MADHABAHU NI NINI?

by Admin | 27 December 2019 08:46 am12

Jiunge na group la Whatsapp, ujifunze biblia na upate Neno la siku kila asubuhi. Pamoja na maswali mengi ya biblia yaliyojibiwa..kwa link hii >>> https://chat.whatsapp.com/FAyJLXo8guQ0iZ0JzQKbXg

Madhabahu ni nini?..Je madhabahu ya kuvukiza uvumba ni nini?..je hata sasa watu wanatengeneza madhabahu za kutolea dhabihu?…madhabahu ya kwanza kutengenezwa ni ipi?

Madhabahu ni mahali ambapo sadaka zinatolewa.. Katika Agano la Kale, Bwana Mungu aliwaagiza wana wa Israeli wamtolee sadaka…Zilikuwepo sadaka za aina mbali mbali kama vile sadaka za dhambi, sadaka za shukrani na nyinginezo.

Lakini sadaka yoyote iliyokuwa inatolewa kama ni sadaka kuteketezwa, Ilikuwa ni lazima madhabahu itengenezwe. Kwa lugha rahisi na ambayo inaweza kueleweka ni kwamba baada ya mnyama yule aliyewekwa tayari kwaajili ya sadaka kuchinjwa..aliwekwa juu ya kuni zilizopangwa vizuri zilizo juu ya mawe…hivyo madhabahu ilitengenezwa kwa mawe na kuni..Ni sehemu maalumu ya kumchomea yule mnyama mpaka eteketee kabisa..

Madhabahu ya kwanza ilitengenezwa na Habili ambaye alimtolea Bwana sadaka ya kuteketezwa juu yake. Na Mungu aliiitakabali zaidi ya Kaini ndugu yake.

Katika Biblia tunasoma pia Nuhu alimjengea Bwana madhabahu baada ya kutoka kwenye safina.(Soma Mwanzo 8:20)

Na pia Ibrahimu alimtengenezea Mungu madhabahu mara kadha wa kadha alipotaka kumtolea Mungu sadaka…Ndio maana tunaona hata wakati ule alipojaribiwa na Mungu amtoe Isaka mwanawe..tunaona alitengeneza madhabahu.

This image has an empty alt attribute; its file name is Abraham-to-Sacrifice-Isaac-2.jpg

Na wengine wote kama akina Yakobo, Eliya, na Musa walipotaka kumtolea Mungu sadaka walitengeneza madhabahu..Na kulikuwa na maagizo maalumu ya namna ya kutengeneza madhabahu kama Mungu anavyotaka…ilikuwa sio ruhusa kutengeneza madhabahu kama za wapagani..kulikuwa na maagizo maalumu ya namna ya kuitengeneza ambapo hatuwezi kuyaangalia yote lakini mojawapo ilikuwa ni hili…

Kumbukumbu  27:5 “Na huko umjengee madhabahu Bwana, Mungu wako, madhabahu ya mawe, usitumie chombo cha chuma juu yake.

6 Jenga hiyo madhabahu ya Bwana, Mungu wako, kwa mawe yasiyochongwa; ukamtolee Bwana, Mungu wako, sadaka za kuteketezwa juu yake;”

Kulikuwepo pia kuna aina nyingine ya madhabahu iliyojulikana kama madhabau ya kuvukizia uvumba (Soma kutoka 30:27). Hii ilitumika kwaajili ya kuchomea uvumba mtakatifu ndani hema ya Mungu au Nyumba ya Mungu ..Madhabahu hii haikutengenezwa kwa mawe na kuni kama ile madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa..Hii ilikuwa ndogo na ilikuwa ni kama jiko hivi…Tazama picha chini.

madhabahu ya kuvukizia uvumba

Lakini katika Agano jipya hatuna tena hizo Madhabahu zenye mfano huo..

Madhabahu yetu kwa sasa ni mioyo yetu…Tunapomkubali Yesu Kristo na kuingia moyoni mwetu…Na anapotusafisha na kutupa Roho wake mtakatifu hapo ndipo madhabahu yetu inapokamilika katika viwango Mungu anavyovitaka..Na kuanzia huo wakati shughuli zotezote za kiibada, ikiwemo sadaka, maombi, dua, sala, utukufu, shukrani ndipo vinakubalika mbele za Mungu.

Zaburi 51:16 “Maana hupendezwi na dhabihu, au ningeitoa, Wewe huridhii sadaka ya kuteketezwa.

17 Dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika; Moyo uliovunjika na kupondeka, Ee Mungu, hutaudharau”

Lakini kama mtu hajasafishwa maisha yake kwa damu ya Yesu basi madhabahu ya moyo wake inakuwa ni chafu na hivyo hawezi kumpendeza Mungu kwa chochote kile.

Mbali na hilo, upo pia utaratibu wa kuiita mimbari ya kanisa kuwa ni madhabahu..Kiuhalisia ile sio madhabahu..Lakini pia si dhambi kuiita madhabahu na kuiheshimu. Kwasababu ni mahali ambapo Neno la Mungu (chakula cha Roho zetu linahubiriwa na tunapeleka matoleo yetu pale)..Na pia chochote kitakachofanyika pale kinyume na Neno la Mungu au kisichokuwa na utukufu wa Mungu, Ni dhambi na hivyo ni kujitafutia laana badala ya baraka..Na kumbuka pia sehemu ya mimbari ya kanisa (ambayo inajulikana kama madhabahu)..haipaswi kupambwa pambwa na mishumaa, au sanamu mpaka kufikia hatua watu wanakwenda kuvisujudia na kuviangukia na kuviogopa…Hiyo ni ibada za sanamu na ni machukizo makubwa mbele za Mungu. Mimbari inapaswa iwe ni sehemu ya kawaida tu…

Lakini madhabahu halisi ni mioyo yetu..Na hatupaswi kuweka msisitizo mkubwa wa kuiheshimu madhabahu ya kanisa na huku madhabahu halisi ya mioyo yetu imechafuka. Biblia inasema..

Mithali 4:23 “Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima”

Utakuta mtu anaiogopa madhabahu ya kanisa na kuiheshimu..Lakini kuiheshimu madhabahu halisi ya moyo wake ambapo ndipo mahali Mungu yupo karibu sana na yeye haiheshimu..Atamwabudu Mungu huku moyoni mwake ni muuaji, mwasherati, mwenye chuki na kinyongo na kutokusamehe.

Bwana atusaidie kufanya madhabahu za mioyo yetu kuwa safi..ili maombi yetu, sala zetu, dua zetu pamoja na sadaka zetu zipate kibali mbele za Mungu wetu.

Ubarikiwe sana.

+255693036618/ +255789001312


Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2019/12/27/madhabahu-ni-nini/