Category Archive Mafundisho

JINSI MATENDO YA IMANI YANAVYOWEZA KULETA UTAMBULISHO MPYA KWA MTU.

Jina la Bwana na Mwokozi wetu YESU KRISTO libarikiwe daima.

Je unajua matendo ya Imani, yanaweza kuleta utambulisho mwingine kwako tofauti na ule wa kwanza, na kibali kipya.

Turejee Biblia, kisa cha Daudi kumwua Goliati, biblia inaonyesha kuwa kabla ya Daudi kumwua Goliati, alikuwa anaishi nyumbani kwa Mfalme Sauli katika jumba la kifalme, na kazi yake pale ilikuwa ni kupiga kinubi, wakati roho mbaya ilipomjia Sauli.

1Samweli 16:21 “Basi Daudi akamwendea Sauli, akasimama mbele yake, naye akampenda sana; naye akapata kuwa mtu wa kumchukulia silaha zake.

22 Kisha Sauli akapeleka watu kwa Yese, akasema, Tafadhali, MWACHE DAUDI ASIMAME MBELE YANGU; MAANA AMEONA KIBALI MACHONI PANGU.

23 Ikawa, ile roho mbaya kutoka kwa Mungu ilipomjilia Sauli, ndipo Daudi akakishika kinubi, akakipiga kwa mkono wake, naye Sauli akaburudishwa, na ile roho mbaya ikamwacha”.

Hapa tunaona tayari Mfalme Sauli amemjua Daudi na tena amemfanya kuwa mchukua silaha wake, sasa ni ngumu kumfanya mtu kuwa mchukua silaha, kama bado hujamjua wala kumkubali.

Lakini tukiendelea kusoma habari hii mbele kidogo baada ya Daudi kumwua Goliati tunaona jambo lingine la kushangaza.. kwamba Sauli anamwuliza tena Daudi yeye ni mwana wa nani, kana kwamba alikuwa hamjui hapo kwanza..

1Samweli 17:54 “Naye Daudi akakitwaa kichwa chake yule Mfilisti na kukileta Yerusalemu; lakini silaha zake akaziweka hemani mwake.

55 Basi Sauli, hapo alipomwona Daudi akitoka ili kumwendea yule Mfilisti, alimwambia Abneri, jemadari wa jeshi, Je! Abneri, kijana huyu ni mwana wa nani? Abneri akamjibu, Ee mfalme, kama iishivyo roho yako, mimi siwezi kusema.

56 Basi mfalme akasema, Uliza wewe, KIJANA HUYU NI MWANA WA NANI.

57 Hata na Daudi alipokuwa yuarudi kutoka katika kumwua yule Mfilisti, Abneri alimtwaa, akamleta mbele ya Sauli, naye anacho kichwa chake yule Mfilisti mkononi mwake

58 Basi Sauli akamwuliza, Wewe, kijana, u mwana wa nani? Naye Daudi akamjibu, Mimi ni mwana wa mtumishi wako, Yese, mtu wa Bethlehemu.”

Kama Daudi asingefanya tendo lile la imani na kishujaa, la kumwua Goliati, Mfalme asingemjua Daudi, ingawa tayari alishajitambulisha kwake na hata kuishi naye… Baada ya tukio hilo tunazidi kuona kibali cha Daudi kuongezeka kwa kiwango kingine.

1Samweli 18:1 “Ikawa Daudi alipokwisha kusema na Sauli, roho ya Yonathani, ikaambatana na roho ya Daudi, Yonathani akampenda kama roho yake mwenyewe”.

Hapo kabla Yonathani huwenda alikuwa anamwona Daudi kama mwimba ngojera tu! kwenye nyumba ya mfalme.

Kama Goliati akiendelea kusimama katika maisha yako usipomwangusha kwa imani unaweza kuendelea kubaki pale pale, lakini kama ukichukua mawe matano kama Daudi na kumwangusha chini, basi hapo umefungua kibali kipya!..  Jina lako linakuwa sio lile lile tena, nafasi yako sio ile ile tena, kujulikana kwako kunakuwa sio kule kule tena.

Goliati ni roho yoyote inayojiinua ya vitisho, na Goliati wa kwanza katika maisha yetu ni Dhambi!.. Huyu ndiye anayesumbua!, ndiye anayeficha kibali chetu, ndiye anayeficha nafasi zetu na kutuzuilia kusonga mbele, tukiweza kumwangusha huyu na jeshi lote la wafilisti (magonjwa, shida, na mambo mengine yatesayo) yanakimbia, na tunabaki washindi na wenye kibali kingine.

Je umetubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha?..kama bado ni nini unasubiri?.. kumbuka kuomba msamaha sio kutubu, bali toba halisi inakamilishwa kwa kuacha matendo yote mabaya ya giza, maana yake baada ya kuomba msamaha wa dhambi kutoka kwa MUNGU, kinachofuata ni kuacha zile njia mbaya, ikiwemo kujitenga na makundi ya watu yanayopalilia dhambi iliyokuwa inakusumbua.

Vile vile kuacha kufanya vitu, au kuangalia vitu vilivyokuwa vinakukosesha, na pia kuacha kuvaa mavazi yaliyokuwa yanakaribisha dhambi maishani mwako. Kwa kufanya hivyo utakuwa umemwangusha Goliati na kubali chako kitaongezeka kama ilivyokuwa kwa Daudi.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kwanini MUNGU alimzuia Daudi asimjengee HEKALU? (1Nyakati 17:12)

Daudi alikuwa na wake wangapi, na je ni halali kuwa na wake wengi?

Waanaki ni watu gani katika biblia?

JE! UNAWEZA KUWA NA GEUKO KAMA LA DAUDI?

Je! aliyemwua Goliathi ni Daudi au Elhanani.

Print this post

UFAHAMU UFUNGUO WA KUMPENDA BWANA ZAIDI

Je unaujua ufunguo wa wewe kumpenda Bwana zaidi?.. kuna jambo ukilifanya basi upendo wako kwa MUNGU utaongezeka kwa kiwango kikubwa sana.. Utajikuta unampenda MUNGU zaidi, unamheshimu zaidi na unamtumikia zaidi.

