Je ni kweli ilikuwa desturi ya Bwana kuishika sabato?(Luka 4:16)

by Admin | 25 June 2022 08:46 pm06

Biblia inatuambia kuwa ilikuwa ni desturi ya Bwana Yesu kuingia hekaluni siku za sabato..Je! hiyo haimaanishi kuwa ni lazima na sisi tuishike sabato? (Luka 4:16)?.


Jibu: Tusome

Luka 4:16 “Akaenda Nazareti, hapo alipolelewa; NA SIKU YA SABATO AKAINGIA KATIKA SINAGOGI KAMA ILIVYOKUWA DESTURI YAKE, AKASIMAMA ILI ASOME”.

Bwana Yesu kuingia siku ya sabato katika masinagogi haimaanishi kuwa na yeye alikuwa anaiadhimisha au kuiabudu siku hiyo,  kama walivyokuwa wanafanya wayahudi..La!.. yeye ndiye aliyekuwa Bwana wa Sabato (Luka 6:5).. hivyo kamwe hakuwahi kuitumikia au kuiadhimisha sabato kama walivyokuwa wanafanya wayahudi.

Sasa kama ni hivyo, ni kwanini biblia iseme ilikuwa ni DESTURI YAKE kwenda hekaluni kila sabato?

Ni kwasababu siku ya sabato ndio siku ambayo wayahudi wengi walikuwa wanakusanyika hekaluni kusikiliza maneno ya Mungu, siku nyingine walikuwa wanafanya kazi…hivyo ili Bwana awapate ilikuwa hana budi awafuate hekaluni katika siku hiyo hiyo ambayo wao wanaiheshimu, lakini endapo wangekuwa wana siku nyingine ya kukusanyika hekaluni tofauti na hiyo sabato, basi ingekuwa ni desturi ya Bwana kuwafuata katika hiyo siku.

Ni sawa na mtu atenge siku moja ya jumamosi au jumapili, na kuifanya kuwa desturi yake kwenda kufanya UINJILISTI WA NYUMBA KWA NYUMBA!!.. Sasa kwa kuitenga hiyo siku haimaanishi kuwa anaiadhimisha hiyo siku.. bali anaitumia hiyo siku kufanya uinjilisti wa nyumba kwa nyumba kwasababu katika siku hizo watu wengi wanakuwa manyumbani, hivyo ni siku nzuri za kufanya uinjilisti, tofauti na siku nyingine za katikati ya wiki ambazo watu wengi wanakuwa katika shughuli zao, na si manyumbani.

Na Bwana Yesu, na mitume wengine wote walizitumia siku za Sabato kuingia katika masinagogi kuhubiri, si kwasababu wanaziadhimisha siku hizo, bali kwasababu katika siku hizo ndizo watu wengi wanakuwa wanapatikana katika majengo ya ibada.

Sasa swali lingine hili; Sabato halisi ni ipi? na ni siku gani tupasayo kuabudu? Ili kufahamu kwa urefu fungua hapa >> Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

IMESALIA RAHA YA SABATO KWA WATU WA MUNGU.

Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?.

Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2022/06/25/je-ni-kweli-ilikuwa-desturi-ya-bwana-kuishika-sabatoluka-416/