Kutahayari ni nini katika biblia?(2Timotheo 2:15)

by Admin | 12 October 2020 08:46 pm10

Kutahayari maana yake ni kuweka katika aibu, kuaibisha, kuaibishwa, kuaibika.

Hivi ni baadhi ya vifungu vinavyolieeleza Neno hilo;

2Timotheo 2:15 “Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, ukitumia kwa halali neno la kweli”.

Hapo ni Paulo akimwambia Timotheo, ajitahidi kuishi maisha yanayopendeza Mungu, ili asiwe na sababu ya kuona aibu katika kuitenda kazi ya Mungu. Kwamfano kama Timotheo angekuwa ni mlevi, na huku anahubiri injili, asingekuwa na ujasiri wa kuwahubiria walevi, angeona aibu, lakini akijionyesha kwa matendo yake kuwa hanywi pombe, hataona aibu kuwahubiria walevi, hata tahayari.

Vifungu vingine ni kama hivi;

2Wakorintho 7:14 “Kwa maana, ikiwa nimejisifu mbele yake katika neno lo lote kwa ajili yenu, sikutahayarishwa; bali, kama tulivyowaambia mambo yote kwa kweli, vivyo hivyo na kujisifu kwetu kwa Tito kulikuwa kweli”.

(Maana yake sikuaibishwa)

2Wathesalonike 3:14 “Na ikiwa mtu awaye yote halishiki neno letu la waraka huu, jihadharini na mtu huyo, wala msizungumze naye, apate kutahayari”;

(Maana yake apate kuona aibu)

Ayubu 11:3 “Je! Majivuno yako yawanyamazishe watu wawe kimya? Nawe hapo ufanyapo dhihaka, je! Hapana mtu atakayekutahayarisha”?

(Maana yake atakayekuaibisha)

Soma pia;

Isaya 50:7 “Maana Bwana MUNGU atanisaidia; kwa sababu hiyo sikutahayari, kwa sababu hiyo nimekaza uso wangu kama gumegume, nami najua ya kuwa sitaona haya”.

2Wakorintho 7:14, Isaya 44:11.

Bwana akubariki.

Tafadhali angalia chini maana ya maneno mengine ya ki-biblia.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Neno Korbani linamaanisha nini? (Marko 7:11)

USIPIGE MATEKE MCHOKOO!

UTAJI ULIOKUWA JUU YA USO WA MUSA.

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

Mshulami ni msichana gani?

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/10/12/kutahayari-ni-nini-katika-biblia2timotheo-215/