Mambo yale yaliyo mbali, na yale yaendayo chini sana,

by Admin | 13 October 2022 08:46 pm10

SWALI: Je! maneno tunayoyasoma katika Mhubiri 7:24, yana maana gani?

[24]Mambo yale yaliyo mbali, na yale yaendayo chini sana, ni mtu yupi awezaye kuyatafuta?


JIBU:  Hapo Kuna vitu viwili.. 

1) Yale yaliyo mbali.

       2) Yale yaendayo chini sana.

Akimaanisha yaendayo mbali na upeo wa mwanadamu..na hayo si mengine zaidi ya mambo ya mbinguni, na kuzimu na ya maisha baada ya hapa..yatakuwa na mwonekano gani..picha yake halisi ipoje, miaka bilioni moja kutoka sasa watakatifu watakuwa wanafanya nini?..Hayo hakuna mtu anayeweza kuyavumbua isipokuwa Mungu tu peke yake.

Na yale yaendayo chini sana, maana yake ni yale yaliyositirika kama madini n.k. ambayo yenyewe yanapatikana chini sana. Hivyo vitu vilivyositirika/ siri za Mungu, ni mwanadamu gani anaweza kuzivumbua..

Kwamfano Siku ya unyakuo itakuwa lini, kabla ya uumbaji Mungu alikuwa anafanya nini,  maji yanajaaje kwenye mawingu, yaliyo hewa tu, halafu baadaye yanamwagika chini kama mvua, mifupa unajiumbaje ndani ya tumbo la mama mjamzito, mapigo ya moyo yanadundishwa kwa nishati gani, mpaka  hayachoki n.k Siri hizo anazo Mungu tu hakuna awezaye kuzivumbua..

Ayubu 11:7 inasema..

[7]Je! Wewe waweza kuuvumbua ukuu wa Mungu?  Waweza kuufikilia upeo wa huyo Mwenyezi?

Soma Kitabu cha Ayubu kuanzia sura ya 38-41, utaona Mungu anamuuliza mwanadamu maswali magumu ambayo mpaka sasa hakuna hata moja lililopatiwa jibu lake.

Hiyo ndio maana ya huo mstari;

Mhubiri 7:24

[24]Mambo yale yaliyo mbali, na yale yaendayo chini sana, ni mtu yupi awezaye kuyatafuta?

Yatosha sisi kumwamini yeye na kulitii Neno lake tu. Kwasababu hata tukijitahidi vipi kwa akili zetu kamwe hatutaweza kuzivumbua siri za ndani za Mungu wetu, isipokuwa yeye mwenyewe atufunulie.

Jina lake BWANA lihimidiwe. milele na milele. Amen.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Birika ni nini?, na yale Matao matano katika birika la Bethzatha ni nini?.

MUME / MKE BORA KUTOKA KWA BWANA UTAMWONA UKIWA KATIKA MAZINGIRA GANI?

nini maana ya kujikana nafsi na kujitwika msalaba?

HUJAPEWA MBAWA ZA KUKIMBIA MATATIZO

Nini maana ya ugonjwa wa kufisha? (Yeremia 17:9)

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2022/10/13/mambo-yale-yaliyo-mbali-na-yale-yaendayo-chini-sana/