 September 2019 08:46 pm09

JIBU: Ikiwa Bwana alituagiza tupendane sisi kwa sisi hata tufikie hatua ya kuweza kutoa uhai wetu kwa ajili ya wengine wapone kama yeye alivyofanya kwetu sisi, Sasa! damu itakuwa ni kitu gani kwetu?. Tumeambiwa tusipende kwa neno au kwa ulimi tu bali kwa tendo.   Biblia inatuambia

1Yohana 3:16 “Katika hili tumelifahamu pendo, kwa kuwa yeye aliutoa uhai wake kwa ajili yetu; imetupasa na sisi kuutoa uhai wetu kwa ajili ya hao ndugu.

17 Lakini mtu akiwa na riziki ya dunia, kisha akamwona ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia huruma zake, je! Upendo wa Mungu wakaaje ndani yake huyo?

18 Watoto wadogo, TUSIPENDE KWA NENO, wala kwa ulimi, BALI KWA TENDO NA KWELI.”  

Ni sawa na kumwona ndugu yako amepungukiwa damu na, hivyo asiposaidiwa atakwenda kufa muda si mrefu, na wewe angali unao uwezo huo wa kumsaidia na hautaki unasema sitoi damu yangu ni dhambi, hivyo nakuombea tu,kisha Mungu akupumzishe salama, je! hapo utakuwa umeonyesha upendo gani kwa ndugu yako huyo?. Huoni kama utakuwa umependa kwa Neno na wala si kwa tendo?.   Lakini wapo watu wanafanya hivyo kama biashara kwa kisingizio cha kuwa wanasaidia watu, wanatoa damu zao, wanatoa figo zao, si kwa lengo la kumsaidia ndugu yake, bali kwa lengo la kufanya biashara. Hiyo ni dhambi mbele za Mungu na wanaofanya hivyo siku zinakuja watuvuna walichokipanda.  

Ubarikiwe.


Mada Nyinginezo:

NI RAHISI KWA NGAMIA KUPENYA KATIKA TUNDU LA SINDANO, JE! NI SINDANO IPI HIYO INAYOZUNGUMZIWA?

JE! NI HALALI KUTOA CHETI KWA WAKRISTO WANAOOANA?

NIFANYE NINI ILI NIIKWEPE HUKUMU.

AMIN! NAWAAMBIA KIZAZI HIKI HAKITAPITA

SIKU YA BWANA INAYOTISHA YAJA!

RABONI!


Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2019/09/02/je-inakubalika-kumtolea-mtu-mwengine-damublood-transfusion/