Nini maana ya kuabudu malaika? (Wakolosai 2:18)

by Admin | 16 July 2021 08:46 am07

SWALI: Nini maana ya “kuabudu malaika”, kama tunavyosoma, katika Wakolosai 2:18?


Wakolosai 2:18 “Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu, kwa kunyenyekea kwa mapenzi yake mwenyewe tu, na kuabudu malaika, akijitia katika maono yake na kujivuna bure, kwa akili zake za kimwili”;

JIBU: Watu wa mataifa walipoipokea injili kwa mara ya kwanza kutoka kwa mitume, utakumbuka kuwa walitoka moja kwa moja katika upagani, na kuingia katika ukristo, Hivyo walikuwa hawana misingi imara sana ya kufahamu utendaji kazi wa Mungu  hususani pale Mungu anapozungumza kupitia malaika zake. Na tatizo hilo lilionekana sana sana kwa  watakatifu waliokuwa  Kolosai kwa wakati ule.

Walikuwa hawajui, kuwa Mungu anafanya kazi na malaika zake kwa ukaribu sana, kama vile biblia inavyosema wale ni wajumbe wanaotumwa kutuhudumia sisi tutakaourithi wokovu(Waebrania 1:14)… Sasa baadhi ya wakolosai pale walipoona Mungu anazungumza nao mara nyingi kupitia sauti za malaika zake, au maono.  wakadhani, malaika nao wana uungu mmoja na Kristo. Hivyo wakaanza kuwaabudu kama vile wanavyomwabudu Yesu Kristo.

Kama jambo kama hilo pia lilitokea kwa mtume Yohana alipokuwa kule Patmo akionyeshwa yale maono na Mungu kwa mkono wa malaika, mpaka na yeye akataka kumwabudu Yule malaika aliyesema naye, sasa jiulize ikiwa yeye ambaye ni mkomavu katika imani alijaribu kufanya hivyo  itakuwaje kwa watu wa mataifa walioamini siku sio nyingi? Ni rahisi sana na wao kuanguka katika makosa hayo..

Soma..

Ufunuo 22:8 “Nami Yohana ndimi niliyeyasikia na kuyaona mambo hayo. Na hapo nilipoyasikia na kuyaona nalianguka, ili nisujudu mbele ya miguu ya malaika yule mwenye kunionyesha hayo.

9 Naye akaniambia, Angalia, usifanye hivi; mimi ni mjoli wako, na wa ndugu zako manabii, na wa wale wayashikao maneno ya kitabu hiki. Msujudie Mungu”.

Soma pia Ufunuo 19:10, utaona tena jambo hilo hilo likijirudia tena.

Hivyo baadhi ya wakolosai waliingia katika makosa hayo, kama ilivyo sasa, kwa baadhi ya makanisa  kama Katoliki, ambao wanakuwa na maombi maalumu kwa ajili ya malaika walinzi waje kuwalinda. Jambo ambalo sio sawa, kwani maombi yetu yote na dua zetu zote, zinapaswa zielekezwe kwa Mungu tu peke yake, kupitia Kristo Yesu Bwana wetu na si mtu mwingine, aidha ni mtakatifu au malaika. Kufanya hivyo ni sawa na kuabudu sanamu.

Vilevile hii inatoa tahadhari, kwa kanisa hususani kwa manabii, ambao Bwana amewajalia neema ya kuona/kupokea ujumbe kwa Bwana kupitia malaika zake. Umakini wa hali ya juu unapaswa uwepo, wa kutowahusisha wajumbe hao na ibada yoyote. Bali wajue kuwa ni Kristo pekee ndiye anayestahili kuabudiwa, kwasababu hata malaika wenyewe wanamwabudu yeye. Tunachukulie tu kama wajumbe lakini sio kuwapa heshima kama ile ya Kristo mwenyewe.

Waebrania 1:6 “Hata tena, amletapo mzaliwa wa kwanza ulimwenguni, asema, Na wamsujudu malaika wote wa Mungu”.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya “saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa anamtolea Mungu ibada?”

Nini maana ya “saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa anamtolea Mungu ibada?”

Nini maana ya kuabudu?

Nini maana ya kumwabudu Mungu katika Roho na kweli?

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2021/07/16/nini-maana-ya-kuabudu-malaika-wakolosai-218/