Tajiri na maskini hukutana pamoja; BWANA ndiye aliyewaumba wote wawili.

by Admin | 15 October 2022 08:46 am10

SWALI: Nini maana ya huu mstari? 

Mithali 22:2

[2]Tajiri na maskini hukutana pamoja;  BWANA ndiye aliyewaumba wote wawili.


JIBU: Pamoja na kwamba kutakuwa na kutokuelewana baina ya makundi haya ya watu..Maskini atamwonea wivu tajiri, na tajiri atamdharau maskini..Lakini katika hayo yote bado tu kila mmoja atamhitaji mwenzake…atakutana na mwenzake mahali fulani tu katika maisha..

Maskini atamfuata tajiri ampe kazi, vilevile tajiri atamtegemea maskini amwoshee gari lake, amfulie nguo zake, amlimie bustani yake.n.k Hivyo kila mahali uendapo makundi yote utayapata .. Na sababu tayari biblia imeshaitoa..”Kwamba Bwana ndiye aliyewaumba wote wawili”Akawaweka hapa duniani..wala mmoja hakumweka mawinguni, mwingine ardhini.

Hii ni kufunua kuwa tumewekwa kusaidiana, wala hakuna mtu anaweza kujikidhi yeye mwenyewe kwa kile alichonacho pasipo mwingine..zaidi sana yule ambaye unamwona hakufai ndiye atakayekufaa sana wakati fulani. Kwasababu ni Mungu ndiye aliyetuumba sote, mmoja hakuumbwa na shetani, na mwingine Mungu.

Hivyo hekima inatufundisha tukae kwa utulivu, tuthaminiane sisi kwa sisi

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KWA KUWA WASEMA MIMI NI TAJIRI.

Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

Azidishaye mali yake kwa riba, Humkusanyia mtu awahurumiaye maskini.

JE! NINAWEZA KUPOTEZA FURAHA YA WOKOVU?

Mimi ni mweusi-mweusi, lakini ninao uzuri.

Vyombo vya uzuri ni vipi vinavyotajwa katika biblia?

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2022/10/15/tajiri-na-maskini-hukutana-pamoja/