Bwana Yesu alizaliwa katika nchi gani?

by Admin | 6 April 2024 08:46 pm04

Bwana YESU KRISTO alizaliwa katika Nchi/Taifa la ISRAELI, lililopo mashariki ya kati. Na mji aliozaliwa ni Bethlehemu ambao ulikuwa katika urithi wa kabila la YUDA.

Mika 5:2 “Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele”.

Pamoja na kwamba Bwana YESU alizaliwa Bethlehemu kulingana na unabii huo wa Mika, lakini hakulelewa katika huo mji wa Bethlehemu badala yake wazazi wake waliishi mahali palipojulikana kama NAZARETI, Mji mdogo sana uliopo kaskazini mwa Taifa hilo la Israeli, na huko ndiko Kristo alikokulia, ndio maana mahali pengine anajulikana kama Mnazorayo (yaani mtu wa Nazareti).

Mathayo 2:23 “akaenda, akakaa katika mji ulioitwa Nazareti; ili litimie neno lililonenwa na manabii, Ataitwa Mnazorayo”.

Lakini pia Mji huo wa Nazareti ulikuwa ndani ya Wilaya iitwayo Galilaya, wakati mji wa Bethlehemu aliozaliwa Bwana YESU ulikuwa katika Wilaya iliyoitwa Yudea au Uyahudi.

Wilaya ya Galilaya ndio uliyojumuisha miji mingine midogo midogo kama Kapernaumu na Korazini na Bethsaida, ambapo wanafunzi wengi wa Bwana YESU walitokea katika hiyo miji, na ndio miji ambayo iliona miujiza mingi ya Bwana YESU lakini haikutubu (Mathayo 11:21)…. Wakati Wilaya ya Uyahudi ndio iliyobeba miji ya Bethlehemu pamoja na Yerusalemu.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba BWANA YESU alizaliwa Bethlehemu ya Uyahudi na kulelewa Nazareti ya Galilaya, na alifia YERUSALEMU na kuzikiwa hapohapo, na kufufuka hapo hapo YERUSALEMU. Na sasa yupo hai na atarudi tena mara ya pili na siku hizo zimekaribia kulingana na unabii wa biblia.

Je umeokoka?

Bwana YESU ANARUDI.

Kama unatamani kuokoka basi fuatiliza sala hii >>KUONGOZWA SALA YA TOBA

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Bwana Yesu alizaliwa mwaka gani?

Raheli aliwalilia vipi watoto wake?

BADO UPO YERUSALEMU TU..GALILAYA HUTAKI KWENDA

Yerusalemu ni nini?

AKAZIDI KUENDELEA KATIKA HEKIMA NA KIMO.

Rudi Nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2024/04/06/bwana-yesu-alizaliwa-katika-nchi-gani/