Na ufunguo huo si mwingine zaidi ya kuutafakari MSAMAHA WAKE KWAKO KWA MAPANA!.. Unaweza kuona jambo la msahama kwako ni dogo tu!.. Lakini nataka nikuambie Msamaha wa MUNGU kwako una uhusiano mkubwa sana na UPENDO WAKO KWAKE!.

Maandiko yanasema “aliyesamehewa sana hupenda sana, na aliyesamehewa kidogo hupenda kidogo”

Luka 7:47 “Kwa ajili ya hayo nakuambia, Amesamehewa dhambi zake ambazo ni nyingi kwa kuwa amependa sana; lakini asamehewaye kidogo, huyo hupenda kidogo”.

Hebu tafakari huu mfano: Mtu mmoja alikuwa anadaiwa shilingi 500 na mwenzake na akasamehewa na mwingine aliukwa anadaiwa shilingi laki 5 na mtu huyo huyo mmoja, naye pia akasamehewa kiasi chote cha pesa (shilingi laki 5)..

Je yupi kati ya hao wadaiwa wawili waliosamehewa, atampenda zaidi Yule aliyewasamehe?.. Bila shaka Yule aliyesamehewa deni kubwa ndiye atakayempenda zaidi aliyemsamehe, na hata kumheshimu sana..

Lakini Yule aliyesamehewa deni dogo, anaweza kuwa mtu wa shukrani lakini si katika kiwango kikubwa, na wala hawezi kutoa heshima ya kiwango kikubwa kwa yule aliyemsamehe.

Ni hivyo hivyo katika upande wa Imani, watu waliojiona ni wenye dhambi nyingi na kubwa kubwa!, na kujiona kama hawajastahili msahama kwa makosa yao, wanapoungama na kupokea msamaha, huwa wanampenda sana Bwana YESU na kumheshimu.

Lakini watu wanaojiona ni wasafi au watakatifu sana, kwamba hawamkosei sana MUNGU huwa hata upendo na MUNGU hawana, au upo kwa kiwango kidogo.

Sasa kiuhalisia wote tumemkosea MUNGU pakubwa sana!.. ukijiona huna dhambi nyingi, basi fahamu kuwa kuna shida kwako ya kutafakari, ambayo hiyo sasa ndio unapaswa ushughulike nayo.

Unapaswa ushughulike na hiyo hali mpaka ifikie hatua ujijue kuwa hukustahili, na wewe ulikuwa ni mbaya mno, na mbovu, na makosa yako yalikuwa makubwa sana!.. ukiweza kufikia hiyo tafakari, basi jua matunda yako ni wewe kumpenda BWANA na kumheshimu sana.

Unawezekana wewe sio mwizi, au muuaji au mzinzi lakini hebu tafakari vipindi ulivyomsema ndugu yako, na MUNGU alikufumbia macho, ingawa ulistahili adhabu ya mauti papo kwa hapo.

Hebu tafakari vipindi ulivyotamani vitu visivyofaa moyoni mwako, na MUNGU alikufumbia macho ingawa ulistahili kufa papo kwa hapo.

Hebu tafakari vipindi ulivyokasirika bila sababu, tafakari vipindi uliyokuwa unawaza mawazo mabaya, tafakari vipindi ulivyodanganya na kusema uongo, tafakari vipindi miguu yako ilipokuwa inaelekea kufanya maovu, tufakari vipindi ulivyotukana mdomoni na moyoni mwako, tafakari mambo ya upumbavu uliyoyafanya mitandaoni,  hayo yote si kwamba MUNGU alikuwa haoni, au hata sasa hayaoni, anayaona yote!.

Inawezekana hujawahi kuua, lakini tafakari vipindi ulivyokuwa mbinafsi, tafakari visasi na vinyongo ulivyokuwa navyo, na huenda unavyo hata sasa, tafakari udunia wote ulioufanya, rudi nyuma kumbuka tukio moja baada ya lingine katika maisha yako, yatakafari sana halafu fikiri YESU AMEJITWIKA makosa yako yote hayo, ambayo kama si rehema zake huenda ungekuwa umeshakufa na upo KUZIMU sasa!.

Lakini alikizuia kifo kisikupate!, umempa nini?, au una umaalumu gani hata akusamehe hayo yote?, kwani waliokufa bila kupata huu msamaha wana kasoro gani zaidi yako?.

Je huoni kama aliyekupa huu msahama ni wa thamani kubwa? Huoni kama amekusamehe makubwa sana.. bado humpendi tu!.. ungepaswa uwe kuzimu muda huu, lakini bado unaishi! Bado kwako unamwona vile vile?

Ndugu tenga muda sana utafakari msamaha wa YESU, kwani ndio uliobeba funguo za kumpenda YESU zaidi, Ukiutafakari msamaha wa YESU utaishia kumpenda, lakini pia kumwogopa (kutokutenda dhambi tena)

Zaburi 130:4 “Bwana, kama Wewe ungehesabu maovu, Ee Bwana, nani angesimama?

4 Lakini kwako kuna msamaha, Ili Wewe uogopwe”.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NGUVU YA MSAMAHA

UMUHIMU WA KUOMBA MSAMAHA.

NI KWA NAMNA GANI KRISTO ALIZIBEBA DHAMBI ZETU?

JE UMEUPOKEA UWEZA WOTE WA UUNGU NDANI YAKO?

Hadhari ni nini kibiblia? (Mithali 1:4)

Print this post

Ni kwanini manabii wa uongo, wanaweza kutoa pepo kwa jina la YESU?

Swali: Inakuwaje manabii wa uongo wanakuwa na uwezo wa kutoa pepo kwa jina la YESU?, na ilihali hawana mahusiano na Mungu wa kweli? je ni nguvu gani wanazitumia? Za Mungu au shetani?.


Jibu: Zipo aina mbili za manabii wa uongo. Aina ya kwanza ni ile inayotumia nguvu za giza asilimia mia moja (100%), kundi hili halihusishi kabisa jina la YESU katika huduma zake, wala halimhubiri YESU wa kweli bali shetani.

