Je mtu akifa anakuwa hana dhambi tena?

by Admin | 5 July 2020 08:46 pm07

 Je ni kweli mtu akifa anakuwa hana dhambi tena kufuatia hili andiko Warumi 6:7 “kwa kuwa yeye aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi.”


JIBU: Bwana Yesu alisema haya maneno mahali Fulani…

Yohana 8:21 “Basi akawaambia tena, Mimi naondoka, nanyi mtanitafuta; nanyi MTAKUFA KATIKA DHAMBI yenu; mimi niendako ninyi hamwezi kuja………

24 Kwa hiyo naliwaambieni ya kwamba MTAKUFA KATIKA DHAMBI ZENU; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye, MTAKUFA KATIKA DHAMBI ZENU”.

Bwana Yesu aliwaambia Waandishi na Mafarisayo maneno hayo..kuonyesha kuwa Kama mtu akikataa kutubu dhambi angali hai na kumwamini basi atakufa na hizo dhambi zake (maana yake hizo dhambi zake zitamfuata hata huko anakokwenda, na atahukumiwa kulingana na hizo).

Hilo utalithibitisha katika andiko hili..

1Timotheo 5:24 “Dhambi za watu wengine zi dhahiri, zatangulia kwenda hukumuni; wengine dhambi zao zawafuata”.

Kwasababu hiyo basi mstari huo wa Warumi 6:7, haumaanishi kuwa mtu mwenye dhambi anapokufa basi anakuwa hana dhambi tena…bali unamaanisha kuwa mtu “yeye aliyekufa Pamoja na Kristo, amehesabiwa haki mbali na dhambi”…Maana yake mtu aliye ndani ya Kristo hakuna hukumu ya adhabu juu yake kwasababu anakuwa amevuka kutoka mautini kuingia uzimani, ingawa bado anaishi ulimwenguni.

Ndio maana ukianzia mstari wa 6 na kuendelea kidogo mpaka wa 8 utaelewa vizuri..anasema..

Warumi 6: 6 “mkijua neno hili, ya kuwa utu wetu wa kale ulisulibishwa pamoja naye, ili mwili wa dhambi ubatilike, tusitumikie dhambi tena;

7 kwa kuwa yeye aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi.

8 Lakini tukiwa tulikufa pamoja na Kristo, twaamini ya kuwa tutaishi pamoja naye”

Hivyo andiko hilo linatuhusu sisi sote…Hatuna budi kufa Pamoja na Kristo, kila mmoja wetu kwa kumwamini yeye na kutubu dhambi na kufufuka Pamoja naye kwa njia ya ubatizo wa maji na wa Roho Mtakatifu.

Warumi 6:3 “Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake?

4 Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima”

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

USIFE NA DHAMBI ZAKO!

TUMAINI NI NINI?

NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU.

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/07/05/je-mtu-akifa-anakuwa-hana-dhambi-tena/