Miungu wasio na kikao pamoja na wenye mwili.

by Admin | 7 October 2022 08:46 pm10

SWALI: Wale wachawi walikuwa na maana gani waliposema..”Miungu wasio na kikao pamoja na wenye mwili”?.

Danieli 2:11

[11]Ni neno la ajabu, hili analolitaka mfalme, wala hapana mwingine awezaye kumwonyesha mfalme neno hilo, ila miungu, wasio na kikao pamoja na wenye mwili.


JIBU: Hiyo ni baada ya Mfalme Nebukadneza kutoa mtihani mzito wa kukumbushwa na kupewa tafsiri wa ndoto aliyoiota,..lakini tunaona wale wachawi wote walishindwa kupokea taarifa yoyote kutoka kwa miungu yao..ndipo wakakiri wazi kuwa fumbo hilo, si kila aina na mungu ilimradi mungu tu anaweza kulifichua, bali ni miungu wengine isiyofanya kikao na wanadamu.

Sasa hawa wachawi walitumia neno “miungu”..kwasababu waliamini katika miungu mingi, ndio màana utaona wanatumia neno miungu na sio Mungu asiyefanya kikao na wanadamu…lakini walimaanisha Mungu mmoja ( ambaye ni Yehova) yeye peke yake, ambaye huwa hafanyi vikao na wanadamu.

Sasa aliposema…asiyefanya vikao na wanadamu” maana yake ni kuwa asiyeishi pamoja na wanadamu..yaani Mungu ambaye makazi yake si duniani, bali ni mbinguni.

Miungu yote ya kipagani, makao yao ni hapa duniani, mizimu, mapepo, vibwengo, majini, n.k. vyote hivyo vinaishi katikati ya watu, na vinawategemea watu kutenda kazi zao..vinazurura zurura huku duniani kukusanya taarifa za matukio mbalimbali…havina kitu cha ziada zaidi ya kupeleleza peleleza, kama baba yao shetani (Ayubu 1:7)..

Haviwezi kujua mambo yajayo, haviwezi kutambua siri za ndani za mioyo ya watu..wakati mwingine hata vikitaka taarifa  fulani ya mtu vitakuambia niletee kwanza unyayo, au nywele, jinsi gani vilivyo vidhaifu, havijui, wala havipo kila mahali..na ndio maana wale wachawi walitaka kwanza wasimuliwe ile ndoto..ndio walau wakisie kisie tafsiri yake..

Lakini  Yehova peke yake ndiye ambaye hategemei, mwanadamu, au kiumbe chake chochote kufahamu au kutenda jambo alitakalo,  

Hii ni kutuonyesha kuwa Mungu pekee(Yehova) ndio tumaini la kweli, shetani au vipepo haviwezi kueleza hatma ya mtu. Unapotazama utabiri wa nyota, ujue kuwa umedanganyika, unapokwenda kwa waganga ujue kuwa ndio umekwenda kujitafutia matatizo, unapofanya mila na kuamsha mzimu, ujue unajifungulia milango mwenyewe wa kupelekwa kuzimu.

Zaburi 115:3-9

[3]Lakini Mungu wetu yuko mbinguni,  Alitakalo lote amelitenda.

[4]Sanamu zao ni fedha na dhahabu, 

Kazi ya mikono ya wanadamu.

[5]Zina vinywa lakini hazisemi, Zina macho lakini hazioni,

[6]Zina masikio lakini hazisikii, Zina pua lakini hazisikii harufu,

[7]Mikono lakini hazishiki, miguu lakini haziendi, Wala hazitoi sauti kwa koo zake.

[8]Wazifanyao watafanana nazo, Kila mmoja anayezitumainia.

[9]Enyi Israeli, mtumainini BWANA; Yeye ni msaada wao na ngao yao.

Amen.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Bwana aliposema kuwa yeye ni “Mungu wa miungu” alikuwa na maana gani?..je! yeye ni Mungu wa sanamu?

JE! PAKA KULIA USIKU NI ISHARA YA UCHAWI?

Kuwiwa maana yake nini katika biblia?

Wasamaria walikuwa ni watu gani?

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

ONDOKA YESU, TUACHIE MAPEPO.

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2022/10/07/miungu-wasio-na-kikao-pamoja-na-wenye-mwili/