Hawa wanakuwa ni wachawi waliovaa suti na kushika biblia, na Neno la MUNGU linasema tutawatambua kwa matunda yao, na si mwonekano wao wa nje.

Kundi la Pili: la manabii wa Uongo, ni wale ambao sio wachawi lakini halina mahusiano na MUNGU, maana yake aidha wanamtumikia MUNGU kwa faida za matumbo yao, au walishamwacha MUNGU na kufuata akili zao, kundi hili ndio hatari zaidi kwasababu bado linaweza kutumia jina la YESU na miujiza ikatendeka.

Mtu anakuwa kashapoteza mahusiano na MUNGU lakini bado upako anao!.. utauliza hilo linawezekanaje?.. Mkumbuke MUSA!.. Bwana MUNGU alimwambia auambie mwamba utoe maji, lakini yeye pamoja na ndugu yake Haruni, hawakumsikiliza MUNGU wakaenda kufanya kinyume na walivyoagizwa, na jambo la ajabu ni kwamba ijapokuwa walikuwa wameenda kinyume na agizo la MUNGU (wapo nje na mpango wa Mungu) lakini walipouchapa mwamba ulitoa maji, binafsi ningetegemea maji yasitoke mwambani kwasababu walikuwa nje na agizo la MUNGU, lakini haikuwa hivyo.

Hesabu 20:6 “Musa na Haruni wakatoka pale palipokuwa mkutano, wakaenda hata mlangoni pa hema ya kukutania, wakaanguka kifudifudi; utukufu wa Bwana ukawatokea.

7 Bwana akasema na Musa, akinena,

8 Twaa ile fimbo, ukawakusanye mkutano, wewe na Haruni ndugu yako, ukauambie mwamba mbele ya macho yao utoe maji yake, nawe utawatokezea maji katika mwamba, na hivyo utawanywesha maji mkutano na wanyama wao.

9 Musa akaitwaa hiyo fimbo kutoka mbele za Bwana kama alivyomwamuru.

10 Musa na Haruni wakawakusanya kusanyiko mbele ya mwamba, akawaambia, Sikieni sasa, enyi waasi; je! Tuwatokezee maji katika mwamba huu?

11 Musa akainua mkono wake akaupiga ule mwamba kwa fimbo yake mara mbili; maji yakatoka mengi, mkutano wakanywa na wanyama wao pia.

12 Bwana akamwambia Musa na Haruni, Kwa kuwa hamkuniamini mimi, ili kunistahi mbele ya macho ya wana wa Israeli, basi kwa sababu hiyo, hamtawaingiza kusanyiko hili katika ile nchi niliyowapa”.

Umeona hapo?.. ijapokuwa Musa alikuwa anatembea nje ya agizo la MUNGU, lakini bado upako alikuwa nao, na manabii wa uongo ni hivyo hivyo, wanaweza kuwa wanatembea na upako wa MUNGU wa kweli lakini hawana MUNGU maishani mwao, na mwisho wao ni mbaya…na hawa tumeambiwa tutawatambua kwa matunda yao na si upako wao, wala mwonekano wao.

Mfano mwingine ni Yule nabii mzee tunayemsoma katika biblia, aliyemwambia uongo nabii mwenzake, na badala nguvu za MUNGU zimwondoke baada ya kusema kwake uongo, kinyume chake ndio kwanza anapokea unabii mwingine kumhusu mwenzie. Soma habari hiyo katika 1Wafalme 12:11-30.

Ikifunua kuwa unabii, au muujiza au upako mtu/mtumishi alionao sio kipimo cha kwanza cha kumtambua nabii/mtumishi wa Mungu wa kweli, bali ni mtu kuwa na mahusiano mazuri na MUNGU, kwani maandiko yanasema Yohana Mbatizaji hakufanya ishara wala muujiza hata mmoja lakini mbinguni alihesabika kuwa  mkuu kuliko manabii wote na watu wote wa agano la kale (Yohana 10:41 na Mathayo 11:11).

Na tena Bwana YESU alisema wengi watakuja siku ile wakisema,  hatukutoa pepo na kufanya unabii kwa jina lako?.. na yeye atasema siwajui mtokako! (Mathayo 7:21-22).

Ili kumtambua kuwa huyu ni Nabii wa kweli na si wa uongo, ni matunda anayoyatoa.. Maana yake Matunda ya maisha yake, na matunda ya kazi yake.

Matunda ya maisha yake ni jinsi anavyoishi, je anazaa matunda ya Roho mtakatifu tunayoyasoma katika Wagalatia 5:22?.. au ni mtu wa namna gani?..kama maisha yake si kulingana na Neno la MUNGU bali ni mtenda dhambi, basi huyo hata kama anauwezo wa kusimamisha jua, bado hatupaswi kudanganyika kwake.

Vile vile kama matunda anayoyazaa kutokana na kazi yake (maana yake watu anao wahubiria) hawawi wasafi mwilini na rohoni, hiyo ni ishara nyingine ya kumtambua nabii huyo kuwa si wa MUNGU. Kwani kama watu anaowatengeneza hawana tofauti na wa ulimwengu, maana yake matunda yake si matunda ya kiMungu bali ya adui.

Hiyo ndio namna pekee ya kuwapima manabii au wachungaji au waalimu au mitume wa kweli na wale wa uongo, na tunapowafahamu biblia imetuonya tujihadhari nao.

Mathayo 7:15 “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.

16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti? 17 Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya.

18 Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri.

19 Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni.

20 Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua.

21 Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Ni mji gani mtakatifu shetani aliomchukua Bwana YESU? (Mathayo 4:5)

SADAKA INAHARIBU NGUVU ZA MADHABAHU ZA MASHETANI.

SADAKA INAHARIBU NGUVU ZA MADHABAHU ZA MASHETANI.

NI KWA NAMNA GANI SHETANI ANAIZUIA INJILI?

MTAWATUPIA MBWA NYAMA HIYO.

Print this post

Tunathibitisha vipi kuwa Yule Malaika wa (Yohana 5:4) ni wa MUNGU?

