Kama Kristo alizichukua dhambi zetu na kutusamehe kwanini kila siku tunatubu?.

by Admin | 23 February 2023 08:46 pm02

Jibu: Ni kweli Kristo alizichukua dhambi zetu kama biblia inavyosema katika kitabu cha Petro..

1Petro 2:24 “Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa”.

Lakini hiyo haimaanishi kuwa tumeshakamilika asilimia mia kwamba hatutakuwa na kasoro zozote kuanzia hapo na kuendelea…Kasoro chache chache na madhaifu machache chache bado tutaendelea kuwa nayo mpaka siku tutakapopata ukombozi wa miili yetu (Waefeso 4:30).

Wakati parapanda ya mwisho itakapolia hapo ndipo tutapata ukombozi wa miili yetu, na tutakuwa wakamilifu asilimia zote kwasababu tutapewa miili mingine isiyo na kasoro wala madhaifu.. lakini sasa ulimwenguni bado tupo katika mapambano, bado tupo vitani, bado ibilisi yupo, bado tutapitia vipindi vya kukosea vidogo vidogo, lakini si vya kutuangusha kabisa!!.. Kama kile Petro alichopitia wakati anakutana na Paulo kule Antiokia (Soma Wagalatia 2:11-14).

Vile vile tutapitia vipindi vya kuudhiwa, na kupata hasira, tutapitia vipindi vya kukosea kuongea, kukosea kutenda, tutapitia vipindi pia vya kuwakosa wengine pasipo kujua au kwa kujua, tutapitia vipindi vya kumkosa Mungu kwa kujua au kwa kutokujua n.k.. sasa kwa kasoro hizo zote tunazozibeba ni lazima tuwe watu wa kuomba rehema na toba mara kwa mara ili muda wote tudumu katika usafi na pia Bwana anyooshe mapito yetu..

Hiyo ndiyo sababu pia Bwana Yesu akatufundisha kuomba toba na rehema kila mara..

Luka 11:1 “Ikawa alipokuwa mahali fulani akiomba, alipokwisha, mmoja katika wanafunzi wake alimwambia, Bwana, tufundishe sisi kusali, kama vile Yohana alivyowafundisha wanafunzi wake.

2  Akawaambia, Msalipo, semeni, Baba [yetu uliye mbinguni], Jina lako litakaswe, Ufalme wako uje, [Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.]……………….

4 UTUSAMEHE DHAMBI ZETU, kwa kuwa sisi nasi tunamsamehe kila tumwiaye. Na usitutie majaribuni [lakini tuokoe na yule mwovu]”.

Kwahiyo ni lazima kuomba rehema na toba kila siku, kwasababu bado tupo katika mwili, na pia ni ishara ya unyenyekevu kwa Mungu.

Bwana atubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Fahamu Namna ya Kuomba.

JIRANI YANGU NI NANI?

Ni kwa namna gani, upendo husitiri wingi wa dhambi? (1Petro 4:8).

SALA YA BWANA. (Namna ya kuiomba)

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2023/02/23/kama-kristo-alizichukua-dhambi-zetu-na-kutusamehe-kwanini-kila-siku-tunatubu/