MSIWE NA UCHUNGU NAO!

by Admin | 6 April 2023 08:46 am04

Usiwe na Uchungu na Mke wako!.

(Masomo maalumu kwa Wanandoa)-UPANDE WA WANAUME/ MAJUKUMU YA WANAUME.

Neno la Mungu linasema..

Wakolosai 3:19  “Ninyi waume, wapendeni wake zenu MSIWE NA UCHUNGU NAO”

Hapo biblia imetoa maagizo mawili; 1)Kupenda na 2)Kutokuwa na uchungu.

1.Kupenda:

Kila mwanaume analo jukumu la kumpenda Mke wake kuanzia siku ile alipofunga naye ndoa mpaka siku ile kifo kitakapowatenganisha!. (Na hiyo ni Amri sio ombi). Tena anapaswa ampende kwa viwango vile vile vya kama Kristo alivyolipenda kanisa..

Waefeso 5:25  “Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake”

Kwahiyo kila Mwanaume ana wajibu wa kumpenda Mke wake siku zote za maisha yake… Ukiona upendo kwa mke wako unapungua, basi tafuta kuurejesha huo upendo kwa gharama zote!.(Jambo hilo linawezekana kabisa endapo ukimwomba Mungu, na wewe ukitia bidii katika kuurejesha upendo)

2. Kutokuwa na uchungu nao:

Amri ya pili waliyopewa wanaume juu ya wake zao, ni “KUTOKUWA NA UCHUNGU NAO” . Na mpaka biblia inasema “wanaume wasiwe na uchungu na wake zao” maana yake ni kwamba “wanawake wana mambo mengi ambayo wakati mwingine yanaleta machungu mengi”.

Kwamfano Matumizi mabaya ya Pesa… Hili ni moja ya jambo ambalo linaweza kumletea Mwanaume uchungu, hususani kama sehemu kubwa ya fedha anazitoa yeye, na pia tabia ya kuzungusha maneno ya siri ya familia kwa marafiki au kwa watu wasio na uhusiano wowote na familia,  jambo hili pia linaweza kuleta uchungu kwa mwanaume. Na pia tabia ya kurudia makosa yale yale, na tabia ya kutokusikia au kukosa umakini wa baadhi ya mambo na hivyo kusababisha hasara Fulani,  au kuwa wazito kufanya baadhi ya mambo, hizi zinaweza kuleta uchungu kwa mwanaume.

Lakini kwa sababu hizo au nyingine zozote, ni amri wanaume wote kutokubali uchungu ndani yao kwasababu ya kasoro hizo za wanawake.

Sasa Kwanini ipo hivyo?

Biblia imeweka wazi kuwa ni kwasababu “wanawake ni vyombo visivyo na nguvu”..

1Petr3:7 “Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, KAMA CHOMBO KISICHO NA NGUVU; na kama warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe”

Kwahiyo kama mwanamke ni chombo dhaifu, ni lazima tu kitakuwa hivyo siku zote!.. hivyo ni lazima kuchukuliana nacho katika hali hiyo.. Lakini usipokichukulia kama ni vyombo dhaifu, na kukifanya kuwa ni chombo chenye nguvu, basi utakuwa ni mtu wa kuumia moyo kila wakati, na kujikuta unakuwa mtu uliyejaa uchungu na hasira na hata kufikia kuwa mtu wa ugomvi na makelele ndani ya nyumba. Jambo ambalo ni dhambi!!

Waefeso 4:31 “UCHUNGU WOTE NA GHADHABU NA HASIRA NA KELELE na matukano yaondoke kwenu, pamoja na kila namna ya ubaya”

Hivyo ni wajibu wa kila mwanaume aliyeoa kutokuwa na uchungu na Mke wake.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

Neno “Uchungu wa mauti” lina maana gani kibiblia?

Mshahara wa Mbwa ni upi? Kama tunavyousoma katika Kumbukumbu 23:18

SHINA LA UCHUNGU, LISICHIPUKE NDANI YETU.

Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?

MAJARIBU 10 WANA WA ISRAELI WALIYOMJARIBU MUNGU.

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2023/04/06/msiwe-na-uchungu-nao/