by Admin | 11 November 2024 08:46 am11
Jibu: Turejee..
Mwanzo 9:27 “Mungu AKAMNAFISISHE Yafethi, Na akae katika hema za Shemu; Na kaanani awe mtumwa wake”
Kunafisisha ni “KUTOA NAFASI au KUTANUA” .. Kwani mzizi wa neno hilo ni “Nafasi”…hivyo andiko hilo tunaweza kuliweka hivi… “Mungu akamtanue Yafethi, Na akae katika hema za Shemu; Na kanaani awe mtumwa wake”
Kwanini Mungu amtanue Yafethi na kumlaani Kanaani?.
Ni kwasababu Hamu alifanya dhambi ya kuutazama uchi wa baba yake.
Mwanzo 9:20 “Nuhu akaanza kuwa mkulima, akapanda mizabibu;
21 akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake.
22 Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake, akawaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje. 23 Shemu na Yafethi wakatwaa vazi, wakalitanda mabegani mwao wote wawili, wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao; na nyuso zao zilielekea nyuma, wala hawakuuona uchi wa baba yao.
24 Nuhu akalevuka katika ulevi wake, akajua mwana wake mdogo alivyomtendea.
25 Akasema, Na alaaniwe Kaanani; Atakuwa mtumwa kabisa kwa ndugu zake”.
Je umempokea YESU?.. Kama bado basi wakati uliokubalika ni sasa, fanya maamuzi kabla kabla hazijaja siku za hatari.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Hema ya kukutania ni nini, na ilikuwaje?
KWANINI NABII ISAYA ALIAGIZWA KUHUBIRI UCHI?
Je shauri la kuipepeleza Kanaani lilitoka kwa wana wa Israeli au kwa BWANA?
Source URL: https://wingulamashahidi.org/2024/11/11/kunafisisha-ni-kufanyaje-mwanzo-927/
Copyright ©2025 unless otherwise noted.