Swali: Je! tunaweza kuthibitisha vipi kuwa Yule malaika aliyekuwa anashuka na kuyatibua maji alikuwa ni malaika wa MUNGU na si wa shetani, kwasababu maandiko yanasema  kuwa shetani naye anaweza kujigeuza na kuwa mfano wa malaika wa nuru (2Wakorintho 11:14).

JIbu: Turejee..

Yohana 5:1 “Baada ya hayo palikuwa na sikukuu ya Wayahudi; naye Yesu akakwea kwenda Yerusalemu. 2 Na huko Yerusalemu penye mlango wa kondoo pana birika, iitwayo kwa Kiebrania Bethzatha, nayo ina matao matano.

3 Ndani ya hayo jamii kubwa ya wagonjwa walikuwa wamelala, vipofu, viwete, nao waliopooza, [wakingoja maji yachemke.

4 Kwa maana kuna wakati ambapo MALAIKA HUSHUKA, AKAINGIA KATIKA ILE BIRIKA, AKAYATIBUA MAJI. Basi yeye aliyeingia wa kwanza baada ya maji kutibuliwa, AKAPONA UGONJWA WOTE ULIOKUWA UMEMPATA.]”

Ni kweli Biblia inasema shetani anaweza kujigeuza na kuwa mfano wa Malaika wa Nuru, lakini haisemi kuwa anaweza kujigeuza na kuwa Malaika wa Nuru, bali mfano wa..

Kwahiyo huyu tunayemsoma hapa katika Yohana 5:4 hakuwa malaika wa giza, kwasababu matunda yake si ya giza kwani Maandiko yanasema “shetani hawezi kumtoa shetani mwenzake”.

Mathayo 12:25 “Basi Yesu akijua mawazo yao, akawaambia, Kila ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, hufanyika ukiwa; tena mji au nyumba yo yote ikifitinika juu ya nafsi yake, haitasimama.

26 Na SHETANI AKIMTOA SHETANI, AMEFITINIKA JUU YA NAFSI YAKE; basi ufalme wake utasimamaje?”

Sasa wote waliokuwa wamelala pale walikuwa wanasumbuliwa na magonjwa yaliyoletwa na mapepo, kwasababu asilimia kubwa ya magonjwa yanasababishwa na mapepo (soma Mathayo 9:32 na Mathayo 12:22).

Sasa kwa mantiki hiyo haiwezekani malaika wa giza kushuka na kuwatoa malaika wenzake wa giza (yaani mapepo) wenzao ndani ya watu, ni jambo ambalo haliwezekani!, vinginevyo ufalme wa giza usingesimama, kwahiyo Yule malaika alikuwa anashuka kuyatibua maji ni malaika wa Nuru na si wa giza.

Jambo la ziada la kujifunza ni kwamba watu wanaokwenda kwa waganga wa kienyeji kwaajili ya kutatuliwa shida zao au magonjwa yao na baada ya kupiga ramli wanaona kama wamepona..

 Kiuhalisia ni kwamba hawajatatuliwa matatizo yao bali ndio yameongezwa, kwamfano mtu ataenda kwa mganga akiwa na tatizo la homa, na anaaguliwa na kujiona amepona kabisa, na kuambiwa kuwa majini yamefukuzwa ndani yake.

Sasa kiuhalisia kulingana na biblia yale mapepo hayajaondoka!, bali yamehamishwa kutoka sehemu moja ya mwili kwenda nyingine, au kutoka sehemu moja ya maisha kwenda nyingine, lakini si kwamba yamefukuzwa/kuondolewa kabisa kutoka katika maisha yake,

 Maana yake sasa huyu mtu atapata unafuu kwenye kifua kilichokuwa kinamshumbua, au kwenye mguu, lakini lile pepo limehamia kwenye tumbo, au miguu, au limepelekwa kusababisha matatizo mengine katika maisha ya Yule mtu, na tena mtu anayeenda kwa mganga anakuwa anaongezewa mapepo mengine kwa ajili ya matatizo mengine yatakayotokea wakati huo huo au wakati mwingine huko mbeleni, kwasababu shetani kamwe hawezi kumtoa shetani mwenzake.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

BIRIKA LA SILOAMU.

Birika ni nini?, na yale Matao matano katika birika la Bethzatha ni nini?.

JE BADO UNASUBIRIA MAJI YACHEMKE?

AKAWAPONYA WALE WENYE HAJA YA KUPONYWA

WAKO WATATU WASHUHUDIAO MBINGUNI NA DUNIANI.

Print this post

Je kibiblia ni sahihi kuadhimisha jumapili ya mitende?

Swali: Je ni vema sisi tuliookoka kushika matawi siku ya jumapili na kuingia nayo kanisani au kutembea nayo?


Jibu:  Jumapili ya mitende ni jumapili moja kabla ya jumapili ya pasaka, ambapo katika historia ni siku ambayo KRISTO aliingia YERUSALEMU, na watu wakakata matawi ya mitende na kuyatandaza njiani ili Bwana YESU apite. (kumbuka, mtende ni mti unaozaa matunda ya tende).

Mathayo 21:1 “Hata walipokaribia Yerusalemu, na kufika Bethfage, katika mlima wa Mizeituni, ndipo Yesu alipotuma wanafunzi wawili akiwaambia,

2 Enendeni mpaka kijiji kile kinachowakabili, na mara mtaona punda amefungwa, na mwana punda pamoja naye; wafungueni mniletee.

3 Na kama mtu akiwaambia neno, semeni, Bwana anawahitaji; na mara huyo atawapeleka.

4 Haya yote yamekuwa, ili litimie neno lililonenwa na nabii, akisema,

5 Mwambieni binti Sayuni Tazama, mfalme wako anakuja kwako, Mpole, naye amepanda punda, Na mwana-punda, mtoto wa punda.

6 Wale wanafunzi wakaenda zao, wakafanya kama Yesu alivyowaamuru,

7 wakamleta yule punda na mwana-punda, wakaweka nguo zao juu yao, naye akaketi juu yake.

