Makanwa ni nini katika biblia? (Danieli 6:22)

by Admin | 1 December 2020 08:46 am12

Neno hilo tunaweza kulisoma katika kifungu hichi;

Danieli 6:22 “Mungu wangu amemtuma malaika wake, naye ameyafumba makanwa ya simba, nao hawakunidhuru; kwa kuwa mbele zake mimi nalionekana kuwa sina hatia; tena, mbele yako, Ee mfalme, sikukosa neno”.

Makanwa kwa jina lingine ni midomo.

Katika habari hiyo tunaona, baada ya Danieli kushitakiwa kwa makosa ambayo hakustahili kutokana na uaminifu wake kwa Mfalme Dario, walimkamata na kumtupa katika tundu la Simba. Simba wale walikuwa ni simba wenye njaa sana, ambao waliweza wakakaa wiki kadhaa, au hata mwezi bila kuona chakula chochote, na hata chakula kikiletwa  kilikuwa ni kidogo sana cha kuweza kuwatosheleza simba wote waliokuwa katika shimo lile, kwani chakula chao kilikuwa ni  wanadamu na si wanyama, hivyo ilikuwa mpaka aonekane mwanadamu muovu, ndipo simba hao wapate chakula.

Walifanya hivyo ili kuhakikisha kuwa mtu yeyote atakayetupwa huko ataliwa bila kubakishwa kitu chochote, mpaka mifupa yao kusagwa sagwa. Na ndicho walichomfanyia Danieli wakitazamia kuwa atakapotupwa, mara moja wale simba watamrukia, na kumpasua pasua angali akiwa bado juu, lakini tunaona Mungu alimtuma malaika wake na kuwafumba MAKANWA yao, (yaani midomo yao) wale simba.,..

Badala yake wao walipotupwa, biblia inatuambia simba wale walipokea angali wakiwa bado juu,(Danieli 6:24)

Je! Tunapata somo gani katika jambo hilo?

Mungu akifumba kinywa cha mlaji, hata kama ana njaa nyingi kwako, hawezi kula kilicho cha kwako..

Walaji sio simba tu, Mungu analo jeshi lingine la walaji, ambalo amelifananisha  ni tununu, nzige , parare na madumadu.. (Soma Yoeli 1:4) . Hawa wanaweza kuwa ni taifa, au jamii ya watu, au viongozi n.k. ambao Mungu anaweza kuwatumia kufunua makanwa yao kwako, wakakuharibu  kote kote bila kukuachia kitu, kama wewe si mtu wa haki, au ni mtenda dhambi. Utaona Mungu aliyaruhusu mataifa mbalimbali yaipige Israeli, na mengine kuwachukua utumwani kwa makosa yao tu ya kumwasi Mungu, ikapelekea makanwa ya wanadamu na mataifa kufunuliwa juu yao.

Na pia biblia inatuonyesha yapo mapepo ambayo yataachiliwa katika siku za mwisho yaliyofananishwa na nzige. Na hiyo itakuwa baada ya unyakuo kupita, na kazi yao itakuwa ni kuwauma wanadamu wote  ambao watakuwa hawana muhuri wa Mungu, juu ya vipaji vya nyuso zao.(Ufunuo 7:3). Kwa maelezo marefu juu ya habari hiyo fungua hapa>>> JINA LAKE KWA KIEBRANIA NI ABADONI,

Hata sasa, ibilisi anafunua makanwa yake na kuwameza , na kuwatafuna watu wengi pasipo wao kujua, biblia inasema….

1Petro 5:8 “Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze”.

Lakini walio na muhuri wa Mungu (yaani Roho Mtakatifu) kama vile Danieli, Mungu anawaepusha nao. Swali ni je wewe nawe umetiwa muhuri huu wa Mungu?(Waefeso 4:30). Kumbuka  Roho Mtakatifu hawezi kuja juu ya mtu ikiwa mtu huyo, hajatubu dhambi zake kwa kumaanisha kabisa kuziacha, na kubatizwa.

Hivyo ikiwa leo hii utapenda kumkaribisha Yesu ndani ya maisha yako au kubatizwa, basi fungua hapa kwa ajili ya kupata maelekezo ya sala ya Toba.>>>  SALA YA TOBA

Ubarikiwe.Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

DANIELI: Mlango wa 1

OLE WAKO KORAZINI NA BETHSAIDA.

UTAWALA WA MIAKA 1000.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 10 (Kitabu cha Zaburi).

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/12/01/makanwa-ni-nini-katika-biblia-danieli-622/