Je! mtu anaweza kutamka Neno zuri au baya kwa akili zake na likaja kutokea ikiwa si Mungu?

by Admin | 2 September 2019 08:46 pm09

SWALI: Bibi yangu amenihadithia kuna Kaka yake mmoja alimuoa mke na akawa anamtesa na baadaye huyo kaka akaja kumkataa huyo mke baada ya kuzaa naye,Yule mke alipokuwa anarudi kwao Arusha alisema huyo Mume wake ataoa wake 1-12,kisha huyo wa 12 atakuwa kama fisi ammalize.Sasa baba huyo anaendelea kuoa leo mke huyu kesho yule kwasasa wameshafika takribani wake 6..Anaendelea..Swali je! Maneno yale ya yule mwanamke yanasimamiwa na Mungu au na Shetani?.


JIBU: Mtu yoyote akizungumza Neno kwa imani ni lazima litokee, uwezo huo Mungu amemuumbia mwanadamu ndani yake..Mwanadamu anaweza akaumba jambo lolote katika kinywa chake na likaenda kutokea kama lilivyo ikiwa atalifanya kwa imani.   Lakini Imani imegawanyika katika sehemu kuu tatu,..  

1.Imani inayotokana na Mungu, hii inakuja kwa kumwamini Mungu, na Neno lake, kwa mfano mtu anaweza kuamrisha ugonjwa utoke kwa Jina la Yesu, na ugonjwa huo ukatii, anaweza akatamka uzima kwa maiti na maiti ile ikarudia uhai,.Sasa imani ya namna hii ni ile imani ya Ki-Mungu na hii haina mipaka.  

2.Pili kuna imani inayotokana na shetani. Hii ni imani ile ambayo mtu anaweza akawa ni mchawi, au mshirikina au ana pepo fulani, kwa hiyo akizungumza Neno kwa imani, zile nguvu zilizopo ndani yake zinachanganyika na nguvu za giza kuhakikisha kuwa lile jambo linakwenda kutimia..kwa lugha ya sasa ndio unaweza ukasema mtu kalogwa au kafanyiwa jambo fulani la kichawi.  

3.Na tatu kuna imani ya mtu binafsi..hiyo haitokani na shetani wala Mungu..bali inatokana na nia ya mtu mwenyewe..kwamfano unapounyanyua mkono wako juu, hiyo ni roho yako unaunyanyua huo mkono kwa Imani, mkono wako lazima utii na kunyanyuka juu, vinginevyo usingenyanyuka kama maagizo yasingetoka rohoni, unapotaka kupaa mpaka mawingu, mpaka mwezini, ni jambo ambalo haliwezekani kwa namna ya kawaida, japo sasa mwanadamu hana mabawa lakini aliposema ninataka kufika kule juu, alifika kwa imani yake..sio Mungu wala shetani anayefanya hivyo ni wewe(roho yako)..Sasa kwa namna hiyo hiyo pia roho ya mtu inaweza ikazungumza jambo na likatimia vilevile, kama Mungu hataingilia kati..(Mathayo 17:20)   Mara nyingi Baraka za wazazi au laana za wazazi, huwa zinatokana na aina hii ya tatu ya imani, utakuta mzazi hamjui Mungu kabisa, wana hana habari yoyote na Mungu, lakini anaweza akambariki mtoto na mtoto anapata zile Baraka, au akamlaani na laana ile ikamfikia.

Kwahiyo kwa suala kama la huyo mwanamke kama sio Mkristo au kama hatumii nguvu za giza, basi inawezekana kaumizwa na tukio hilo sana na akaamua kuzungumza Neno lile la laana kwa Imani, na kama ni kama Mungu hatoliingilia kati basi ni lazima litimie.   Hivyo tuwe makini na sisi katika vinywa vyote, na ndio maana biblia inatushauri wakai wote tubariki wala tusilaani, maana hatujui maneno yetu tunayotoa yatakwenda kumuathiri yule kwa kiwango gani.(Warumi 12:14)

Ubarikiwe.


Mada Nyinginezo:

NJIA KUU YA KUINGIA KATIKA ULE MJI.

WATU WASIOJIZUIA.

KISASI NI JUU YA BWANA.

CHACHU YA MAFARISAYO NA CHACHU YA HERODE.

MAVAZI YAPASAYO.

DAMU YA ZAKARI BIN BARAKIA.

KWA MUNGU ASIYEJULIKANA.



Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2019/09/02/je-mtu-anaweza-kutamka-neno-zuri-au-baya-kwa-akili-zake-na-likaja-kutokea-ikiwa-si-mungu/