8 Watu wengi katika ule mkutano wakatandaza nguo zao njiani; NA WENGINE WAKAKATA MATAWI YA MITI, WAKAYATANDAZA NJIANI.

9 Na makutano waliotangulia, na wale waliofuata, wakapaza sauti, wakisema, Hosana, Mwana wa Daudi; ndiye mbarikiwa, yeye ajaye kwa jina la Bwana; Hosana juu mbinguni.

10 Hata alipoingia Yerusalemu, mji wote ukataharuki, watu wakisema, Ni nani huyu?

11 Makutano wakasema, Huyu ni yule nabii, Yesu, wa Nazareti ya Galilaya”.

Sasa swali ni je! Na sisi ni sahihi/ruksa kuisheherekea/kuiadhimisha hii siku?

Jibu: Hatujapewa agizo lolote kwenye Biblia la kuiadhimisha jumapili ya mitende, wala jumapili ya pasaka. Isipokuwa kutokana na umuhimu wa hizo siku katika historia ya Ukristo, si vibaya kuzifanya hizo siku/tarehe kuwa za ibada ya kutafakari mambo yaliyotokea wakati huo.

Kwamfano katika jumapili ya mitende, ni wakati ambao watu walimsifu YESU kwa kumwimbia Hosana Hosana (yaani Okoa). Nasi kwa kutafakari jambo hilo twaweza kutengeneza kama igizo la wakati huo, na kumwimbia Bwana kwa furaha tukisema Hosana amebarikiwa yeye ajaye kwa jina la BWANA, kwa kufanya hivyo huku tumeshika matawi ya mitende sio kosa wala dhambi kwani ni sehemu ya sifa tu kama sifa nyingine zinazohusisha shangwe za kurusha rusha leso juu au matawi ya miti.

Lakini matawi yale yakifanyika kama ni vitu vitakatifu, (kwamba vimebeba nguvu Fulani ya kiungu, kama vile sanamu zinazowekwa kwenye baadhi ya makanisa) hilo ni kosa, kwani tayari hizo ni ibada za sanamu, na si tena kwa lengo la sifa za kumtukuza MUNGU.

Utakuta mtu anatembea na tawi lile si kwa lengo la sifa, wala tafakari ya mambo yaliyotokea miaka elfu mbili iliyopita, bali kama kisaidizi cha kuondoa mikosi, au matatizo, au cha kufukuzia wachawi n.k Huyu mtu anakuwa anafanya ibada za sanamu, na inaweza isiwe ni kosa lake bali la waliomfundisha.

Kwahiyo jumapili ya mitende si vibaya kuadhimishwa ikiwa itafanyika kwa ufunuo na maarifa namna hiyo, lakini kama itafanyika kidini na kidesturi, inageuka kuwa ibada ya sanamu, jambo ambalo ni machukizo kwa BWANA.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini Maana ya Hosana?

AKAUKAZA USO WAKE KWENDA YERUSALEMU.

MUNGU AKETIYE MAHALI PA JUU PALIPOINUKA.

Ni mji gani mtakatifu shetani aliomchukua Bwana YESU? (Mathayo 4:5)

EPUKA KUJIFANYA HUJUI.

Print this post

Ipi tofauti kati ya Uhai na Uzima kibiblia?

Jibu: Turejee maandiko machache..

“Uhai” ni hali ya kuwa “HAI” (yaani kuishi) ili kiumbe kiwe kinaishi ni lazima kipumue, kile, kikue na hata kijongee. Hizo ndizo tabia chache za viumbe HAI,  Wanadamu, wanyama na mimea vyote vina uhai kwasababu vinapumua, vinaongezeka na pia kujongea.

Lakini “UZIMA” Umeenda mbali zaidi kuelezea UHAI wa kiroho ambao unapatikana kwa mtu kuwa na mahusiano na MUNGU.

Uhai unaelezea mwili lakini Uzima unaelezea roho. Mimea haina UZIMA bali ina UHAI.. wanyama hawana UZIMA bali wana UHAI maandiko yanaonyesha hivyo…

Mithali 12:10 “Mwenye haki huufikiri UHAI WA MNYAMA WAKE; Bali huruma za mtu mwovu ni ukatili”.

Na UZIMA unapatikana kwa mmoja tu ambaye ni YESU KRISTO,

Yohana 10:10 “Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili WAWE NA UZIMA, kisha wawe nao tele”.

ikiwa na maana kuwa wanadamu yoyote aliye nje ya YESU KRISTO anao “Uhai” tu kama wanyama lakini hawana “Uzima”… anapumua, anakula, anatembea lakini akisha kufa hana UZIMA tena.. Lakini aliye ndani ya KRISTO, hata akiwa amekufa ataendelea kwasababu anao  UZIMA wa MILELE alioupokea kutoka kwa YESU.

Je unao uzima wa milele ndani yako?…Je YESU ni sehemu ya maisha yako?

Yohana 17:2 “kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili, ili kwamba wote uliompa awape UZIMA WA MILELE.

3 Na UZIMA WA MILELE ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na YESU KRISTO ULIYEMTUMA”.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE! UPO KATIKA MAJI YA UTULIVU?

Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?

SIKU ZA MWISHO ZA UHAI WANGU.

Kwanini pawekwe MITI pale bustanini na si kitu kingine?.

Uzao wa Ibrahimu unamilikije mlango wa adui? (Mwanzo 22:17)

Print this post

SHUKA UPESI

Luka 19:1 “Naye alipoingia Yeriko alipita katikati yake.

2 Na tazama, palikuwa na mtu, jina lake Zakayo, mkubwa mmoja katika watoza ushuru, naye ni tajiri.

3 Huyu alikuwa akitafuta kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, asiweze kwa sababu ya umati wa watu, maana ni mfupi wa kimo.

4 Akatangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu apate kumwona, kwa kuwa atakuja kuipitia njia ile.

5 Na Yesu, alipofika mahali pale, alitazama juu, akamwambia, Zakayo, SHUKA UPESI, KWA KUWA LEO IMENIPASA KUSHINDA NYUMBANI MWAKO.

6 Akafanya haraka, akashuka, akamkaribisha kwa furaha”.

YESU hawezi kuingia nyumbani kwako kama “hutashuka kwenye Mkuyu”..

