Nini maana ya Shalom na Maran atha

by Admin | 6 August 2020 08:46 am08

Utauwa umewahi kusikia maneno haya mawili yakitamkwa miongoni mwa wakristo. (Shalomu na Maranatha) Lakini pengine huelewi maana yake!.

Nini maana ya Shalomu?

Shalomu au Shalom ni neno la kiebrania lenye maana ya “AMANI” Kwa kiingereza “PEACE”. Hivyo wayahudi pamoja na wakristo wa kanisa la kwanza walipokutana walisalimiana na kwa salamu ya neno hilo “Shalomu”.

Pia Mungu wetu jina lake ni YEHOVA-SHALOMU, maana yake “Mungu wa amani”

Waamuzi 6:22 “Gideoni akaona ya kuwa ni malaika wa Bwana; Gideoni akasema, Ole wangu, Ee Bwana MUNGU! Kwa kuwa nimemwona Bwana uso kwa uso.

23 Bwana akamwambia Amani iwe pamoja nawe; usiogope; hutakufa.

24 Ndipo Gideoni akamjengea Bwana madhabahu hapo, akaiita jina lake, Yehova-Shalomu; hata hivi leo iko huko katika Ofra ya Waabiezeri”.

Kasome pia Warumi 15:33, Warumi 16:20, Wafilipi 4:9, 1Wathesalonike 5:23, Waebrania 13:20

Na Bwana wetu Yesu anajulikana kama Mfalme wa Amani (kasome Isaya 9:6, Waebrania 7:2).

Hivyo kama Mungu wetu ni Mungu wa Amani na mwana wake wa pekee Yesu Kristo ni Bwana wa Amani, Basi na sisi pia tunapaswa tuwe watu wa Amani na watu wote ili tufanane na yeye, na sio Amani ya midomo tu! bali ya vitendo. Neno Shalom litokapo vinywani vyetu liwe ni udhihirisho wa kitu kinachoendelea katika maisha yetu kwamba tunayo Amani na watu wote. Na lisiwe linatoka tu vinywani na huku mioyoni mwetu kuna unafiki, shari na chuki. Ukitamka tu! na huku moyoni mwako kuna vinyongo na hasira, na shari basi utakuwa hujaelewa nini maana ya shalomu.

Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”

1Petro 3:10 “Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme hila.

11 Na aache mabaya, atende mema; Atafute amani, aifuate sana“.

Maana ya Maran atha

Ni neno la kiebrania hivyo hivyo lenye maana ya “Bwana wetu anakuja” ni neno la Faraja kwa wakristo wote wanaomgonja Bwana....1Wakorintho 16:23

Bwana atubariki.

Shalom.


Tafadhali washirikishe na wengine na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

UBATIZO NI NINI NA ULIO SAHIHI NI UPI?

NI NINI TUNAJIFUNZA JUU YA MT. DENIS WA UFARANSA?

Je Mungu anawapenda watu wote au ana chuki?

MAMBO MENGINE HAYATOKI ISIPOKUWA KWA KUFUNGA.

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/08/06/nini-maana-ya-shalom-na-maran-atha/