Nini maana ya kuabudu?

Nini maana ya kuabudu?

Kuabudu ni nini?

Kuabudu maana yake ni “kufanya Ibada”.. Kitendo cha kufanya Ibada ndio “kuabudu”. .

Hivyo Ibada yoyote ile ni lazima ijumuishe vitu hivi vitano vifuatavyo.

  1. Kujifunza Maneno yake na kuyatafakari

Hii ndio sehemu ya kwanza na ya muhimu katika Ibada.. Na kumbuka kujifunza sio kukariri, bali ni kukaa chini na kuyachambua maandiko kwa uwezo wa Roho kama vile Mwalimu na mwanafunzi wanavyofundishana wakiwa darasani.

  1. Kumwimbia

 Hichi ni kipengele cha pili cha muhimu katika ibada, ambacho kinaweza kuwa katika mfumo wa kumshukuru Mungu na kumsifu kwa (Aidha tenzi za rohoni, au kwa nyimbo za sifa na kuabudu au vyote kwa pamoja)

  1. Kushiriki Meza ya Bwana

Hichi ni kipengele cha Tatu, na cha muhimu pia katika ibada…1Wakorintho 11:25 “Na vivi hivi baada ya kula akakitwaa kikombe, akisema, Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu; fanyeni hivi kila mnywapo, kwa ukumbusho wangu”.

  1. Maombi

Maombi yanajumuisha pia dua na sala..na ili ibada iwe ibada ni lazima kuwepo na kipindi cha maombi, wakati huu ndio wakati wa fursa ya kupeleka haja zetu kwa Mungu wetu.

         5 . Matoleo

Hichi ni kipengele cha mwisho kabisa, ambacho kinakamilisha IBADA. Biblia inasema (katika Kumbukumbu 16:16), kwamba tusiende nyumbani kwake, mikono mitupu. Matoleo ndio yanayokamilisha ibada. Hivyo mtu hawezi kusema leo nimekwenda kumwabudu Mungu bila kumtolea.

Hivyo mtu akivifanya vipengele hivyo vitano, katika ROHO NA KWELI,  Basi anakuwa amemwabudu wa kweli wa mbingu na nchi.

Sasa utauliza, je tunamwabudu vipi Mungu katika Roho na kweli?. Inamaana tuingie katika ulimwengu wa roho?

Ni muhimu kufahamu kuwa kuishi katika Roho sio kuishi kwa kuona mambo yasiyoonekana kama mapepo, au malaika, au kuona mbingu au kuona maono, hapana hiyo siyo tafisiri ya kuishi kwa Roho au kuabudu kwa Roho.. Tafsiri ya kuishi kwa Roho ni kuishi kwa kulifuata Neno la Kristo… Mtu yeyote anayeishi kwa kuyafuata maneno ya Kristo, huyo ni mtu wa rohoni asilimia mia, hata kama maisha yake yote hajawahi kuona ono hata moja, au hajawahi kuona malaika, wala mapepo. Kwasababu biblia inasema Maneno ya Kristo ndio Roho.

Yohana 6: 63  “Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu; MANENO HAYO NİLİYOWAAMBİA Nİ ROHO, tena ni uzima”.

Hivyo tunapomwambudu Mungu katika roho na kweli, maana yake ni kwamba tunafanya ibada kulingana na jinsi NENO LAKE linavyosema katika ukweli wote na usafi wa moyo.

Je umempokea Kristo?.. kama bado hujampokea na unakwenda kanisani tu kutimiza wajibu fulani, basi jua hapo huendi kumwabudu Mungu katika Roho na Kweli, hivyo hakuna baraka zozote za rohoni ambazo ulikuwa unazipata. Lakini leo ukiamua kutubu, na kuacha dhambi..Kristo ataingia moyoni mwako na kukuponya..na atakusafisha kwa damu yake, na kukufanya uweze kumwabudu Mungu katika Roho na Kweli.

Kama leo hii upo tayari kumpokea, basi fuatilisha sala hii fupi ya toba kwa kufungua hapa >> SALA YA TOBA.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Je! Mwanamke anapaswa afunikwe kichwa anapokuwa ibadani?

JE KUVAA PETE NI DHAMBI?

KUABUDU SANAMU/IBADA ZA SANAMU.

USIMWABUDU SHETANI!

JIFUNZE KULIGAWANYA VYEMA NENO LA MUNGU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
7 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Lucas
Lucas
11 months ago

Nimebarikiwa sana na somo

Gideoni Kassim
Gideoni Kassim
1 year ago

Jina la Yesu libarikiwe. Nauliza, Je, kunazo nakala za mafundisho yo yote? Nahitaji.

Gideon – Kenya

nelson bilinje
nelson bilinje
2 years ago

mungu awabariki sana kwa masomo haya