Mkuyu ni kitu chochote kijiinuacho juu ya  YESU,…. Kiburi cha mali ni mkuyu,… kiburi cha cheo ni mkuyu, kiburi cha uzuri ni Mkuyu n.k.. Mtu anavyovitumia hivi ili kumwona Bwana YESU au kumtumikia, Kristo yeye anaenda kinyume navyo..

Zakayo asingeweza kuzungumza na Bwana akiwa juu ya mkuyu..ilimpasa ashuke upesi… Sauti ile ilikuwa na mamlaka, ilipenya katika moyo wa Zakayo na kumfanya ashuke si tu chini ya Mkuyu, bali hata kiburi chake chote, kwani alikuwa ni mtu mkubwa kifedha…

Alipokubali  tu kushuka na kiburi chake cha mali nacho kikashuka, kiburi chake cha cheo kikashuka akawa mtu mwingine, mnyenyekevu na YESU akaingia nyumbani mwake..

Nusu ya mali yake aliwapa maskini na wote aliowadhulumu aliwarudishia mara nne.

Luka 19:6 “Akafanya haraka, akashuka, akamkaribisha kwa furaha.

7 Hata watu walipoona, walinung’unika wote, wakisema, Ameingia kukaa kwa mtu mwenye dhambi.

8 Zakayo akasimama, akamwambia Bwana, Tazama, Bwana, nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimenyang’anya mtu kitu kwa hila namrudishia mara nne.

9 Yesu akamwambia, Leo wokovu umefika nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Ibrahimu.

10 Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea”.

Na wewe leo, shuka chini ya Mkuyu.. kiburi cha Elimu kinaweza kuwa kizuizi cha Kristo kutembea na wewe, kiburi cha pesa kinaweza kuwa kikwazo cha YESU kuingia kwako, kiburi cha cheo na uzuri ni hivyo hivyo, lakini unyenyekevu unaleta Neema.

Yakobo 4:6 “Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NINI MAANA YA KUTUBU

ALIYOKUTANA NAYO YESU, YERIKO.

JE YESU AMEJIAMINISHA KWAKO?

LEO WOKOVU UMEFIKA NYUMBANI HUMU

JE! WEWE NI MWANA WA IBRAHIMU?

Print this post

OMBA JAMBO KATIKA MAJIRA YAKE.

Zekaria 10:1 “Mwombeni Bwana mvua wakati wa masika, naam, Bwana afanyaye umeme, naye atawapa manyunyu ya mvua, kila mtu atapewa nyasi kondeni”.

Umewahi kujiuliza kwanini hapo maandiko yanasema “Mwombeni Bwana mvua WAKATI WA MASIKA” na si wakati mwingine wowote kama kiangazi?..

Ni kwasababu msimu wa masika ni msimu wa mvua, hivyo inapotokea hakuna mvua si jambo la kawaida, kwahiyo tukiomba mvua msimu huo ni hoja yenye nguvu, lakini tunapoomba mvua msimu wa kiangazi zinakuwa si hoja zenye nguvu!.. Ndicho maandiko yanachokimaanisha hapo.

Maombi ya kuomba kwa wakati ni mazuri na yana majibu ya haraka kuliko yale ya kuomba nje ya msimu/majira.

Unaomba mume/mke  na bado ni mwanafunzi, unaomba mali na bado unasoma, unaomba umtimikie MUNGU na bado hujaokoka!, maombi ya namna hiyo ni nadra sana kujibiwa!.. ni wachache sana wanaojibiwa hayo maombi!!.. sio kwamba ni maombi mabaya au vinavyoombwa ni vitu vibaya!. La! Ni vizuri lakini vinaombwa nje ya majira yake.

Hapo maandiko yanasema “Mwombeni Bwana Mvua wakati wa Masika”..  Maana yake ni lazima ujue uhusiano wa kile unachomwomba MUNGU na majira uliyopo. Kama kitu bado majira yake usitumie nguvu kubwa kuomba, shughulika na vile ambavyo sasa ndio majira yake.

Kama wewe ni mwanafunzi usiombe MUNGU akupe hela kwa sasa….badala yake mwombe akufanikishe katika masomo ufaulu, uwe kichwa, hayo mengine bado msimu wake!..

Kama wewe ni binti/kijana na bado upo chini ya wazazi unawategemea, usiombe MUNGU akuonyeshe mume wako/mke wako, badala yake mwombe ulinzi juu ya tabia yako mpaka utakapofika wakati wa wewe kujitegemea na kufikiri kuingia katika ndoa.

Lakini kama umeshaingia katika msimu basi ni haki yako kumwomba BWANA!, Na unapomwomba Bwana jambo sahihi katika msimu sahihi, MUNGU ni mwenye huruma atakupa unachokihitaji haraka sana, na hata kikichelewa atakupa sababu kwanini kinachelewa, na sababu za BWANA zote ni Bora na wala si za kumwumiza Mtu, kwasababu yeye kamwe hawezi kuruhusu tujaribiwe kupita tuwezavyo.

Vumilia tu ukiona umeshaingia kwenye msimu na bado matokeo hujayaona!, yatakuja tu!..usikate tama a wala kuishiwa nguvu, mwamini MUNGU na mngojee, naye atakupa nguvu mpya kila siku.

Jambo la mwisho la kujua ni kwamba wokovu pia unao msimu wake, na msimu wa Wokovu ndio sasa..

Huu ndio wakati wa MUNGU kutupa wokovu na kutusikia maombi yetu, kwani utafika wakati ambapo hakutakuwa tena na wokovu wala maombi kusikiwa, ndivyo maandiko yanavyosema..

2Wakorintho 6:1 “Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure.

2 (Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia; tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa)

Sasa kama  siku ya Wokovu ndio sasa, unasubiri nini usimpokee YESU?.. je unadhani itakuwa hivi siku zote?.. utafika wakati mlango wa Neema utafungwa, na hakutakuwa tena na msamaha wa dhambi wala ondoleo la dhambi, mti ulipoangukia huko huko utalala (Mhubiri 11:3).

