Ni madhara gani yatampata mtu yule anayetafsiri Neno isivyopaswa!

by Admin | 1 July 2021 08:46 am07

Jibu: Kuna hatari kubwa sana ya kulihubiri Neno isivyopaswa, Ni vizuri kulielewa Neno vizuri kabla ya kulifundisha.. Leo nitakuambia ni kwanini.

Miaka ya nyuma nikiwa bado ni mchanga katika Imani, nilikuwa natamani sana kuhubiri, kwasababu tu nilikuwa naona watu wanahubiri.. Hivyo na mimi, nilikuwa na shauku ya kuhubiri, hata ikiwezekana kuielezea biblia yote,. Hivyo hiyo ikanifanya, nisiwe na muda mwingi wa kulitafakari Neno, wala kulielewa sana wala kulichimba kwa undani, badala yake nilishika tu biblia na kuhubiri kwa jinsi nilivyolielewa Neno, nikiamini kuwa kila nitakachokisema kitakuwa ni cha Roho Mtakatifu!.. kumbe sikujua nilikuwa nafanya jambo la hatari sana kwangu.

Siku moja niliota ndoto nimekaa kwenye kiti, kama sehemu ya dining hivi,  halafu chini ya miguu yangu kuna kama sufuria inatokota maji, na miguu yangu ilikuwa ndani ya hayo maji ila nilikuwa sijui kama miguu yangu ipo kwenye hayo maji ya moto tena yanayotokota kabisa, kwasababu nilikuwa sisikii maumivu yoyote. Baada ya muda kukaja kama sahani mbele yangu ambayo ilikuwa na mchemsho wa nyama, ilipokuja ile sahani nikawa naanza kuzila zile nyama, zilipopungua nikawa kama nazivuta nyingine kwa chini, zinakuja juu ya hiyo sahani kubwa iliyopo mbele yangu..

Halafu baada ya muda wakaja watu Fulani mbele yangu ambao huwa nawahubiria..nikawa nawapa na wenyewe zile nyama wale…wakawa wanakula huku wanashukuru, wote tukawa tunafurahia mlo.. wakati hilo jambo linaendelea, nikajikuta naitazama miguu yangu, kumbe zile nyama nilizokuwa nakula na kuwalisha wengine zilikuwa ni nyama kutoka kwenye miguu yangu, hivyo zilivyokuwa zinazidi kwenye ile sahani ndivyo nilivyokuwa naimaliza miguu yangu. Baada ya hapo nikashtuka kutoka usingizini!, nikiwa na hofu!

Nikiwa kitandani natafakari maana ya hiyo ndoto!, Roho Mtakatifu akazungumza na mimi, na kuniambia… Ndivyo ninavyojimaliza mwenyewe kwa kuwalisha watu wake chakula kinachotoka katika akili zangu badala ya kutoka kwake!.

Tangu siku hiyo nikaacha! Kukimbilia kuhubiri kabla ya kuhakikisha kuwa jambo hilo halitoki katika akili zangu bali linatoka kwa Bwana. Nikajifunza kama jambo sijalielewa vizuri katika maandiko nitangoja mpaka nilielewe ndipo niwafundishe wengine!.. Nisije nikawalisha watu nyama kutoka katika mwili wangu mwenyewe.. Mwisho wa siku mimi ndiye nitakayepata madhara wa kwanza kabla ya wao!..

Hivyo Bwana alinionyesha hatari hiyo na tahadhari yake, na nikamshukuru sana mpaka leo, nazidi kuwa makini..

Hivyo ndugu!.. kamwe usihubiri, wala kufundisha wengine, jambo ambalo wewe mwenyewe hulielewi vizuri… ukifanya hivyo katika roho unajimaliza mwenyewe kabla ya kuwamaliza wale unaowafundisha.. Usiwe na haraka na utumishi!, bali keti chini kwanza kumtafuta Mungu, na kujifunza mambo kwa kina!

Jambo moja lisilojulikana na wengi ni kufikiri kuwa jambo la kwanza linalompendeza Mungu ni sisi kuhubiri!.. la! Nataka nikuambie jambo la kwanza linalompendeza Mungu ni sisi kukaa kujifunza(kuwa wanafunzi wake). Ndio maana ilibidi awaweke mitume wake chini ya madarasa kwa miaka mitatu kabla ya kuwatuma..

Jambo hili linawafanya wengi wairuke hatua ya kuwa wanafunzi wa Yesu.. vile vile inawafanya waruke kanuni ya vigezo vya kuwa mwanafunzi ambavyo Bwana Yesu alivisema katika…

Luka 14:27 “Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”.

Wengi tunairuka hii hatua, na kutaka kuwa waalimu, kabla hatujawa wanafunzi!..kumbuka huwezi kuwa mwanafunzi kama hujajikana nafsi, wala kuuchukua msalaba wako. Siku zote kumbuka hilo! Huwezi kuwa mwalimu kwa wengine kama wewe hujapitia uanafunzi..na huwezi kuwa mwanafunzi kama hukujikana nafsi na kubeba msalaba wako kumfuata Yesu.

Bwana atubariki na kutusaidia.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

INJILI YA MANENO LAINI ITAKUGHARIMU.

Kwa herufi gani kubwa nimewaandikia kwa mkono wangu mimi mwenyewe.

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

DAMU YA ZAKARI BIN BARAKIA.

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2021/07/01/ni-madhara-gani-yatampata-mtu-yule-anayetafsiri-neno-isivyopaswa/