TIMAZI NI NINI

by Admin | 11 November 2019 08:46 pm11

Timazi ni nini?

Ni kifaa kidogo kilichokuwa kinatumika zamani katika Ujenzi na hata sasa bado kinaendelea kutumika…kifaa chenye umbo la PIA. Kinakuwa kimetengenezwa kwa chuma kizito kidogo. Na kinafungwa kamba, na kuwa katika hala ya kuning’inia. Na kinaning’inizwa kutokea juu ya ukuta kwenda chini.

Kifaa hichi kinamsaidia mjenzi kujua kama Ukuta wake umenyooka au la!.

Katika Biblia kifaa hichi kimetajwa mara kadhaa (Soma 2Wafalme 21:13, Isaya 28:19-17 na Zekaria 4:10,). Na kifaa hiki kimekuwa kikiwakilisha Upimwaji wa Taifa la Israeli. Bwana alipotaka kutumia lugha ya kupima kiwango cha maovu au wema, mara nyingi alitumia lugha ya kijenzi.

Ndio maana utaona Mfalme Nebkadneza baada ya kumchukiza Mungu aliambiwa “Amepimwa katika Mizani na kuonekana umepunguka” (Danieli 5:27). Kiuhalisia mtu hawezi kuwekwa kwenye mizani ya nafaka na kupimwa!..Hapana bali utaona hiyo ni lugha tu ya kuonesha kiwango cha maovu cha mtu huyo. Mfano mwingine tunaona kwa Nabii Amosi.

Amosi 7:6 “Bwana akaghairi katika jambo hili pia. Jambo hili halitakuwa, asema Bwana MUNGU.

7 Haya ndiyo aliyonionyesha; na tazama, Bwana alisimama karibu na ukuta uliojengwa kwa timazi, mwenye timazi mkononi mwake.

8 Bwana akaniambia, Amosii, unaona nini? Nikasema, Naona timazi. Ndipo Bwana akasema, Tazama, nitaweka timazi kati ya watu wangu Israeli; sitawapita tena kamwe”

Hata sasa Bwana ameshika TIMAZI juu ya mtu mmoja mmoja, na juu ya Ulimwengu kwa Ujumla..Anayapima matendo ya kila mtu, aangalie kama yamepunguka! au la!. Kama yanampendeza basi mtu huyo atapata rehema na thawabu kutoka kwa Mungu na kupendwa sana, lakini kama yamepunguka basi kuna hatari ya kuhukumiwa kama Mfalme Nebkadneza alivyohukumiwa.

Je matendo yako yanastahili hukumu au thawabu?. Jibu unalo. Kama hujampa Yesu Kristo maisha yako. Mlango wa Neema upo wazi, fanya hima uingie, kabla siku muda wako wa kuishi duiniani haujaisha.

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

KAMA MUNGU ANABORESHA KAZI ZAKE, KWANINI WEWE USIBORESHE ZA KWAKO?.

KUACHA KUVUTA SIGARA.

KUOTA UPO UCHI.

KUOTA UNAPAA.

KUSAMBAA KWA ROHO YA MPINGA-KRISTO.

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2019/11/11/timazi-ni-nini/