Sasa unayadharau mahubiri na mafundisho ya uzima, unayoyapokea kila mahali yanayokuonya kuhusu dhambi, je unadhani hali itakuwa hivyo kila siku?…Majira yatabadilika ndugu, utafika wakati kutakuwa hakuna kuponywa tena mwili na roho!.

2Nyakati 36:15 “Naye Bwana, Mungu wa baba zao, akatuma kwao kwa mikono ya wajumbe wake, akiondoka mapema, na kutuma; kwa sababu aliwahurumia watu wake, na makao yake;

16 lakini waliwadhihaki wajumbe wa Mungu, na kuyadharau maneno yake, na kuwacheka manabii wake, HATA ILIPOZIDI GHADHABU YA BWANA JUU YA WATU WAKE, HATA KUSIWE NA KUPONYA”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nzige, Parare, madumadu na tunutu ni wadudu gani? (Yoeli 2:25)?

MAASI KUONGEZEKA NI ISHARA YA NINI?.

JIFUNZE JAMBO KWENYE UKOO WA YESU, UWE NA AMANI

Kwanini madhabahu zilitengenezwa kwa mawe yasiyochongwa?

Kwanini Mungu auweke Mti wa Mema na Mabaya katikati ya bustani?

Print this post

Je ni Petro au Mariamu Magdalene aliyekuwa wa kwanza kutokewa na Bwana YESU?

Swali: Kati ya Simoni Petro na Mariamu Magdalene ni yupi aliyekuwa wa kwanza kutokewa na Bwana YESU baada ya kufufuka kwake?, kwa maana katika Luka 24:34 tunasoma kuwa ni Simoni ndiye wa kwanza kutokewa na Bwana, lakini tukirudi katika Marko 16:9 tunaona ni Mariamu Magdalene je hii imekaaje?.


Jibu: Turee mistari hiyo..

Luka 24:33 “Wakaondoka saa ile ile, wakarejea Yerusalemu, wakawakuta wale kumi na mmoja wamekutanika, wao na wale waliokuwa pamoja nao,

34 wakisema, Bwana amefufuka kweli kweli, NAYE AMEMTOKEA SIMONI”.

Hapa tunaona anatajwa Simoni, lakini turejee Marko 16:9..

Marko 16:9 “Naye alipofufuka alfajiri siku ya kwanza ya juma, ALIMTOKEA KWANZA MARIAMU MAGDALENE, ambaye kwamba alimtoa pepo saba.

10 Huyo akashika njia akawapasha habari wale waliokuwa pamoja naye, nao wakali wanaomboleza na kulia”.

Hapa tunasoma ni Mariamu Magdalena ndiye aliyetokewa kwanza, sasa swali ni yupi aliye sahihi au biblia inajichanganya?..

Jibu ni La! Biblia haijichanganyi na wala haina kasoro yoyote… Sasa kama ni hivyo ni nani aliyetokewa wa kwanza?

Jibu, aliyetokewa wa kwanza na Bwana YESU alikuwa ni MARIAMU MAGDALENE, kama maandiko yanavyoonyesha hapo juu (Marko 16:9).. huyu ndiye aliyekuwa wa kwanza kumwona Bwana kwani baada tu ya kukuta jiwe limeviringishwa mbali na kaburi aliondoka na kwenda kuwafuata akina Petro kuwapasha yaliyojiri, na Petro pamoja na Yohana walipokwenda kaburini kuhakiki hizo taarifa za Magdalene,  walikuta tu vitambaa vya sanda, na walipoondoka ndipo Bwana YESU akamtokea Mariamu Magdalene kama mtu wa kwanza (na saa hiyo akina Petro wameshaondoka).

Yohana 20:1 “Hata siku ya kwanza ya juma Mariamu Magdalene alikwenda kaburini alfajiri, kungali giza bado; akaliona lile jiwe limeondolewa kaburini.

2 Basi akaenda mbio, akafika kwa Simoni Petro na kwa yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, akawaambia, Wamemwondoa Bwana kaburini, wala hatujui walikomweka.

3 Basi Petro akatoka, na yule mwanafunzi mwingine, wakashika njia kwenda kaburini.

4 Wakaenda mbio wote wawili; na yule mwanafunzi mwingine akaenda mbio upesi kuliko Petro, akawa wa kwanza kufika kaburini.

5 Akainama na kuchungulia, akaona vitambaa vya sanda vimelala; lakini hakuingia.

6 Basi akaja na Simoni Petro, akaingia ndani ya kaburi; akavitazama vitambaa vilivyolala,

7 na ile leso iliyokuwako kichwani pake; haikulala pamoja na vitambaa, bali imezongwa-zongwa mbali mahali pa peke yake.

8 Basi ndipo alipoingia naye yule mwanafunzi mwingine aliyekuwa wa kwanza wa kufika kaburini, akaona na kuamini.

9 Kwa maana hawajalifahamu bado andiko, ya kwamba imempasa kufufuka.

10 Basi wale wanafunzi wakaenda zao tena nyumbani kwao.

11 Lakini Mariamu alikuwa akisimama karibu na kaburi, nje yake, analia. Basi akilia hivi, aliinama na kuchungulia ndani ya kaburi.

12 Akaona malaika wawili, wenye mavazi meupe, wameketi, mmoja kichwani na mmoja miguuni, hapo ulipolazwa mwili wake Yesu.

13 Nao wakamwambia, Mama, unalilia nini? Akawaambia, Kwa sababu wamemwondoa Bwana wangu, wala mimi sijui walikomweka.

14 Naye akiisha kusema hayo, akageuka nyuma, akamwona Yesu amesimama, asijue ya kuwa ni Yesu.

15 Yesu akamwambia, Mama, unalilia nini? Unamtafuta nani? Naye, huku akidhania ya kuwa ni mtunza bustani, akamwambia, Bwana, ikiwa umemchukua wewe, uniambie ulipomweka, nami nitamwondoa.

