Kwanini biblia ni neno la Mungu?

by Admin | 8 July 2024 08:46 pm07

Swali: Je ni kweli biblia ni Neno la Mungu?


Kabla ya kujibu kwanini biblia ni Neno la Mungu, na si kitabu kingine chochote?… hebu tujiulize kwanza na tujadili kwanini

Biblia ni Neno la Mungu kwasababu lina maneno yaliyo hai..

Vivyo hivyo biblia ni kitabu cha Mungu, kwasababu kimebeba taarifa sahihi kumhusu Mungu.. Na taarifa KUU ndani ya kitabu hiko kitukufu, ni taarifa ya mwanadamu kuondolewa dhambi kupitia YESU KRISTO (Hiyo ndiyo taarifa kuu) ambayo inaleta “UZIMA WA MILELE KWA MTU”..Na ndio karama kuu ya MUNGU kwetu.

Warumi 6:23 “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

Vitabu vingine vyote vilivyosalia havijabeba suluhisho lolote la ondoleo la dhambi za Mtu, badala yake zimebeba tu taarifa za maadili, au staha, mambo ambayo yanapatikana hata katika vitabu vya sheria za nchi.

Lakini taarifa na njia ya ondoleo la dhambi zipo katika BIBLIA TU PEKE YAKE!!!..

Kwasababu “dhambi” ndio sumu pekee ya mwanadamu, na hiyo ndio kizuizi kikubwa cha mtu kumkaribia Mungu, hivyo mtu akiondolewa hiyo anakuwa ameokoka! Hata kama maisha yake hapa duniani bado yanaendelea.

Na ni kwa njia gani mtu anaondolewa dhambi zake moja kwa moja??

Matendo 2:36 “ Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulibisha kuwa Bwana na Kristo.

37 Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38 Petro akawaambia, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, MPATE ONDOLEO LA DHAMBI ZENU, NANYI MTAPOKEA KIPAWA CHA ROHO MTAKATIFU”.

Kanuni ya kuondolewa dhambi, ni kutubu na kubatizwa (Marko 16:16). Na toba halisi ni ile inayotoka moyoni yenye madhamirio ya kugeuza mwelekeo moja kwa moja. Na ubatizo sahihi ni ule wa maji mengi (Yohana 3:23) na kwa jina la BWANA YESU (Matendo 8:16, na Matendo 19:5).

BWANA YESU AKUBARIKI.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JIPE NAFASI KATI YA TAARIFA UNAYOIPOKEA NA MAAMUZI UNAYOYATOA.

UNYAKUO WA KANISA UMEPITA LEO!!

UPEPO WA KUSI HULETA MVUA;

NENO LA MUNGU KATIKA UTIMILIFU WOTE.

UWEZA WA MUNGU NJE YA WAKATI.

Rudi Nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2024/07/08/kwanini-biblia-ni-neno-la-mungu/