Usimwache rafiki yako mwenyewe, wala rafiki ya baba yako.

by Admin | 27 February 2023 08:46 pm02

SWALI: Mstari huu una maana gani?

Mithali 27:10 “Usimwache rafiki yako mwenyewe, wala rafiki ya baba yako, Wala usiende nyumbani mwa ndugu yako siku ya msiba wako. Afadhali jirani aliye karibu kuliko ndugu aliye mbali”


JIBU: Ni mstari unaolenga umuhimu wa marafiki wema katika maisha yetu. Hapo anaanza kwa kusema usimwache rafiki yako mwenyewe, lakini haishii tu kwa rafiki yako, anaendelea kusema pia hata rafiki wa baba yako. Kwasababu wanaweza wakawa msaada kwako wa karibu kuliko ndugu wakati mwingine.

Kauli hiyo haimaanishi kuwa ndugu hawana msaada, hapana, lakini kutegemea tu ndugu peke yake, na kuwapuuzia marafiki wema kwaweza kukukwamisha, kwamfano umezidiwa na ugonjwa chumbani kwako, na unahitaji huduma ya kwanza, hapo huwezi kumpigia simu ndugu yako aliye mkoa mwingine, au wilaya nyingine aje kukusaidia, ni wazi kuwa msaada wa kwanza utauhitaji kutoka kwa jirani yako.

Ndio maana ya huo mstari, usimwache rafiki yako mwenyewe, yaani usimpuuzie, wala usimpuuzie rafiki wa Baba yako hata kama sio rafiki yako. Marafiki wa ndugu zetu, mara nyingi hufanyika msaada mkubwa kwetu wakati mwingine, Hili ni jambo la kawaida katika jamii, mara nyingi tumeona marafiki wa wazazi, au wa ndugu zetu wakitumika kutusaidia kwa sehemu moja au nyingine.

Lakini tukiwa ndani ya Kristo, tunapata marafiki ambao ni zaidi hata ya ndugu, kwasababu wao, husukumwa na upendo wa Kristo ambao umezidi wote. Bwana ameahidi hivyo kwamba tukiacha vyote kwa ajili ya jina lake, basi hayo yote atatujalia (Marko 10:30).

Je! Umeokoka? Je! Unatambua kuwa hizi ni nyakati za mwisho, na Yesu yupo mlangoni kurudi? Maisha yako yapo kwa nani. Kama upo nje ya Kristo ni heri ukatubu sasa, kwasababu mlango wa neema unakaribia kufungwa, kisha ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo kama hukubatizwa, ili upate ondoleo la dhambi na upokee kipawa cha Roho Mtakatifu, ikiwa utahitaji msaada huo basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618 / +255789001312.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

USIWE ADUI WA BWANA

Rafiki hupenda sikuzote; Na ndugu amezaliwa kwa siku ya taabu.

Usimwache mwanamke mchawi kuishi! Biblia ilimaanisha nini?

BASI, IWENI NA HURUMA, KAMA BABA YENU ALIVYO NA HURUMA

Je ni kweli Musa alikuwa mtu mpole kuliko wote duniani?

KWA HIYO NDUGU, VUMILIENI, HATA KUJA KWAKE BWANA.

NDUGU,TUOMBEENI.

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2023/02/27/usimwache-rafiki-yako-mwenyewe-wala-rafiki-ya-baba-yako/