Lumbwi ni nini katika biblia?

by Admin | 1 November 2021 08:46 am11

Lumbwi ni jina lingine la mnyama anayeitwa  KINYONGA.

Katika biblia utamsoma kwenye kifungu hiki..

Mambo ya Walawi 11:29-30
[29]Tena katika vitu vile vitambaavyo, vitambaavyo juu ya nchi, hivi ni najisi kwenu; kicheche, na panya, na mjombakaka, kwa aina zake,
[30]na guruguru na kenge, na mjusi na goromoe, na lumbwi.
[31]Wanyama hao ndio walio najisi kwenu katika hao watambaao; awaye yote atakayewagusa, wakiisha kufa, atakuwa ni najisi hata jioni.
Lumbwi /kinyonga ni mmoja wa wanyama ambao walikuwa najisi kuliwa au kuguswa mizoga yake.
Unaweza ukajiuliza ni kwanini Mungu amweke kama kundi la wanyama najisi ni kwasababu ya tabia yake ya kujibadilisha badilisha kutokana na mazingira.
Na hata leo hii wapo watu ambao Mungu anawaona ni vinyonga rohoni. Na hivyo sikuzote wanakuwa najisi mbele zake.
Utakuta leo anatembea na Mungu vizuri lakini akikutana tu na watu wa kidunia anakaa kama mtu wa kidunia..au leo anamsifu Mungu kweli katika Roho kesho yupo disco anamwimbia shetani na kumchezea kwa shangwe kabisa..ni mtu ambaye anabadilika kutokana na mazingira. Na hiyo ni hatari sana.
Bwana atufumbue macho yetu..tusiwe wakina lumbwi. Tumfuate Kristo kila mahali..tusibadilishwe na mazingira yoyote..viwango vyetu viwe vilevile bila kujali tunapitia nini sasa, moto au baridi. Tuwe walewale kwa Bwana.
Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

ZIKUMBUKE FADHILI ZA MUNGU

Biblia inamaanisha nini inaposema “Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake”?

Wibari ni nani?(Mithali 30:26)

POPOBAWA NI KWELI YUPO?

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2021/11/01/lumbwi-ni-nini-katika-biblia/