Moabu ni nchi gani kwasasa?

by Admin | 14 March 2022 08:46 am03

 1) Moabu ni nchi gani kwasasa? 2) Wamoabu walikuwa ni akina nani? 3) Na waamoni walikuwa ni watu gani na wa nchi gani?


1) Moabu ni nchi gani kwasasa?

Moabu ni Mji uliokuwepo maeneo ya nchi ya YORDANI kwasasa. Yordani ni nchi iliyopakana na Nchi ya Israeli kwa upande wa Mashariki.

2) Wamoabu walikuwa ni akina nani?

Asili ya Wamoabu na Waamoni ni kutoka kwa LUTU, aliyekuwa ndugu yake Ibrahimu (Baba wa imani). Mabinti wawili wa Lutu, walilala na Baba yao na kila mmoja kubeba mimba, Watoto hao waliozaliwa mmoja aliitwa MOABU na wa PILI aliitwa AMONI.

Mwanzo 19:30 “Lutu akapanda kutoka Soari akakaa mlimani, na binti zake wawili pamoja naye, kwa sababu aliogopa kukaa katika Soari. Akakaa katika pango, yeye na binti zake wawili.

 31 Yule mkubwa akamwambia mdogo, Baba yetu ni mzee, wala hakuna mtu mume katika nchi atuingilie kama ilivyo desturi ya dunia yote.

32 Haya, na tumnyweshe baba yetu mvinyo, tukalale naye, ili tumhifadhie baba yetu uzao.

 33 Wakamnywesha baba yao mvinyo usiku ule, akaondoka huyo mkubwa akalala naye, wala yeye hana habari alipolala wala alipoondoka.

34 Ikawa siku ya pili, mkubwa akamwambia mdogo, Tazama, nimelala jana na baba yangu, tumnyweshe mvinyo tena usiku huu, ukaingie ukalale naye.

35 Wakamnywesha tena baba yao mvinyo usiku ule, akaondoka mdogo akalala naye, wala yeye hana habari alipolala wala alipoondoka.

36 Basi hao binti wote wawili wa Lutu wakapata mimba kwa baba yao.

37 Yule mkubwa akazaa mwana, akamwita jina lake Moabu; huyo ndiye baba wa Wamoabi, hata leo.

38 Na yule mdogo naye akazaa mwana akamwita jina lake Benami; huyo ndiye baba wa Waamoni hata leo”.

3) Na waamoni walikuwa ni watu gani na wa nchi gani?

Kama tulivyosoma hapo Mwanzo 19:38, kwamba walikuwa ni kutoka uzao wa Lutu.

Taifa la Moabu ni moja ya mataifa yaliyolisumbua sana Taifa la Israeli, hususani katika safari yao ya kutoka Misri, utakumbuka Mfalme wa Moabu alimwajiri BALAAMU MCHAWI ili awalaani Israeli (yaani awaloge!).. lakini mpango huo ulishindikana!.

Bwana hakupendezwa na Taifa hilo, na alililaani.

Kwa maelezo marefu kuhusu Balaamu na uchawi wake unaweza kufungua hapa >> Balaamu mchawi

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

USIJITUMAINISHE JUU YA SIRA YAKO ANGALI UPO KATIKA DHAMBI.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

Ninawi ni nchi gani kwasasa?

Babeli ni nchi gani kwasasa?

KUSAMBAA KWA ROHO YA MPINGA-KRISTO.

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2022/03/14/moabu-ni-nchi-gani-kwasasa/