KUOTA UNAENDESHA GARI.

by Admin | 15 October 2019 08:46 pm10

Awali ya yote ni vizuri kufahamu kuwa asilimia kubwa ya ndoto tunazoota kila siku au mara kwa mara huwa zinatokana na mawazo yetu wenyewe, naweza kusema hata asilimia 95 ya ndoto zote tuziotazo usiku hutokana na sisi wenyewe, na hizo zinakuja  aidha kwa shughuli tunazozifanya kila siku au mazingira yanayotuzunguka au kitu tunachokiwaza sana…

Hivyo ndoto kama hizi, huwa hazibebi ujumbe wowote wa rohoni, ikitokea umeota  wewe zipuuzie tu vinginevyo utajikuta unachanganyikiwa ukidhani kuwa kila ndoto unayoota ina maana, ikiwa bado hujaweza kuzitofautisha aina za ndoto katika makundi yake basi pitia kwanza somo hili ili upate msingi kisha tuendelee. >>>NITAJUAJE KAMA NDOTO NI YA MUNGU AU YA SHETANI?

Lakini kama ndoto unayoota haihusiani na mazingira uliyopo, na huwa inajirudia mara kwa mara, basi lipo jambo ambalo Mungu anataka kukuonyesha hapo.

Sasa Kuota unaendesha gari na wakati mwingine umewapakiza watu nyuma,  ni ishara kwamba wewe mwenyewe unayaongoza maisha yako au maisha ya wengine, kukufikisha mahali Fulani au kuwafikisha mahali fulani..Kama wewe umeokoka na unalifanya kusudi la Mungu au unaifanya kazi ya Mungu basi zidisha mwendo katika safari yako kwasababu lengo lako utalifikia, kama hutapunguza mwendo kama alivyofanya Yehu, pale alipokuwa anakwenda kumuua Yule mfalme muasi Yoramu na mama yake Yezebeli waliowakosesha Israeli mpaka kupelekea wakaingia kwenye uchawi na ibada za sanamu, na Kumkasirisha Mungu kwa viwango vya juu sana.

2Wafalme 9:20 Yule mlinzi akatoa habari, akasema, Amewafikilia wala harudi tena; na mwendo huu ni kama mwendo wa Yehu mwana wa Nimshi; MAANA ANALIENDESHA GARI KWA KASI.

Hivyo kama unalo kusudi la Mungu mkononi mwako,litimize bila kuogopa kipingamizi au mitazamo ya watu..

Lakini pia,

unapaswa uwe makini ni gari la aina gani unatumia kuliendesha kusudi la Mungu wakati Fulani mfalme Daudi alikuwa analitoa sanduku la Mungu kutoka kwa Abinadabu kwenda Yerusalemu, lakini alifanya makosa kuwatumia ng’ombe kama usafiri wa kulisafirisha kusudi la Mungu badala ya kutumia watu tena makuhani ambao ndio Mungu aliowaagiza walibebe wakati wote,  wao wakawaweka ng’ombe kama magudurumu ya gari lao na ikapelekea kifo cha mtu mmoja..soma 1Nyakati 13:7

1Nyakati 13:7 “Hivyo Wakalipandisha sanduku la Mungu juu ya gari jipya kutoka nyumba ya Abinadabu; na Uza na Ahio WAKALIENDESHA LILE GARI.

8 Wakacheza Daudi na Israeli wote, mbele za Mungu, kwa nguvu zao zote; na kwa nyimbo na kwa vinubi, na kwa vinanda, na kwa matari, na kwa matoazi, na kwa tarumbeta.

9 Hata walipofika penye uga wa Nakoni, Uza akaunyosha mkono wake alishike sanduku; kwa maana wale ng’ombe walikunguwaa.

10 Ndipo hasira ya Bwana ikawaka juu ya Uza, naye akampiga, kwa sababu alilinyoshea sanduku mkono wake, hata akafa pale pale mbele za Mungu.

Hivyo uwe makini unapolifanya kusudi la Mungu na wale unaowaongoza, zingatia vigezo cha maandiko . Na ndio maana wengine wanaota wanaendesha vyombo tofauti tofauti , wengine wanaota wanaendesha malori, wengine wanaota wanaendesha baiskeli, wengine wanaota wanaendesha pikipiki n.k. Vyovyote vile, kuendesha ni kuendesha tu, hiyo ni kulingana na kusudi Mungu alilokupa cha msingi hapo ni kutimiza kusudi hilo kwa ukamilifu wote, ili uepuke kulaumiwa huko mbeleni.

Lakini kama unajijua wewe bado ni mwovu na hadi sasa upo katika dhambi, Hiyo ni Ishara mbaya sana kwako, Aidha Unajiongoza mwenyewe katika mauti au unawaongoza wengine katika mauti, au vyote viwili kwa pamoja..

2Nyakati 21:12 “Likamjia andiko kutoka kwa Eliya nabii, kusema, Bwana, Mungu wa Daudi baba yako, asema hivi, Kwa sababu hukuziendea njia za Yehoshafati baba yako, wala njia za Asa mfalme wa Yuda;

13 lakini umeiendea njia ya wafalme wa Israeli, UKAWAENDESHA KATIKA UASHERATI Yuda na wenyeji wa Yerusalemu, kama walivyofanya nyumba ya Ahabu; tena umewaua ndugu zako wa nyumba ya baba yako, waliokuwa wema kuliko wewe;

14 tazama, Bwana atawapiga pigo kubwa watu wako, na watoto wako, na wake zako, na mali yako yote;

15 nawe utakuwa na ugonjwa mkuu kwa maradhi ya matumbo, yatakapotokea matumbo yako kwa sababu ya ugonjwa huo siku kwa siku.

Unaona hapo huyu mfalme Yehoramu, alikuwa mtu mwovu, alikuwa ni muuaji, na mwabudu sanamu, akawafanya na Israeli wote wote wawe kama yeye, au kwa lugha nyingine akawaendesha waisraeli mpaka kwenye uasherati wa kiroho, kwa sababu hiyo basi Mungu akampiga kwa mapigo yale..

Hata na wewe, unayaongoza maisha yako sasa ukidhani kuwa upo salama, lakini mwisho wake utakuwa ni mauti kama hutatubu, unawasababishia wengine mauti wale walio chini yako, au wanaokutegemea, au wanaokutazama kwa mwenendo wako na maisha yako..

Hivyo Bwana anakupenda na ndio maana anakuonya Leo hii, Utubu umgeukie yeye, ili uliendeshe gari la maisha yako katika njia sahihi ya kutimiza makusudi ya Mungu na sio makusudio ya Shetani.

Ubarikiwe.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

KUOTA UNAFANYA MTIHANI.

KUOTA UPO UCHI.

KUOTA UNAPAA.

KUOTA UNASAFIRI.

TOFAUTI KATI YA NDOTO NA MAONO NI IPI?

JE! KUBET NI DHAMBI?

AGANO LAKO LINABEBWA NA NANI?.


Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2019/10/15/kuota-unaendesha-gari/