16 Yesu akamwambia, Mariamu. Yeye akageuka, akamwambia kwa Kiebrania, Raboni! (Yaani, Mwalimu wangu)”.

Hivyo baada ya kumtokea Mariamu Magdalena ndipo akamtokea Simoni Petro, katika tukio ambalo halijarekodiwa katika Biblia.

Kwahiyo Simoni Petro alikuwa ni Mtume wa kwanza kutokewa na Bwana YESU lakini si mtu wa kwanza, aliyekuwa wa kwanza ni Mariamu Magdalena na Simoni Petro anasimama kuwa wa kwanza kati ya Mitume wa Bwana.

Mtume Paulo analiweka hilo vizuri zaidi..

1Wakorintho 15:4 “na ya kuwa alizikwa; na ya kuwa alifufuka siku ya tatu, kama yanenavyo maandiko;

5 na ya kuwa ALIMTOKEA KEFA; tena na wale Thenashara;

6 baadaye aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano pamoja; katika hao wengi wanaishi hata sasa, ila baadhi yao wamelala;

7 baadaye akamtokea Yakobo; tena na mitume wote;

8 na mwisho wa watu wote, alinitokea mimi, kama ni mtu aliyezaliwa si kwa wakati wake”.

Je umempokea YESU?.. Unao uhakika wa kwenda naye mawinguni atakaporudi?… fahamu kuwa tunaishi majira ya siku za mwisho, siku yoyote parapanda ya mwisho inalia na wafu waliokufa katika Kristo watafufuliwa kuungana na walio hai katika Kristo na kunyakuliwa juu, je utakuwa wapi siku hiyo?, ikiwa leo habari ya msalaba kwako ni upuuzi mtupu!.

Neema ya Bwana YESU itusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mariamu Magdalene ni nani. Na hilo jina amelitolea wapi?

MAMBO YA KUJIFUNZA KWA KLOPA NA MKE WAKE!

Nyongeza ya majina ya watu katika biblia

MUONEKANO MPYA WA YESU BAADA YA KUFUFUKA.

UFUFUO WA UZIMA NA WA HUKUMU.

Print this post

ONDOA UDANGANYIFU KATIKA MAISHA YAKO.

Jina la Mwokozi YESU libarikiwe.

Wakati Fulani Bwana YESU aliuona “Mtini” (yaani mti unaozaa matuna aina ya Tini) usio na matunda na matokeo yake aliulaani.

Mathayo 21:18 “Hata asubuhi alipokuwa akienda mjini, aliona njaa.

19 Akaona mtini mmoja kando ya njia, akauendea, asione kitu juu yake ila majani tu; AKAUAMBIA, YASIPATIKANE MATUNDA KWAKO TANGU LEO HATA MILELE. MTINI UKANYAUKA MARA.

20 Wanafunzi walipoona, walistaajabu, wakisema, Jinsi gani mtini umenyauka mara?”

Sasa ukifuatilia vizuri hii habari utaweza kufikiri kwamba  Bwana YESU alikuwa anaweza kuwa amekosea kuulani.., kwani ule mtini haukuwa msimu wake wa kuzaa matunda…

Hata wewe ukienda kutafuta machungwa kwenye mchungwa nje na msimu wake ni wazi kuwa hutashangazwa pale utakapokuta ule mchungwa hauna tunda lolote.Zaidi sana utashangazwa kama endapo umefika msimu halafu hukukuta machungwa.. Lakini sasa tunasoma Bwana YESU ilikuwa kinyume chake alijua kabisa si msimu wake Mtini kuzaa lakini aliulaani hivyo hivyo.

Sasa kwanini aulaani??

Sababu zipo nyingi, lakini hii yaweza kuwa kuu kuliko zote… ULE MTINI ULIONYESHA SIFA ZOTE  ZA NJE  KUWA NA MATUNDA lakini haukuwa na matunda! (Maana yake ulikuwa unahubiri udanganyifu).

Unaonaje  umewekewa bahasha tatu mbele yako, halafu kati ya hizo bahasha tatu mbili zinaonekana kabisa kwa macho kuwa ndani hazina kitu, lakini moja inaonekana imetuna (kana kwamba ina fedha), halafu unaichagua hiyo iliyotuna kisha ndani unakuta hamna kitu, bila shaka utakwazika na unaweza ukaichana ile bahasha, ili isiendelee kudanganya wengine.

Vivyo hivyo Kristo alijua kabisa ule si wakati wa Tini kwani mitini mingine  yote ilikuwa na sifa zinazofanana kwa wakati huo, lakini ajabu ni kwamba huu Mtini mmoja ulikuwa na mwonekano wa tofauti kana kwamba unao matunda, pengine wakati mitini mingine ilikuwa imekauka inapukutisha huu ulikuwa na majani mabichi, ulikuwa unahubiri udanganyifu kwamba unao matunda na kumbe hauna, na ili kuondoa udanganyifu huo suluhisho ni kukatwa/kulaaniwa.

Naam na maisha ya wakristo wengi yamejaa UDANGANYIFU, ni kama wanasifa zote za kuitwa wakristo lakini ukichunguza kwa undani hawana matunda!. Kwa nje wana majina ya kikristo, ni wahubiri,  wana biblia nzuri na kubwa, wana nafasi katika kanisa, lakini ndani si wakristo, hawana matunda!, ni watu vuguvugu wale Bwana aliosema atawatapika katika Ufunuo..

Ufunuo 3:15 “Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.

16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.

17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi”.

Toka katika uvuguvugu, ili kuepuka laana ya KRISTO, kama umekusudia kuwa Moto, kuwa Moto mpendwa, kama umeamua kuchagua baridi maandiko yanasema ni heri uwe baridi kabisa kuliko kuwa hapo katikati, vuguvugu..

Bwana YESU atusaidie sana.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Tafsiri ya Mithali 27:18 Yeye autunzaye mtini atakula matunda yake;

Je Bwana YESU alipanda mlimani na wanafunzi wake baada ya siku sita au nane?

MWISHO WA MAVUNO, NI MWISHO WA DUNIA.

Biblia unapozungumzia kuhusu kupewa jina jipya inamaanisha nini?

Nini tofauti ya Uwezo na Uweza kibiblia?

Print this post