Je kuchonga Nywele na Ndevu ni dhambi?

by Admin | 17 June 2022 08:46 pm06

Jibu: Kabla ya kupata jibu la swali hili, hebu tujiulize kwanza swali lifuatalo: Je! Kuchonga nyusi (kuzitinda) ni dhambi??

Kama kuchonga nyusi ni dhambi, au ni kosa au ni jambo lenye taswira mbaya, na lisilopendeza basi pia kuchonga nywele za kichwani au kidevuni pia ni dhambi.. kwasababu zote ni nywele na zipo katika eneo la kichwa. Kama tutamhukumu anayechonga nyusi na tukamwacha anayechonga ndevu au nywele za kichwani, basi tutakuwa wanafiki!!.

Ni jambo gumu kidogo kulipokea lakini ukweli ndio ukweli, kuwa Wote wanaochonga ndevu, au vichwa vyao, au Nyusi zao, wanaenda kinyume na Neno la Mungu.  Na mimi nilikuwa hivyo zamani, lakini nimebadilika!..na nitazidi kubadilika kama nitagundua kuna mambo mengine ambayo nayafanya yanayokinzana na Neno au kanuni zake.

Tumepewa ruhusa ya kuzipunguza nywele zetu, lakini si kuzichonga!..tunapozichonga tunajitoa katika uhalisia na kwenda katika udunia, na kufanana na watu wa kidunia.

Sasa kwa kusema hivi sio kwamba tusiwe watanashati! La!.. tunapaswa tujiweke watanashati, lakini bila kuharibu uhalisia wetu.

Maandiko yanasema..

Walawi 19:27 “MSINYOE DENGE pembe za vichwani, wala msiharibu pembe za ndevu zenu”.

Sasa Neno “kunyoa denge” tafsiri yake ni “kuchonga panki” .. Hivyo maana ya huo mstari ni huu “Walawi 19:27 “Msichonge pembe za vichwani, wala msiharibu pembe za ndevu zenu”.

Maandiko yanasema miili yetu ni Hekalu la Roho mtakatifu, na kupitia miili yetu, tunahubiri injili kwa watu walio nje! Hivyo kimwonekano na kimwenendo hatupaswi kufanana kabisa na watu ambao wapo nje ya wokovu..

Kwasababu wakituona tunafanana nao watajiona wao wapo sawa katika njia zao mbaya, na mwisho wa siku ndio tunahubiri uvuguvugu ambao Kristo aliukataa na kuulaani katika kitabu cha Ufunuo 3:16.

1Wakorintho 3:16 “Hamjui ya kuwa NINYI MMEKUWA HEKALU LA MUNGU, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?

17 Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Je kwa mkristo aliyeokoka, ni dhambi kunyoa ndevu zake?

NGUVU YA MNADHIRI WA BWANA.

Kwanini ndugu wanaokaa pamoja wawe kama mafuta ya Haruni?

Panda/ Sauti ya panda ni nini kibiblia?(Danieli 3:5)

KUJIPAMBA NI DHAMBI?

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2022/06/17/je-kuchonga-nywele-na-ndevu-ni-dhambi/